Waziri Sophia Simba - Mwenyekiti Mpya UW-CCM (Taifa)

Waziri Sophia Simba - Mwenyekiti Mpya UW-CCM (Taifa)

Suala hapo lipo kwa Tido ngoja tumsikilizie atafanya nini??akiruhusu goma lake hili...awashauri tu watulize mzuka wao.....kwani alikuwa hategemei?nafikiri wa kufanya party ya kushukuru MunguNna sadaka ni yule mwenyekiti uvccm maana hakutegemea na wala hakuwa wazo kabla.....
 
- Kutoka Secretary wa ofisi, kuwa girlfriend wa influencial politician, mbunge wa viti maalum, kugombea viti maalum na kukosa, kugombea viti vya mkoa na kutoswa pia, kujaribu kwa wananchi na kunyimwa pia, the next thing mbunge wa kuteuliwa na rais, na uwaziri juu wa kina mama na watoto, next waziri wa katika ofisi ya rais (Usalama na Takukuru) na sasa mwenyekiti UWT,

- Waziri ofisi ya rais utawala bora, mbunge wa kuteuliwa na rais, na mwenyekiti wa UWT vyeo vote hivi mama mmoja tu katika taifa lenye wananchi millioni 40! Kwakweli huyu ni role model!

Na ni only in Tanzania tu!

Lakini yeye si amefata role models wa waliomtangulia? Hivi mwenyekiti aliyemtangulia anaitwa nani? na yeye alifikaje ngazi za juu?
 
Janet Kaham alitumia close to 2 million USD na akashindwa kwa sababu ya ujinga wake wa kutaka kufuata sheria kichwa kichwa

Sasa pamoja na dhiki tuliyonayo hapa nyumbani ukweli ni kuwa TIDO (mdini) MHANDO keshapewa milioni 6 ili TBC kuonyesha jinsi Sophia Simba atakavyofanya pati la NGUVU la ushindi

Binafsi ningenyamaza lakini hii inaudhi wakati tunajua kuwa hizo pesa zingetumika kufanya mengi ya maana. Zaidi ya hayo pamoja na JANET kutoa hotuma ya kukubali kushindwa iliyojaaa uozo surely Sophia angeonyesha polital maturity kwa kuwa humble na kuwa kiunganishi baada ya balaa lakini wapi....


Kwa sie tunaojua alama za nyakati kila mtu anajua kuwa nguvu za kuteua watawala hazitokuwa tena kule wa central committee sasa whats the point ya kuwaste ma milioni yote haya wakati tunajua kuwa bunge linazidi kuwa na nguvu zaidi? bila kusahau jinsi serikali za liberal democracy zinavyoshika hatamu kila kukicha

I mean whats the point of this party wakti hata JK mwenyewe hakufanya pati ambalo hawa UWT wanataka kuifanya?

I dont care lakini nimeona bora niwa pre empt kusudi hii party isifanyike na pesa zitumike kwenye ya maana




GT,
Hiyo party ya 6m ni pati ya soda tu, mbona kidogo sana? let us be realistic, kunatatizo gani kwa kufanya pati ya 6m kama mwenyewe anamudu na yuko tayari kufanya hivyo?
 

GT,
Hiyo party ya 6m ni pati ya soda tu, mbona kidogo sana? let us be realistic, kunatatizo gani kwa kufanya pati ya 6m kama mwenyewe anamudu na yuko tayari kufanya hivyo?

siku hizi hata kwa sisi tunaoitafuta kama kuku wa kienyeji ...pati ya milioni 6..ni birthday party...inawezekana mmekosea ni pati ya milioni 60...but 6 million now days hardly you can intertain 100 pax.....thats why siku hizi hatufanyi fanyi party kwenye familia zetu kama zamani...
 
.....baada ya hizi pilika pilika itabidi huyu binti aende kucheki afya....asije akaanguka tena....ana kazi ngumu mbele yake na majukumu mazito katika vita dhidi ya ufisadi!!!!
 
Janet Kaham alitumia close to 2 million USD na akashindwa kwa sababu ya ujinga wake wa kutaka kufuata sheria kichwa kichwa
Sasa pamoja na dhiki tuliyonayo hapa nyumbani ukweli ni kuwa TIDO (mdini) MHANDO keshapewa milioni 6 ili TBC kuonyesha jinsi Sophia Simba atakavyofanya pati la NGUVU la ushindi

Game Theory

Ni vizuri ukawatendea haki sawa wote wawili hata kama umelalia upande mmoja. Kwa nini unatutajia kiasi alichotumia J Kahama lakini hutaji kiasi alichotumia S Simba?. Inasemekana SS ametumia kiasi kikubwa zaidi ya alichotumia Kahama. Let us be fair.
 
Huu uroho wa madaraka kwa SS wizi mtupu.
Jiuzuru madaraka mengine wizi mtupu.
Utavaaje kofia zote hizo wizi mtupu.
 

GT,
Hiyo party ya 6m ni pati ya soda tu, mbona kidogo sana? let us be realistic, kunatatizo gani kwa kufanya pati ya 6m kama mwenyewe anamudu na yuko tayari kufanya hivyo?

pundamilia07'
Hata kama ingekua ni 10,000/= (elfu kumi) kuna maana gani nzr ya kufurahi kwa kufanya sherehe unapochaguliwa au kuteuliwa kuwa kiongozi kwenye kundi la masikini wenye matatizo lukuki kama watanzania!!!!

Huwezi shawishika kufanya sherehe kama kweli unajua uzito wa mzigo uliobebeshwa kuongoza watu wa namna yetu!!

Tanzania sio dar!! wengi wanaona maisha ya watanzania wote wanaishi kama watu wa dar wanavyoishi!!

Anayeijua nchi hii vzr hawezi kutetea UJINGA kama huu wa kufanya sherehe kushinda uongozi!!
 
Quote:
"- Waziri ofisi ya rais utawala bora, mbunge wa kuteuliwa na rais, na mwenyekiti wa UWT vyeo vote hivi mama mmoja tu katika taifa lenye wananchi millioni 40! Kwakweli huyu ni role model!

Na ni only in Tanzania tu!"


Mkuu naona hili tatizo labda ni la kiafrika si Tanzania pekee. Majirani zetu hapo Rais wao ni Mbunge wa jimbo, Mwenyekiti wa chama na Amirijeshi Mkuu.

Besides SS ni "freelance" Mbunge kwa maana hana jimbo la kulitumikia wala kundi analoliwakilisha bungeni,.... that is, ubunge wa kuvuna tu bila kuwajibika!
 
Uanzishwe umoja wa Wanaume Tanzania.....wa CCM....!!!!
 

GT,
Hiyo party ya 6m ni pati ya soda tu, mbona kidogo sana? let us be realistic, kunatatizo gani kwa kufanya pati ya 6m kama mwenyewe anamudu na yuko tayari kufanya hivyo?
GT kasema Tido kapewa milion 6 ili aonyeshe hiyo pati
Sio gharama za pati ni 6m
 
GT kasema Tido kapewa milion 6 ili aonyeshe hiyo pati
Sio gharama za pati ni 6m

..ni kweli dada sofia simba ameamua kulipia airtime ili mapokezi yake ya dar es salaam ya TBC ......na tunavyoongea sasa ndio TBC wanaonyesha live mapokezi ya sofia mnazi mmoja...pamoja na kuwa mahudhurio sio makubwa...

....its seems haya ni special au kwa kuwa wenyeviti wa jumuia nyingine ,wazaai na vijana ..waliingia kwa mapokezi ya kawaida kabisa ..lakini naona haawa kina sofia wana pesa hadi zimebaki...inaelekea alikusanya pesa nyingi sana!
 
All politics are local! anachofanya Sophia ni kutake advantage ya pulicity iliyoletwa na Mama Kahama ya kulia lia rushwa ilhali na yeye katoa tena sana.

Mwacheni Mama ajimwae kwenye uwanja wake wa nyumbani. Kwenye siasa vikorombwezo vya mapokezi kama hayo vinakujengea territorial advantage.

Hivi leo mtu kufanyiwa mapokezi imekuwa nongwa? Zitto aliposimamishwa alizunguka akisukumwa na gari tena watu wakipokezana kama jeneza nchi nzima mbona hakuna alie lala pesa za kufanya yale zimetoka wapi.

Kamua Mama Sophy wakhti wako huu wenye wivu wajinyonge!
 
All politics are local! anachofanya Sophia ni kutake advantage ya pulicity iliyoletwa na Mama Kahama ya kulia lia rushwa ilhali na yeye katoa tena sana.

Mwacheni Mama ajimwae kwenye uwanja wake wa nyumbani. Kwenye siasa vikorombwezo vya mapokezi kama hayo vinakujengea territorial advantage.

Hivi leo mtu kufanyiwa mapokezi imekuwa nongwa? Zitto aliposimamishwa alizunguka akisukumwa na gari tena watu wakipokezana kama jeneza nchi nzima mbona hakuna alie lala pesa za kufanya yale zimetoka wapi.

Kamua Mama Sophy wakhti wako huu wenye wivu wajinyonge!

Miafrika ndiyo tulivyo. Nipeni kamba nikajinyonge.
 
naona ili sual limekubikwa na utata mtupu tokea wakati wa kampeni mara wameoneka mikumi inn guest...

kwa kuwa Wanawake wameamua kuongozwa hivyo basi wacha waendelee na fikra zao zilizoganda.

polytical analyst
 
Nimesoma mahala kuwa Sofia Simba alikutana na Kitwana na wakiwa wanafunzi wa Kikwete Chuo Kikuu cha Dar es salaam. Nadhani siyo kweli; huyu Sofia Simba alisoma na akina Lawrence Masha pale sheria akiwa "CHUA" mwishoni mwa miaka ya 80. Nadhani alikuwa intake moja na mama Sita au walipishana kidogo. Wakati huo Kitwana Kondo alikuwa ni Meya wa jiji la Dar na Kikwete alikuwa kwenye siasa siku nyingi sana. Inawezekana Mzee Kitwana Kondo alianza kumkamua mama huyu wakati angali akifanya huko MEIDA kabla ya kuingia chuo.

Ingawa ni kweli kuwa mama Sofia Simba "kashinda uchaguzi huo kihalali kulingana na taratibu za chama chake" yeye kama kiongozi alitakiwa atumie effort kubwa kuunganisha jumuia yake mara moja badala ya kuanza kujibarangua na mapati ya gharama ambayo yanazidi kusambaratisha jumuia yake hiyo. Angejifunze kwa mwenzake Obama aone jinsi alivyomtunza mpinzani wake mkuu Hilary, na yeye amtunze mpinzani wake mkuu Janeti ili wajenge jumuia yao. Angalia kuwa sehemu kubwa ya kabinet ya Obama imetokana na kabineti ya Clinton.
 
UWT kupanguliwa
Kaanaeli Kaale
Mwenyekiti mpya wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Sophia Simba, amesema ana mikakati ya kuubadilisha na kuuboresha umoja huo ili kwenda na wakati. Akizungumza katika hafla ya kumpongeza iliyofanyika jana katika viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam, Simba alisema ataunda kamati ambayo itasaidia kuleta mabadiliko hayo na kuufanya kuwa kimbilio la wanawake.

Alifafanua kuwa tofauti na viongozi waliotangulia, viongozi wa sasa wanafanya kazi kwa kuzingatia matakwa ya karne ya 21 ambayo yametawaliwa na changamoto nyingi zinazotokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia.

“UWT ilianzishwa mwaka 1962 lakini saa tupo karne ya 21 ... wengine wanaiita karne ya dot com,” hivyo nitafungua ukurasa mpya ndani ya UWT ili tuweze kwenda na mabadiliko ya kisasa,” Simba alieleza. Simba, ambaye ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora), alisema kazi kubwa ya umoja huo ni kutekeleza sera za CCM na kuhakikisha maisha bora kwa kila Mtanzania.

Alisema maisha bora yanaanzia katika familia na mtendaji mkuu katika familia ni mama, hivyo umoja huo utaanzisha programu zitakazowawezesha wanawake kuboresha familia zao. “Kama kila familia itakuwa na maisha bora, ni wazi kila Mtanzania atakuwa na maisha bora ... hivyo tutajipanga kuhakikisha mkakati huo unafanikiwa,” alisema.

Aliwasihi wanachama wa UWT kuvunja makundi na kufanya kazi kwa pamoja ili kufikia malengo na kutekeleza sera za CCM na kuongeza kuwa Umoja huo utaendelea kuwa na ushirikiano kama kawaida, ila utaongeza kazi ya kuleta maendeleo.

Alisisitiza kuwa ili Umoja huo uweze kufanikiwa, ni lazima viongozi wakubali kufanya kazi na wasomi pamoja na kuhakikisha kuwa idadi ya wanachama wa Umoja huo inaongezeka maradufu. “Wasomi watasaidia kuleta maendeleo ya haraka ndani ya chama, hivyo tusiwaogope kwani ni mabinti zetu na wamesoma kwa kutumia fedha zetu … nawasihi viongozi kuanzia ngazi ya kata kukaribisha wasomi hao,” alisisitiza.

Aliahidi kufanya kazi kwa uaminifu bila kubagua mtu yeyote kwani anaamini kuwa wagombea wote waliopambana naye wana uwezo na sifa za uongozi ila aliwashinda kwa kuwa Mungu alimchagua yeye kuwa kiongozi wa umoja huo. Simba katika uchaguzi huo uliofanyika Dodoma wiki hii, aliwaangusha Janet Kahama na Joyce Masunga.

Source: HabariLeo: Gwiji la habari Tanzania | UWT kupanguliwa
 
Back
Top Bottom