Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Makabidhiano hayo yamefanyika, leo Disemba 16, 2024 katika Ofisi za Wizara ya Ujenzi zilizopo Mtumba Mkoani Dodoma ambapo pamoja na mambo mengine Waziri Bashungwa amempongeza Waziri Ulega na kumusisitiza kuendelea kusimamia utekekelezaji wa miradi mbalimbali ya Sekta ya Ujenzi.
“Watumishi na Wataalam hawa ni wachapakazi, wanajituma usiku na mchana hata katika kile kipindi cha Mvua za El-Nino na Kimbunga Hidaya kilivyoathiri miundombinu ya barabara na madaraja, wataalam hawa walihakikisha wanarudisha mawasiliano kwa wakati”, amesema Bashungwa.
Naye, Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega amemshukuru Rais wa Jamhuri wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kumuamini na kumteua kusimamia Sekta ya Ujenzi na kumuahidi Mheshimiwa Rais kuendelea kutekeleza pale alipoishia mtangulizi wake.
Makabidhiano hayo yameshuhudiwa na Naibu Waziri wa Ujenzi Mhandisi Godfrey Kasekenya, Katibu Mkuu Balozi Mhandisi Aisha Amour, Naibu Katibu Mkuu Dkt. Charles Msonde, Menejimenti pamoja na watumishi wa Wizara ya Ujenzi.