Waziri Ummy Mwalimu: Maambukizi COVID-19 ya ndani kwa ndani yameanza, Watanzania wajiandae kwa maambukizi ya Jumuiya

Kama serikali hamna strategy,xia watu wasitoke mkoa kwenda mkoa kwa kibalimaalumu

Hilo ndio lingekua la msingi sio kuzuia Jambo fulani gafla wangekuwa na utaaratibu wa kuwaanda raia kwa maamuzi ya baadae... Mfano Kama watazuia raia kusafiri kwa siku kadhaa au kwa muda fulani watu wasitoke nje... Watoe taarifa mapema ili raia wajiandae.
 
Hali ishakuwa tete jamani
 

Asee na nipo hapa napiga senge laga moja. Ni kweli unachosema... acha nisepe home.
 
Ameongea kwa unyenyekevu kuonesha hatari inayoweza kujitokeza kuanzia wiki ijayo.

Binafsi nimeona kabisa akiwa anatarajia viongozi wa dini watatumia busara kubwa kuamua kuwepo kwa ibada ama lah.

Kufuata masharti ya distancing kwa vipimo vilivyowekwa kuanzia mita moja,ni jambo gumu pengine haliwezekani kabisa katika makanisa yetu.

Watu ni wabishi,wana kiburi cha uzima,wakiamini nchi za wazungu zimeadhibiwa kutokana na uasi wao,na hivyo kwetu sio rahisi hali kama ile kutokea.

Suala la kuvaa barakoa(mask) linaonekana sasa kupata nguvu sana.Na ametoa wito watu watakaotoka nje wavae barakoa ili kuzuia mambukizi kwenda kwa wengine ama wao kupata maambukizi.Je kanisani watu watavaa barakoa?

Ni hekma na busara tu za viongozi wa dini sasa zinatakiwa kwani naona serikali imewapa Uhuru.

Itakuwa vibaya kuruhusu watu wako wakusanyike na wapate maambukizi au wasambaze maambukizi yanayoweza kuleta maafa makubwa.

Mungu hadhihakiwi.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…