Waziri Ummy Mwalimu: Maambukizi COVID-19 ya ndani kwa ndani yameanza, Watanzania wajiandae kwa maambukizi ya Jumuiya

Waziri Ummy Mwalimu: Maambukizi COVID-19 ya ndani kwa ndani yameanza, Watanzania wajiandae kwa maambukizi ya Jumuiya

Tusiogope kama Wachina wamemudu immune muda mfupi vile Bongo tutaishi na corona bila shida. Limao, tangawizi na kitunguu swaumu ikibidi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dalili zilishaonekana sio nzuri, walikuwa wanajitahidi kutoa taarifa zenye mkanganyiko sasa hali imeshajidhihirisha, Corona Tanzania ipo, na ipo miongoni mwetu.

Tumuombe Mungu tu, hizo sanitizer tulizoweka kila mahali sidhani kama ndio suluhisho, mmarekani anaumizwa na Corona sidhani kwa sababu hawatumii sanitizer, kazi ipo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hizo barakoa zinatolewa wapi, maana sijashuhudia watu wakigawiwa. kwa nchi za ulaya na marekani wataalamu wameshapendekeza barakoa zivaliwe muda wote mtu akiwa kwenye public, tuseme daladala, sokoni, minadani, maofisini, benki,kanisani nk.
 
Hawa kuna kitu wanatuficha hasa kwenye takwimu za walioambukizwa huu ugonjwa nchini. Ngoja ngoma isambae watafichua wenyewe.
Nimefuatilia graph ya corona cases tanzania inaonyesha inapanda kwa watu 2 kila wanapotangaza wanatumia mbinu ya kuongeza watu 2 kila wanapotangaza, usije kushangaa wakitangaza tena ikiwa 27
 
Leo kwa maoni yangu ilitakiwa aongee Rais,Vice au PM ili kusitishe baadhi ya shughuli zenye muingiliano mkubwa,Ummy utakuwa unamuonea tu,namna alivyopata shida kuongea kuhusu viongozi wa dini utaelewa tu kuwa alikosa mamlaka fulani ya kusema direct kusitisha ibada zote.

Tunaingia kwenye hatari zaidi kwa sasa
 
Huu ndio wakati muafaka wa kujua uwezo wa viongozi wetu, nyakati za dhiki na taabu, siyo nyakati za bata, tukitulia vizuri tutaweza kuwajua viongozi wa kweli na wale wa mbeleko. Tuangalie sana kunena kwao na kutenda kwao nyakati hizi za covid 19

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Waziri wa Afya Ummy Mwalimu akiongea na viongozi wa dini, amesema kuwa kwa sasa hali ya ugonjwa wa Korona nchini imebadirika kutoka kuletewa ugonjwa na watu kutoka nje imegeuka kuwa hali ya kuambukizana sisi wenyewe kwa wenyewe.

Wakati huo Waziri Ummy ameonya kuwa ndani ya muda mfupi ujao maambukizi yatageuka kuwa maambukizi ya jumuia(Community Transmission), akawataka watanzania wajiandae kwa hali hiyo.

MY TAKE:
Tuliwaambia mapema kabisa, Fungeni hii mipaka ya nchi mtatuletea janga, lakini tukaendelea kujivutavuta sasa tunakwenda kwenye hali ngumu sana

Tumeona juzi hapa mtu katoka Dubai tarehe 24 March kashuka Dar, kisha tukasikia kaenda mwanza tarehe 29 March alipopimwa na kukutwa na Korona, huyu mtu ilikuwaje hakuwekwa karantini?

Kwa hiyo ina maana Kwenye Karantini hatukuwa serious na pia kwenye kufunga borders hatukuwa serious, sasa matokeo yake huenda tukaingia kwenye hali ngumu

Kiufupi serikali haiwezi kukwepa lawama hali ikigeuka na kuwa mbaya nchini.

Saa hivi hao wachina tuliokuwa tukiwapokea kwa bashasha pale KIA kipindi wapo kwenye hali ngumu sasa hivi wamefuta residence permit na viza za foreigners walio nje ya mipaka ya nchi yao na wanawasumbuasumbua foreigners walio nchini mwao kwa sasa kwa kuwabagua na kuwafanyia kila aina ya ubaguzi kuwa eti ndo wanawapelekea New cases, Wanawanyima hoteli, kuingia kwenye supermarkets,Weusi wakipanda mabasi wachina wanashuka. Sasa najiuliza Je sisi wema wetu wa kufungua mipaka kipindi kile umetuletea nini zaidi ya kuhatarisha maisha ya watu wetu?

Msikilize Ummy Mwalimu hapa akiongea
View attachment 1413820
Magufuli priority yake ni pesa,uhai wa wanyonge wa nchi hii si issue kwake? Sometime huwa najiuliza, tunataka Magufuli afanye kitu gani ndo tujue hstufai
 
Magufuli priority yake ni pesa,uhai wa wanyonge wa nchi hii si issue kwake? Sometime huwa najiuliza, tunataka Magufuli afanye kitu gani ndo tujue hstufai
Labda aanze kutuniga mmoja mmoja mpaka kufa live TBC, ila vinginevyo ni chaguo sahihi atatuvusha salama
 
Duh, ina maana huyu waziri hakugundua hilo mapema? afukuzwe kazi imemshinda
Sasa angefanyaje wakati rais na naibu rais wanatuhimiza tutoke kukapige kazi serikali ipate Kodi? Yaani wakati Kenya mwisho kutembea ikiwa saa moja jioni bongo hapa tunazitaka bank zipige kazi hadi saa mbili usiku ili serikali ikusanye kodi
 
Back
Top Bottom