Waziri Ummy Mwalimu: Maambukizi COVID-19 ya ndani kwa ndani yameanza, Watanzania wajiandae kwa maambukizi ya Jumuiya

Waziri Ummy Mwalimu: Maambukizi COVID-19 ya ndani kwa ndani yameanza, Watanzania wajiandae kwa maambukizi ya Jumuiya

Zile wiki mbili nadhani sasa zinaelekea kutimia,huu ndo wakati hasa wa ku apply safe distance na kuosha mikono.

Nimegundua kwenye uoshaji mikono wahudumu mfano wa maduka, bar etc hawaoshi mikono kabla na baada ya kumuhudumia mteja mmoja.

Wakati wait ndo wanakamata pesa kutoka kila mtu, hii Ni hatari maana mfano uko bar,umeagiza beer,umenawa, muhudumu kakufungulia bia,kumbe mikono yake imeshika pesa za mtu mwingine na iko taitend, anaacha virusi kwenye chupa,wewe unakamata chupa unakunywa huku unaperusi mtandaoni, bila kujua umeshika virus na umehamishia kwenye simu.

Unamaliza bia unalipa,unanawa na kuondoka huku ukiperusi,umesahau Sasa simu Ina virus,unapeleka virus kwako,unaingia ndani unashika kitasa cha mlango, umeacha virus.

Unashika chupa ya chai,umeacha virus,hivyo yeyote atakaeshika hizo sehemu anaingia kwenye mlolongo
Mkuu tuombe radhi,pesa yetu ni ya quality ya hali ya juu sana haiwezi sambaza virusi vya corona.mdudu akigusa tu either anakufa au anateleza na kudodoka by BOT
 
Kama Mh. Mwalimu waziri wa Afya alivyosema maambukizi yamehamia kuwa ya ndani, ninamshauri na kumuomba Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, aliangalie suala la mikusanyiko ya nyumba za Ibada kwa mapana.

Kiukweli nyumba za Ibada zinapaswa kuacha kuendelea kukusanya waumini ikizingatiwa mikusanyiko ni moja ya njia za kuongeza maambukizi kwa umma. Ushauri wangu mikusanyiko ya nyumba za Ibada izuiwe. Mh. Rais unaweza kuwaita viongozi wa Imani tofauti na kuwaeleza hili kabla hali haijawa mbaya!
Unamuomba

huyu au mwingine?
 
Hatujachelewa Sana,kinachohitajika full lockdown hasa miji mikubwa dar,mz,Arusha,mbeya kwa mda wa siku 14,hii itazuia maambukizi mapya na wale walioambukizwa hizo siku zinatosha ugonjwa kuwa incubated na hivyo watajulukana na kuwa isolated
Mkuu wanaccm walikuwa wanasema watanzania ni wabangaizaji ukiweka total lockdown utawaua wote kwa njaa,so acheni uvivu kapigeni kazi
 
Ameongea kwa unyenyekevu kuonesha hatari inayoweza kujitokeza kuanzia wiki ijayo.

Binafsi nimeona kabisa akiwa anatarajia viongozi wa dini watatumia busara kubwa kuamua kuwepo kwa ibada ama lah.

Kufuata masharti ya distancing kwa vipimo vilivyowekwa kuanzia mita moja,ni jambo gumu pengine haliwezekani kabisa katika makanisa yetu.

Watu ni wabishi,wana kiburi cha uzima,wakiamini nchi za wazungu zimeadhibiwa kutokana na uasi wao,na hivyo kwetu sio rahisi hali kama ile kutokea.

Suala la kuvaa barakoa(mask) linaonekana sasa kupata nguvu sana.Na ametoa wito watu watakaotoka nje wavae barakoa ili kuzuia mambukizi kwenda kwa wengine ama wao kupata maambukizi.Je kanisani watu watavaa barakoa?

Ni hekma na busara tu za viongozi wa dini sasa zinatakiwa kwani naona serikali imewapa Uhuru.

Itakuwa vibaya kuruhusu watu wako wakusanyike na wapate maambukizi au wasambaze maambukizi yanayoweza kuleta maafa makubwa.

Mungu hadhihakiwi.


Sent using Jamii Forums mobile app
Makanisa na misikiti isitishe ibada zao kwa muda
 
Iliporipotiwa kesi ya kwanza ya uwepo wa mgonjwa wa Corona, kama kawaida yetu tukaanza kumsingizia Mungu atalinusuru taifa letu ili kukwepa kuingia gharama za ziada ktk kukabiliana na gonjwa hili. Tulisikia uropikaji wa wanasiasa eti hatuwezi kuzuia wageni kuja nchini kwa sababu ya tamaa ya fedha za kigeni.

Kuna msemo ktk lugha ya Kiingereza usemao, "Truth is stranger than fiction", nafikiriki ndipo hasa walipokwana viongozi wetu na wale wafuasi wao wenye kupenda kusifu na kuabudu tu. Nahisi akili sasa zitaanza kuwarudi na kuchukua hatua stahiki ili kuokoa maisha ya wananchi.

Ni vyema Jiji la DSM likaingia kwenye karantini mara moja, ili watu wasiweze kuingia ama kutoka kwa siku angalau 21.

Sent using Jamii Forums mobile app
Tutakosa Kodi,Kuna watu hawatalipwa mishahara
 
Ameongea kwa unyenyekevu kuonesha hatari inayoweza kujitokeza kuanzia wiki ijayo.

Binafsi nimeona kabisa akiwa anatarajia viongozi wa dini watatumia busara kubwa kuamua kuwepo kwa ibada ama lah.

Kufuata masharti ya distancing kwa vipimo vilivyowekwa kuanzia mita moja,ni jambo gumu pengine haliwezekani kabisa katika makanisa yetu.

Watu ni wabishi,wana kiburi cha uzima,wakiamini nchi za wazungu zimeadhibiwa kutokana na uasi wao,na hivyo kwetu sio rahisi hali kama ile kutokea.

Suala la kuvaa barakoa(mask) linaonekana sasa kupata nguvu sana.Na ametoa wito watu watakaotoka nje wavae barakoa ili kuzuia mambukizi kwenda kwa wengine ama wao kupata maambukizi.Je kanisani watu watavaa barakoa?

Ni hekma na busara tu za viongozi wa dini sasa zinatakiwa kwani naona serikali imewapa Uhuru.

Itakuwa vibaya kuruhusu watu wako wakusanyike na wapate maambukizi au wasambaze maambukizi yanayoweza kuleta maafa makubwa.

Mungu hadhihakiwi.


Sent using Jamii Forums mobile app
Zenji naona wameshatangaziwa kufunga misikiti
 
Tumeambiwa na Waziri wa Afya, Mhe,Ummy Mwalimu kuwa ugonjwa wa corona unaweza kuambukizwa kwa njia ya hela hii maana yake kunawa mikono pekee hakutoshi na sasa tumeanza kusisitizwa tutumie mask(barakoa).

Swali linakuja,watanzania wangapi wamepata taarifa hii mpya na ni wangapi watakuwa wameandaa mask za kuvaa wanapoenda kwenye nyumba za ibada hasa siku ya kesho watapomiminika katika makanisa kwa Ibada ya Ijumaa kuu?

Kutokana na taarifa hii mpya na kwa kuzingatia tahadhari tuliochukua ni ya kunawa mikono tu kabla ya kuingia katika nyumba zetu za Ibada,nashauri serikali ichukue maamuzi magumu ya kuzuia ibada zote kwa muda(kuanzia kesho) kama walivyozuia mikusanyiko mingine, vinginevyo huko mbeleni tutakuja kulaumiana na serikali ndio itakuwa ya kwanza kulaumiwa unless janga hili halitakuwa tishio hapa nchini.

Tutambue wenzetu huko Ulaya sasa wanatembea na mask hivyo tusijichukulie kirahisi jambo hili.

Tusisubiri mazingira ya ugonjwa yatulazimishe kuchukua tahadhari fulani fulani, bali tutumie mazingira ya ugonjwa kuona umuhimu wa kuchukua tahadhari hizo angali mapema.

Majuto ni mjukuu;maji yakimwagika,hayazoleki.
 
Ibada inafanyika mara moja kwa wiki kwa muda wa masaa yasiyozidi mawili halafu mnasema zisitishwe! Mbona masoko yako wazi siku zote kwa masaa hadi kumi na mbili kila siku lkn hamsemi yafungwe?

Vv

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Utakuwa mganga wa kienyeji bila shaka.

Maana nilisikia ibada huwa zinawaharibia mizimu yenu
 
Huyu mama anajaribu kuwazuga Watanzania sasa kama anakiri ugonjwa umeletwa kutoka nje kwanini saivi aseme tunaambukizana wenyewe kwa wenyewe sio kutoka nje tena??,, Sasa kama ni ivyo lawama zitaendelea kubaki kwao kwanini waliruhusu apo kabla wageni kuingia kuleta maradhi? sasa anajaribu kuleta lawama kwa watanzania nadhani ameongea kauli mbaya sana na kuna jambo linafichwa fichwa watanzania amkeni
 
Back
Top Bottom