Waziri Ummy: Rushwa sekta ya afya inatisha imefika hatua Daktari anamuomba rushwa Daktari mwenzake. Nashauri JKCI ihamie Mloganzila

Waziri Ummy: Rushwa sekta ya afya inatisha imefika hatua Daktari anamuomba rushwa Daktari mwenzake. Nashauri JKCI ihamie Mloganzila

Unafikiri hakuna walimu wanaopokea 1.5 milion?
Hakuna wote wanaoanza wanaanzia na D1 kwa degree wakat dactar anaanza na E1 kwa degree na mpaka afikie hiyo kupokea 1.5 daktar aliyeanza nae takuwa anapokea mara 2 yake
 
Ndogo Sana lingana na KAZI zao ,lakini pia na masomo yao, Sasa Mbunge anaechukua mil 10 plus ,ni ya nini? alafu wanasiasa hacheni porojo kwa watu Hawa, afya ni idara ambayo hapatakiwi siasa, mpaka mlisha lazimisha watu kujifukiza, yani leo pesa ya madafu 1.5 m ni pesa kweli hacha watupige
Hata akipokea 10 au 14 kama wazr mbona bado wanaopokea hyo wanakula rushwaaa
 
Hii ni sehemu tu ya nchi hii ilivyo kwa sasa, yaani sio kwenye afya tu. Kuna watu walidanganyika wazungu waliposema eti rushwa imepungua nchi hii. Ni uwongo kabisa.
 
Waulize KWANZA wabunge huko wao hawali rushwa pamoja na pesa zote walipwazo, ukishapata jibu njoo tupigane spana, ma doctor hawali rushwa bali hupata takrima, binafsi Kama doctor ametoa huduma nzuri KWa mgonjwa wangu, nikampa hata laki mbili Kama ahukrani utasemaje ni rushwa? Iyo nitakrima,
Hata akipokea 10 au 14 kama wazr mbona bado wanaopokea hyo wanakula rush
 
Waziri wa Afya Ummy Mwalimu amesema rushwa katika sekta ya afya imefikia hatua mbaya kwani sasa madaktari wanaombana Rushwa hata wao kwa wao

Waziri Ummy amesema hili halikubaliki kabisa

Aidha Waziri Ummy ameishauri bodi ya Kituo cha moyo cha Jakaya Kikwete kuhamia Mloganzila ambako wanaweza kujenga Hospitali kubwa na ya kisasa zaidi

Chanzo: ITV
๐Ÿฅฒ๐Ÿฅฒ๐Ÿฅฒ๐Ÿฅฒ๐Ÿฅฒ๐Ÿฅฒ๐Ÿฅฒ๐Ÿฅฒ๐Ÿฅฒ๐Ÿฅฒ๐Ÿ™ƒ poleni sana ma Dakitari. Kumbukeni sisi watanzania wanyonge tunawapenda mno, msife moyo iko siku atapatikana mtetezi wenu na hivyo vihela mnavyosimangwa navyo hamtavitamani tena.
 
Mfumo wa utawala ndo umepalilia rushwa acha kushoboka na madaktari, eboo? nyie mawaziri kamba zenu mlizoambiwa na hangaya mjipimie zina urefu kiasi gani? tuanzie hapo kwanza......
 
Ametudhalilisha sana sisi madaktari,ngoja aumwe tutampa dose ya UTI huku anaumwa amoeba
Madarakani ni binadamu kama wengine,sio kwamba kila daktari ni msafi.
Na sio kweli kwamba daktari anafanya kazi kuliko mwalimu au mkulima,tena udaktari wa leo ni mwepesi sababu ya mitambo ya kupimia na kusaidiwa na mitandao.
Sio muda mrefu tutakuwa na madaktari maroboti ya AI,ambayo kwanza hayabahatishi kazi yao ipo sahihi mno,hayagomi wala kudai mshahara wala hawana sikukuu.Lazima madaktari mtafute kimbilio jipya .
 
Madaktari wanaombana vipi rushwa wao kwa wao, wanakuwa na shida gani hao jamaa mpaka waombane rushwa?
Maana yake ni kuwa, Daktari huyu akipiga dili fulani la rushwa huku mwenzie akimwona basi huyo mwenzake naye lazima aombe gawio la rushwa hiyo..!
 
Kisu kimeingia kwenye mfupa. UVCCM ni kusanyiko la wadokozi,malaya na wenye kila aina ya tamaa. Nilikudaka kijinga sana kuwa makini next time.
Sio kosa lako. Ni mwaka uliozaliwa na malezi ya smartphone.
 
Sasa bibi ummy anashangaa au anatupa taarifa..? Na kwanini ashangae..?Taasisi/sekta zote zilivyo jaa uozo/madudu/ujinga na upumbavu toka kitambo,HAKUNA CHA SHANGAZA AMA KUPIGWA NA BUTWAA HAPA.
 
Waziri wa Afya Ummy Mwalimu amesema rushwa katika sekta ya afya imefikia hatua mbaya kwani sasa madaktari wanaombana Rushwa hata wao kwa wao

Waziri Ummy amesema hili halikubaliki kabisa

Aidha Waziri Ummy ameishauri bodi ya Kituo cha moyo cha Jakaya Kikwete kuhamia Mloganzila ambako wanaweza kujenga Hospitali kubwa na ya kisasa zaidi

Chanzo: ITV
  • Kuna taasisi imelalamikiwa sana kutotimiza wajibu wake, hii ni dhahiri sasa inatakiwa ifutwe - PCCB
  • Hii inakwenda kuichafua Ikulu na vyombo vyake very soon - where are the whatch dogs?
  • Rushwa katika sekta ya afya ni ishara kuwa wagonjwa wengi wasio na uwezo kifedha watapoteza maisha
 
Back
Top Bottom