Harry Mapande
Senior Member
- May 18, 2020
- 109
- 363
Nadhani madaktari wanaopaswa kulaumiwa hapo ni wa kitengo cha emergency ambapo kwa nyakati za usiku wao ndio huwaona wagonjwa na kuwastabilize kabla ya kuwapeleka katika wodi husika.So emergency team ya hapo Mwananyamala means haikuwepo? Kuanzia wauguzi na madaktari? Kama ni hivyo basi hapo kuna shida.Wajaribu kuiga au kutengeneza emergency department kama za muhimbili upanga au Mloganzila...i have been there..wanafanya kazi nzuriHuu ni udhaifu, hata kama angekuwa mmoja, hiyo ni hospitali ya rufaa haiwrzekani wafanye uzembe kama huo. Uzembe unaweza kuwa wa daktari au uongozi kwa kushindwa kuweka madaktari wa kuweza kusimamia changamoto za wagonjwa kama zinavyojitokeza.
Ukimsikiliza waziri wao anaongea utagundua kinachofanyika hospital za serikali hakifikii hata 30% ya kile wanapaswa kufanya
Mkuu hapana. Hospital zetu nazijua sana. Pamoja na kuwa serikali haiwalipi vizuri na mazingira yao ni magumu sana lakini nao wana sehemu yao ya uzembeNafikir umeshindwa kumuelewa watoa huduma ni wachache sio kwamba anahalalisha serikali iajiri fikiria hapo kuna dokta moja tu na watu walikuw wa 5 kweli asife hata mmoja?
Hizi kelele alipiga sana jamaa mmoja anaitwa Dr Ulimboka enzi za Kikwete. Matokeo yake akatekwa na kupigwa karibu kuuawa. Wananchi badala tuungane kum-suport tukabaki kushangaa.Serikali iboreshe huduma za afya,maslahi ya watumishi yaongezwe,haiwezekani wanasiasa ,wabunge na wengineo wajilipe mishahara mikubwa huku kada nyingine zikiwa hoi...
ILA WATOA HUDUMA ZA UMMA TUJITATHIMINI,
MH. MAGUFULI HAWA WATU WAMEANZA KUJISAHAU HEBU ILE KAMBA YA CHUMA ULIYOWAFUNGA 2015 HEBU IFUNGE TENA MWAKA 2021 TUMBUA TUMBUA HAWA WATU MH RAIS...
Mkuu hapana. Hospital zetu nazijua sana. Pamoja na kuwa serikali haiwalipi vizuri na mazingira yao ni magumu sana lakini nao wana sehemu yao ya uzembe
Sasa kwanini tuamue kufanya hivi kwa watu ambao ni hawakupaswa kufanyiwa vitendo kama hivi,Ishinikizeni Serikali iboreshe maslahi ya watumishi hao, iboreshe pia upatikanaji wa vitendea kazi alafu ndio uwalaumu.
Hao unaowalaumu kwa uzembe hapo ( kwe hospitali za umma) ndio hao hao wanatumiwa na hospitali binafsi ambazo unasifia huduma zao.
Ukiona kazi haikulipi achana nayo usilazimishe,ILA WATOA HUDUMA ZA UMMA TUJITATHIMINI,
MH. MAGUFULI HAWA WATU WAMEANZA KUJISAHAU HEBU ILE KAMBA YA CHUMA ULIYOWAFUNGA 2015 HEBU IFUNGE TENA MWAKA 2021 TUMBUA TUMBUA HAWA WATU MH RAIS.
Nimependa hii aya yako,Ila tambua kuwa watoa huduma hawa wamedharauliwa,wamenyanyaswa,wamefedheheshwa sana sana na mtu huyo kwa kutowapa HAKI na STAHIKI zao za MSINGI kabisa za kisheria.
1 Annual increment
2Madaraja na vyeo
3Malimbikizo
Zinafanyika siasa katika HAKI zao.
Walimu,madaktari,wauguzi,maaskari n.k wamefanya Kazi miaka 5 na 6 sasa inaelekea bila bila.
"Show me your brutality I will show you blood suckers"
Nireteeni gwajima!
Au nasema uongo ndugu zangu?
Kuna kazi za wito inabidi watu waambiwe na si kuweka maslahi mbele mkuu hizi huduma wanapata wengi maskini na matajili waliokuwa nacho na wasiokuwa nacho.Umemaliza yote Mkuu.... Inasikitisha Sana kuona Watanzania wenzetu wakishupaza misuli ya shingo kuwalaumu Watumishi wa imma wa nchi hii huku wakishindwa kabisa kuwasapoti kudai hayo maslahi yao..... Mwaka wa sita Sasa bila maboresho ya maslahi yao,na Kuna maeneo mengine huko kwe hospitali za halmashauri madaktari wanaofanya ON CALL DUTIES hawalipwi allowances zao kwa madai kuwa pesa hakuna,huku wakilazimishwa kuendelea kufanya kazi.
Hawa watumishi wa umma ,ni binadamu wenzetu ambao wanahitaji maslahi bora ili waweze kuendesha maisha yao ya kila siku. Bila kujali maslahi yao, hawawezi kuwa na utulivu unaotakiwa kutimiza majukumu yao.
Niwashauri tu ,Watanzania wenzangu tuache kuwalaumu Watumishi wetu wa umma, badala yake tupaze sauti kuitaka serikali ya Rais Magufuli kuheshimu na kujali maslahi yao ili wawe na utulivu,furaha ya kufanya majukumu yao, watuhudumie vema.
Sasa kwanini tuamue kufanya hivi kwa watu ambao ni hawakupaswa kufanyiwa vitendo kama hivi,
Kama unaona maslahi hamna tujaribu kuwaachia wenye wito wakufanya kazi hizi wafanye
Watu wasio na hatia wanaumia nachosisitiza
Usiombee hili likukute
Kuna kazi za wito inabidi watu waambiwe na si kuweka maslahi mbele mkuu hizi huduma wanapata wengi maskini na matajili waliokuwa nacho na wasiokuwa nacho.
Kwahiyo unaona akirudi ndo atamaliza tatizo. Tupunguze mihemko. Mbona hatujiulizi kwanini wahumu wa Afya wamefikia hapo?Naomba nieleze hili ambalo kwenye Moyo wangu siwezi kuliacha kamwe na sintolisahau katika mwaka uliopita linalohusu hospitali ya Mwananyamala.
Mnamo Tarehe 30/12/2020 nilimsaidia majeruhi wa pikipiki ambaye alikuwa amegongwa na gari kumuwahisha hosptali kwa ajili ya Matibabu, aligongewa mitaa ya Sinza , so awali tulifika hosptali ya Palestina then palestina kwaissue ya mgonjwa ilivyo walituambia twende hosptitali ya Mwananyamala.
Hapa ndio msingi wa Jambo ambalo nataka kuwasilisha kwenu wanajamii,
Tulipofika hosptali ya Mwanayamala majila ya saa Nne usiku tuliandikisha kadi pale Reception Then tukaenda ili tuonane na daktari, tulipofika pale tuliambiwa vyumba vinavyotoa huduma ni No 3 na No 5 lakini havikuwa na mtu,
pale pembeni pakusubilia wagonjwa tulimkuta Mama mjamzito mmoja amekaa,
ilibidi tumuulize daktari kaenda wapi,
Alitujibu yeye alipofika majira ya saa mbili daktari alikuwa anatoka kwenye chumba No 5 so aliniambia anarudi ,hadi muda huu Saa Nne hajarudi,
duuh kwanza hilo lilitushtua kuona mama Mjamzito kafika Muda wote huo na bado hajapata huduma ilibidi tukae tumsubilishe mgonjwa wetu tukimsubili daktari,
Muda ulienda ,waliongezeka watu kadhaa pale nao wakiwa seriously kidogo ilibidi tusubili hapo muda unaenda saa tano ,
Watu uzalendo ukawashinda ikabidi kila mmoja aanze kuongea kwa Jazba kidogo,
Mimi nikiangalia kushoto kwangu kuna mtu anaumwa mbavu hapumui vizuri kulia huku kuna mtu vidole vimechanika nikimwangalia mgonjwa wangu huku naye Mguu umevunjika analalamika daaah nikasema kimoyo moyo duuh hii ni hatari sasa,
Huku nikiendelea kuwaza mara ghafla aliingia Jamaa kamuweka mtoto kwenye mikono yake miwili ya mbele wanaandikisha kadi wapo haraka haraka akiwa na mama cjui kama ndio alikuwa mama wa mtoto sikujua kabisa ,
wakafika moja kwa moja kufungua mlango chumba cha kwwnza hamna mtu chumba cha pili nacho hmna mtu kama nusu saa hivi wanahangaika kumtafuta daktari ,
tulipomuangalia mtoto yule tukaona analegea kabisa ilibidi tuanze kupiga kelele pale jamani dakatri ,mara tukamuona kuna jamaa anadeki kavaa kama nguo za manesi tukazani muhusika kumbe alikuwa nimfagizi wa pale akawaambia wale waliokuja na mtoto Nendeni emergence napo emergence hamna mtu wakarudi tena ikabidi twende Reception kugomba pale mara wakapiga simu wakaongea sijui na nani mara akaja Nesi pale na daktari ikabidi sisi wote tusubili
Wale wenye mtoto waanze,
kufungua malango kuingia ndani kwa daktari wakakaa kama dakika Moja mara mama anatoka ndani anaanza kulia,
Mtoto alikuwa kashafariki tena mikononi mwao kwa kukosa huduma ya Mapema ,mtoto wa miaka 9 au 8 maskini alipoteza uhai wake mikononi mwao wazazi wake ,
Wote tuliumia sana Huzuni ilikuwa imetawala kubwa sana tena sana mahali pale .
Haikuishia hapo baada ya kutoka nilikuwa nikisikia kuna Mzee mmoja wa makamo alimfwata yule daktari nikisikia Maongezi yao kwa nje pale ,
Mzee alimwambia Yule daktari hivi kuwa
Kazi anayofanya siyo kazi yakuweka Maslahi mbele , Udkatari ni kazi ya Wito kutoka kwenye Moyo wako nasi vinginevyo sikuyamwisho ya hukumu atajibia hichi kitendo walichofanya leo mzee aliongea aya flani za kiislamu sikuweza kuzielewa maneno niliyosikia ndio hayo .
Nini nachotaka kuwasilisha kwenu kwanza kwa Watanzania na Kwa waziri wa Afya
Kwa waziri wa Afya jaribu kupitia hizi hosptali zako za serikali zinashida sana tena sana Hasa nyakati za usiku nakuachia wewe hili.
Kwa Watanzania Wenzangu kama unauwezo na umepata emergence issue nyakati za usiku kabisa please napenda kusema usimpeleke mgonjwa wako katika hosptali za serikali Nenda private kama unachochote mfukoni kama hauna haina Jinsi tujibane hivyo hivyo humu
ILA WATOA HUDUMA ZA UMMA TUJITATHIMINI,
MH. MAGUFULI HAWA WATU WAMEANZA KUJISAHAU HEBU ILE KAMBA YA CHUMA ULIYOWAFUNGA 2015 HEBU IFUNGE TENA MWAKA 2021 TUMBUA TUMBUA HAWA WATU MH RAIS.
Nimevutiwa na hoja yakoNdugu, hii kauli ya eti "ni wito" isiwe kisingizio Cha kuminya maslahi ya hao watu, tambua na wao Wana familia za kuzihudumia.... Wito bila utulivu wa fikra haiwezekani.
Cha msingi ni kwa sisi Wananchi tunaoumizwa na hayo badala ya kuwalaumu watoa huduma hao, tuishinikize serikali iboreshe maslahi yao plus mazingira wanayofanyia kazi ili wasiathiriwe na msongo wa mawazo unaotokana na ugumu wa maisha ili watuhudumie vizuri.
Huyo anaishi enzi ya zama za mawe za mwanzo. Kazi ya wito ndo kazi gani? Na kazi gani sio ya wito?Hakuna kazi ya wito siku hizi ndugu,hata hao watu wa dini wamegeuka wajasiriamali siku hizi....FUTA KABISA HIYO "MENTALITY"
Da,Hawa wahudumu wa afya ni wajinga,kwani kama wanadai ongezeko la mshahara wangetumia taratibu sahihi.Ni dhambi kusababisha mtu apoteze maisha,hiyo laana hawataikwepa.Wajirekebishe.Mbona hapo kuna unafuu njoo hapa mawilayani dakitari anapatikana siku mbili tu kwa wiki, ukipata emergency akikisha inangukia siku ya dakitari, ukiwa huna bahati basi unapoteza maisha au unatafuta private kwa gharama kubwa
Hizi changamoto watu hawaelewi kabisa...tangu nianze kazi hosp flan ya serikali natimiza mwaka sasa sijawah pata on call allowance hata moja...na mshahara ulikuw wa november..na hii ndio january...ila tunaendelea kufanya kazi kwa kuw ni wajibu wetu despite na mazingira husikaUmemaliza yote Mkuu.... Inasikitisha Sana kuona Watanzania wenzetu wakishupaza misuli ya shingo kuwalaumu Watumishi wa imma wa nchi hii huku wakishindwa kabisa kuwasapoti kudai hayo maslahi yao..... Mwaka wa sita Sasa bila maboresho ya maslahi yao,na Kuna maeneo mengine huko kwe hospitali za halmashauri madaktari wanaofanya ON CALL DUTIES hawalipwi allowances zao kwa madai kuwa pesa hakuna,huku wakilazimishwa kuendelea kufanya kazi.
Hawa watumishi wa umma ,ni binadamu wenzetu ambao wanahitaji maslahi bora ili waweze kuendesha maisha yao ya kila siku. Bila kujali maslahi yao, hawawezi kuwa na utulivu unaotakiwa kutimiza majukumu yao.
Niwashauri tu ,Watanzania wenzangu tuache kuwalaumu Watumishi wetu wa umma, badala yake tupaze sauti kuitaka serikali ya Rais Magufuli kuheshimu na kujali maslahi yao ili wawe na utulivu,furaha ya kufanya majukumu yao, watuhudumie