Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu: Wagonjwa 37 wamethibitishwa kupona virusi vya Corona na wameruhusiwa kwenda nyumbani

Ni wakati mwafaka kwa serikali ya Kusadikika kujitokeza na kuitangazia dunia kuwa hakuna covid 19 katika nchi hiyo

Tunashukuru waziri kutuambia wamebaki wagonjwa 70 tu,ambao kesho na keshokutwa watakuwa wamepona,hii ni habari njema sana

Naiomba Serikali iruhusu wanafunzi warudi shule,zile hostel za jina la Rais nadhani sio karantini tena, wanachuo warudi chuoni wakasome angalau wale wa miaka ya mwisho wakamalizie Semista

Nitashangaa kuwa mpaka sasa kuna mkoa una karantini,sijui ili iweje

Tunashukuru serikali kwa kudhibiti hivi virus,sasa vimeanza kutokomea kabisa,nahis baada ya siku tatu hatutakuwa na mgonjwa

Mungu ibariki serikali

Mungu ibariki nchi yangu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa hivi itakuwa inatangazwa waliorecover tu. Ukisikia mgonjwa ni mmoja ama wawili.

Baada ya ile idadi 89 kutangazwa na watu kuanza kumshambulia rais akashtuka na ndiyo lengo LA mkutano wake wa juzi kupiga biti.

Haya yote hayaondoi kasi ya maambukizi na vifo hata serikali ikiendelea kuficha uhalisia. Na hii ni kwa sababu hakuna jipya linalofanywa kuthibiti maambukizi.

Hivyo ni swala la kila RAIA kujipambania..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii ni baada ya ushauri wa kuanza kutumia tiba asili ya kufukiza, sasa endeleeni kubeza. Safari hii lazima mabeberu waje kujifunza kwetu
Wala si kwa tiba asili. Hawa walitibiwa kwa madawa mchanganyiko wakiwa hospitalini. Na wametoka..
Hakuna mahali wametumia miti shamba

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yani toka ugonjwa uingie mpaka ile juzi waliopona walikua ni 11 tu

Ila sasa toka juzi mpaka leo yani siku mbili tu waliopona ni 37 ! Ni maajabu haya

Kwa hiyo ulihitaji kusikia vifo zaidi au! Unazungumziaje ongezeko la ghafla la wagonjwa siku kadhaa zilizopita? Je ulihoji idadi ya wagonjwa kuongeza ghafla?
 
Najuta kuunga mkono hoja ya kutofunga mipaka hapo nyuma, nilijua serikali ina mkakati wa kupambana


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Naona mvuke wa Muarobaini na tangawizi unaponya kwa haraka sana. Viva JPM!
 
Kutokana na yale maneno ya juzi na Mkwara ingemlazimu tu atangaze hivi.

Iwe uongo au kweli, lazima atoe taarifa zinazomridhisha Mfalme.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ummy hajamwelewa boss wake. Alitakiwa kutangaza wagonjwa wote wamepona na hakuna maambuzi mapya.
 


Hakuna maambukizi mapya hakuna kifo[emoji4]


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mweka mada ulimpata wa kukaanae karantini au ulimkosa hasira ndo umehamishia kwa serikali ya kusadikika..??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…