DOKEZO Waziri wa Elimu, huu mtindo wa Kubakiza watoto shuleni wakati wa likizo ni Sahihi?

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Kuna mtu anakuambia jumatatu hadi jumapili za mwezi mzima akae na watoto nyumbani eti wanapumzika huo ni ujinga
Kama ni jumatatu hadi Ijumaa za siku za likizo wapumzike pia.. Maana likizo zenyewe wanapewa fupi ni muhimu Watumie kupumzika lakini in a controlled environment. Sio kwa kuwa wapo likizo basi ni TV na games sijui simu kuanzia mawio hadi machweo. Lazima kuwe na utaratibu mzuri nyumbani wa shughuli za watoto.
 
Sijaelewa,aliyetoa agizo ana shida gani?
 
Unaongea kitu usichokielewa,mtoto wa darasa la nne anafanya mtihani November leo June unataka abaki shuleni kufanya nini?

Suala la kusema akimaliza atakuwa na muda mrefu nalo unaongea bila kufikiria,huyu ameshasoma mfululizo miezi mingi kichwa kinahitaji mapumziko ili kiweje kurudi katika ubora wewe unataka umjaze tena vitu,kitaalamu haikubaliki hio
 
Labda kama umesoma miaka ya tisini huko hivyo unaweza kusema mwanafunzi akili inakua imechoka kwa hizo siku kadhaa.
Ila kwa tuliosoma miaka ya 2000's hilo jambo sio la kushangaza.

Na pia mtoto hasomi kama alivokua anasoma kipindi cha kawaida, mara nyingi masomo yanaisha saa 6 au 7 mchana kukiwa na kipindi kirefu cha mapumziko.
 
Ni sawa ila hata kubadili mazingira ni vizuri,wanapaswa kuondoka maeneo ya shule
 
Mliosoma hiyo miaka ya 2000 ndio shida ilipoanzia
Shule ndioi zilianza kukaririsha watoto na kuondoa likizo
Wamekaririshwa tu notes darasani hakuna skills zozote wamepata
Hata kupika tu watoto wetu hawajui kisa kukaa shule
 
Huu ni mtaji hasa kwa shule binafsi, kama kweli wana nia ya kumaliza mtaala kwann wawe wanaongeza gharama kinyume na ada au wamalize ndan ya mda uliopagwa. Kukomesha huu ubadhirifu au wizi au unyonyaji vyovyote utakavyoitwa, ni kutunga sheria ya kuzuia hili, na sio matamko kila siku, huku shule sikijificha kwa kusema wazazi wamekubali, wazaz hawakubali ila unakuwa kama unalazimishwa tu
 
Mliosoma hiyo miaka ya 2000 ndio shida ilipoanzia
Shule ndioi zilianza kukaririsha watoto na kuondoa likizo
Wamekaririshwa tu notes darasani hakuna skills zozote wamepata
Hata kupika tu watoto wetu hawajui kisa kukaa shule
Nyie wa miaka ya 90 mmelifaidisha nini taifa kama sio uchawa tu kwa serikali iliyo madarakani.
Wengi wenu mmepewa UDc ona mnachofanya, upigaji umeongezeka tu hamna kitu ni yaleyale.

Na hilo la kukaririshwa sio kweli. Na likizo haijafutwa ipo palepale.
 
kwan hapa shda ni kuenda shule likizo ama ada ongezi ya kusomea likizo

hii kimsingi nahisi ni ada kama ela yko ni ya mawazo

mpeleke government skul kijana wko elimu ni bure tuh na mtoto atafunga skul kulngana na mwngozo wa serkal....!!


unless otherwise tafuta mwlmu amfunze mwanao nyumban

anaeza kuw anasoma sku 3 tu za wki nyngne analalia

mgongo apumzke vzur.

kwnza wazaz wng vijana wao wakrud nyumban ndy wnawahangaikia wasome tuishen hapo anaend kupmzka wp ....

ukiona uhangaiki na elimu ya mwnak ujue unabeti na hali hii ndy inafnya watot wng wanaosoma serkalni kufeli wazazi wanachangia asilimia 35 ya hilo

kupumzka n muhimu ila mtot hata akipumzka wki mbil sio haba sana dunian hatujaja kupumzka zaidi sna mapumzko yamillele ni kaburini....

nitoe RAI kama unahela za mawazo mwnao mwache asome

government on your own risk ila tu jitahd kumfatilia na

matuishen ya likizo sivyo unaanza mechi aggregate ya 0-1

kuishia form 4 n swala la chap unless dogo ajielew mwnyw.... hii ni kwa risk takers

tusiopenda risk wengne tuztafute hela tuwalipie watoto private skul na ada ongez pia fresh tu tulpe si kw elimu ya vijana wetu hapa winning probabilty ni 75%

TUACHE KULALAMIKUA UJINGA
HUNA HELA PELEKA MWANAO SERKALINI FULL STOP

SIO KILA KTU SERKAL IINGILIE KATI UPUUZ HUU

ITAKUJA WATU BADAE WAJE WAIOMBE SERKAL IPUNGUZE NA ADA ZA FEZA WATOTO WAO WASOME...

Huna pesa tafuta njia nyngne mtot atoboe punguza lawama.... weng watoto wa maskni wametoboa kw matuisheni mitaani na mabro mashulen FULL STOP
 
Ni kweli wao wanasema tumekubaliana wakati si kweli,wao wanakuandikia tu ki note kwamba tunaomba uchangie,kwanini sasa wasimalizie muhula kwa gharama ya ada niliyolipa?nyongeza ya nini wakati mimi nililipa ada ili wao wamalize muhula?

Hapa inatakiwa kutungwa sheria tu kama ulivyosema.
 
We huelewi hata unachokizungumza,unadhani kwa hela pekee unaweza kumjenga mtoto?tunazungumzia haki ya mtoto kupumzika na kujifunza vitu nje ya darasani,we anasema kupumzika ni kaburini,mbona kazini unachukua likizo kwanini usiende kupumzika kaburini sasa?

Hili ni suala lilifanyiwa tafiti sio porojo za kuokoteza mitaani kama unazoleta hapa.

Labda nikupe taarifa tu,baada ya kuandika huu Uzi tayari serikali imeshachukua hatua ,ina maana inakubaliana na hiki kilichosemwa hapa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…