MR TOXIC
Senior Member
- Jun 4, 2019
- 190
- 525
Nimefuatilia kwa ukaribu mjadala unaoendelea kwa sasa kuhusiana na kauli iliyotolewa na mkuu wa mkoa wa dodoma mheshimiwa Mtaka kuhusu kuanzisha makambi ya kitaaluma kwa wanafunzi.
Katika mjadala huo nimesikitishwa sana na maoni ya wadau mbali mbali wanaomnyooshea kidole Waziri wa Elimu Prof. Joyce Ndalichako.
Huyu mama ni mchapakazi mzuri mwenye misimamo isiyoyumbishwa hasa tunapokuja kwenye suala la elimu tangu alipokuwa katibu wa baraza la taifa la mitihani(NECTA).
Lakini tangu apewe dhamana ya uwaziri wa elimu mama wa watu amekuwa akizodolewa hapa na pale kwamba hafai muda mwingine kwa makosa ambayo siyo yake.
Mfano kwenye suala la usimamizi wa elimu, mama ndalichako anasimamia elimu kwa ngazi ya vyuo vya kati na vyuo vikuu huku usimamizi wa elimu ngazi ya msingi na sekondari ukiwa chini ya TAMISEMI ambayo inaongozwa na Ummy Mwalimu.
Cha kushangaza kwenye hili saga la Mkuu wa Mkoa anayelalamikiwa ni Ndalichako lakini watu wanasahau kwamba hilo jukumu la usimamizi wa elimu kwa sasa lipo chini ya tamisemi ambayo inaongozwa na waziri ummy kwahiyo kama ni lawama wanaopaswa kulaumiwa ni TAMISEMI, mama ndalichako anaonewa tu.
Katika mjadala huo nimesikitishwa sana na maoni ya wadau mbali mbali wanaomnyooshea kidole Waziri wa Elimu Prof. Joyce Ndalichako.
Huyu mama ni mchapakazi mzuri mwenye misimamo isiyoyumbishwa hasa tunapokuja kwenye suala la elimu tangu alipokuwa katibu wa baraza la taifa la mitihani(NECTA).
Lakini tangu apewe dhamana ya uwaziri wa elimu mama wa watu amekuwa akizodolewa hapa na pale kwamba hafai muda mwingine kwa makosa ambayo siyo yake.
Mfano kwenye suala la usimamizi wa elimu, mama ndalichako anasimamia elimu kwa ngazi ya vyuo vya kati na vyuo vikuu huku usimamizi wa elimu ngazi ya msingi na sekondari ukiwa chini ya TAMISEMI ambayo inaongozwa na Ummy Mwalimu.
Cha kushangaza kwenye hili saga la Mkuu wa Mkoa anayelalamikiwa ni Ndalichako lakini watu wanasahau kwamba hilo jukumu la usimamizi wa elimu kwa sasa lipo chini ya tamisemi ambayo inaongozwa na waziri ummy kwahiyo kama ni lawama wanaopaswa kulaumiwa ni TAMISEMI, mama ndalichako anaonewa tu.