Waziri wa Fedha, Dkt. Nchemba: Nchi inayoendelea lazima ikope

Waziri wa Fedha, Dkt. Nchemba: Nchi inayoendelea lazima ikope

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760


NCHI INAYOENDELEA LAZIMA IKOPE

"Duniani kote nchi zinazotekelea miradi mikubwa ya maendeleo na zenye uchumi mkubwa, zina madeni makubwa, ipo hivyo nendeni mkaangalie

Huwezi linganisha uchumi wa Tanzania na Marekani,” - Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba

Kuna nchi masikini hazina madeni na hazikopesheki, watu wajue kadiri unavyotekeleza miradi mikubwa ndivyo deni lako linavyokuwa, hivyo ni uchaguzi wako tu

Mfano Tanzania kabla ya kuunganisha barabara zote deni lilikuwa chini ya Bilioni 10 tu

Leo hii tunafurahia 4G na 5G lakini mkongo wentu wa taifa tumetengeneza deni. Miradi ya aina hiyo ni mingi

Watanzania wajue deni la taifa ni tofauti na fedha za kwenye ATM, deni ni mikataba inayosainiwa na fedha zitaingia kulingana na mikataba

Kuna madeni tumemalizia kulipa ya Awamu ya Kwanza, nimesaini kulipa deni ambalo lilikopwa sijazaliwa, yapo madeni ya Awamu ya 2, 3, 4 na 5 na tunakopa sasa yataipwa baadaye

Anayekopa siyo Rais, inakopeshwa Serikali na hakukopeshwi kwa awamu

Mikopo ya muda mrefu ndio inayotakiwa ina masharti nafuu kuliko ya muda mfupi, mfano mkopo wa Bwawa la Mwalimu ilishasainiwa, mradi unaendelea na tunaendelea kupokea fedha zake

Mikopo ya SGR tunaendelea kuipokea fedha

Fedha ya mkopo haitoki siku moja, zinapoendelea kuingia ndivyo deni linavyokua

Tumepata mkopo wa UVIKO19 ambao hauna riba, huwezi kuuacha kwa kuwa watangulizi walishakopa na deni limeshakuwa kubwa, pia huwezi kuacha kukopa kuogopa deni

Niwahakikishie hakuna mkopo unaolipwa kwa matumizi ya kawaida wala kwa matumizi ya mishahara au posho, ni kwa ajili ya miradi ya maendeleo

Hatuwezi kuachia mradi njiani, deni la Serikali uwiano wake na pato la taifa tupo 31%, ukomo ni 55%

Deni la nje kwa uwiano wa pato la taifa tupo 18% ukomo wake ni 40%, deni la nje kwa mauziano ya nje 142% ukomo wake ni 180%

Rais anapotafuta mikopo anazingatia ile ya masharti nafuu na inayoenda katika miradi muhimu
 
Waziri wa fedha amefafanua kwamba inakopeshwa serikali na sio Rais.

Sasa sitaki kusikia tena mkisema Rais kakopa.
 
Lakini wabunge wanaowakilisha wananchi ndani ya mhimili utasikia wanasema "namshukuru raisi/mama kwa kunipatia zahanati, barabara n.k" wakati ni serikali imekopa.
 
'…Fedha za Rais Samia…, Mama katuletea Billion 7 za kuboresha Madarasa …'

Itumike sasa Serikali imeleta fedha …'

inakopeshwa Serikali au inakopeshwa Nchi?

Serikali ya Daruso inaweza kukopa IMF?

kuanzia 2015 tulianza ku personalize Kazi za Dola na ndio 'pasi ' ilipotelea hapo …Mtu wa kwanza kukemea hadharan mbele ya Waasisi wa Tabia hii alikuwa Hayati Mzee Mkapa …akapuuzwa
 
Tulianza kupoteza dira awamu ya 5 kumtukuza MTU zaidi ya Katiba.
 
Kama hakopeshwi Rais, mbona kila fedha mnasema katoa Rais!? Huyo Rais ana mfuko mkubwa kiasi gani!?
 
Rais ndo serikali yenyewe hasa na nembo ya uwailishaji huko Duniani.na Mihimili yake ni jeshi.Mahakama.polisi.usalama! Nk.sasa msijaribu kuropoka tu na kutuchanya km mabwege tusiojua kitu.......hata huyo Mwigulu amedandia tu siasa hajui kitu.....km Rais siyo serikali ni nani saa Raia au???
Amuombe radhi Rais faster.....
 
Huu mjadala ni wa kijinga wachangiaji wote hawakusoma....km wamesoma basi walinunua mitihani na haya ndo madhara yake.....
 
Waziri wa fedha amefafanua kwamba inakopeshwa serikali na sio Rais.

Sasa sitaki kusikia tena mkisema Rais kakopa.
Na pia hahutaki kusikia yale mapambio eti Rais ametoa pesa bilioni kadhaa kufanya jambo fulani!.
Pesa sio zake ni za serikali.
 
Back
Top Bottom