TANZIA Waziri wa Fedha, Dkt. Willliam Mgimwa afariki dunia!


Nyongise ulonzile mbegali, tukangalage kuno twilumba..
 
Tumwombee roho yake ilazwe pema.Na pia awaongoze wanaoteua mwingine watuletee mtu mzalendo kwani wakati huu ni Mgumu tusitengeneze epa nyingine
 
Nimepokea taarifa ya kusikitisha.

Mzee wetu na mjomba wangu, Dr. William Mgimwa amefariki dunia asubuhi hii
Baada ya kufuatilia vyanzo vya uhakika, niliwataarifu TBC ambao hawakuwa na habari yeyote mpaka nilipokuwa nazungumza nao. Ninashukuru kwamba wamefuatilia na kuthibithisha na walinipigia simu kunishukuru na tayari wametoa kama breaking news. Mheshimiwa Raisi yuko kwenye kipindi kigumu sana, badi sitaelewa kamwe wanaoukimbilia uongozi wakati ni msalaba mzito lazima awe mwizi fisadi na fedhuli hawezi kuwa mtu mwenye nia njema! Nyakati ngumu kama hizi kama umekimbilia madaraka huwezi kuwa na busara za kuweza kumudu kipindi kigumu kama hiki!

R.I.P. Mheshimiwa Waziri Mgimwa!
 
what do you mean taarifa rasmi! ina maana mnaweza kuja kusema he is still alive?

Huyu Dr. ameishazushiwa kifo mara kibao hapa jf ndio maana watu wanahoji usahihi wa hii taarifa.

Tiba
 
Inguluvi ikutange Mnyalukolo...mvaha vangu,kuna munu akatigile vakusopye va mbeva,umulomo huu nene...Alee gendelage uludodifu,ulukafu luladenyeka...Vahungilage va maseto, mng'anzagala,mahuvi,mhafiwa,va sengelingosi...mbevalii....longolage myaaa

.... S U mU

...Lexicon yangu ya kihehe imepotea,..ila wamaanisha hvyo,,
 
RIP dr Mgimwa.....hujaduma kabisa kwenye hii wizara na huzuni hii ni faraja kwa wengine.....Nakumbuka takwimu zako au style yako ya kujibu maswali kisomi zaidi daaaah,Mungu nae bwana,unaweza tamani amchukue fulani ili kuache ww ila kwa vile yeye ndiye achaguaye bs hatuna budi kumshukuru kwa chaguo lake:

Pole kwa familia yako
Pole kwa chama chako
Pole kwa mwenyekiti wa chama chako
Pole kwa watanzania wote
Pole kwa wafanyakazi wenzako
 
waziri wa fedha dk william mgimwa amefariki dunia baada ya kuugua na kulazwa nchini Afrika kusini.
 
Picha wakuu wengine hatumjui,RIP father mgimwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…