Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba tunaomba uachane na uvaaji wa tai zenye rangi ya bendera ya Tanzania

RWANDES

JF-Expert Member
Joined
Jun 12, 2019
Posts
1,788
Reaction score
4,401
Wananchi wanaumia kwa sababu yako na tozo zako ambazo pamoja na kuzichukua zinawanufaisha nyie na familia yenu na kikundi chenu.

Acha kudhalilisha bendera yetu kwa kuwaumiza wanachi na matozo ya kila aina mmekosa ubunifu bidhaa zimepanda bei bado unaendelea kuweka tozo hivi wewe na serikali yako hamuoni aibu, tembea mtaani hasa vijijini muone maisha yanavyochapa watu.

Asubuhi ukiamka wewe hujui njaa mda wote kiuno kipo kwenye V8 na kiyoyozi kumbuka hayo yote hamuwezi kuyapata bila wananchi oneni huruma muwapunguzie mzigo wananchi.
 
Naunga mkono hoja yan ningekuwa mchaw ningemroga iyo tai imnyonge
 
[emoji28][emoji28][emoji28]nchi ngumu sana aiseeee
 
Huwa nikiliona na hizo tai za bendera ya taifa natamani kutapika kabisa na vindevu vyake vya kama limeuma kuku. Ila haya yana mwisho, wana CCM tunapitia kipindi kigumu mno. Rais Samia ondoa hii takataka weka Dkt Ashatu Kijaji awe waziri wa Fedha na Mipango
 
100% jana naweka mafuta ya 20k inakuja risiti ni lita 5.6. Then wanatumia bei ya nchi ambazo uchumi uko juu kufanya justication ya wizi wao.
 
Jana usiku wa manane nimeota kuwa nchi inaongozwa na Mapaka😁😁😁
Your browser is not able to display this video.
 
Shida inaanzia Kwa Bibi tozo mwenyewe maana kinachofanywa na huyo waziri wake wa fedha kina baraka zake
Mwigulu anajipambanua Kama daktari wa uchumi ambaye hapaswi kutiliwa mashaka.

Tunategemea angemshauri vyema bosi wake!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…