Waziri wa Kilimo, zao la bangi ni muhimu sana kwa maendeleo ya haraka

Waziri wa Kilimo, zao la bangi ni muhimu sana kwa maendeleo ya haraka

Kama Kenya inavyonufaika na miraa/mirungi

Ni tofauti sana. Mirungi inauzwa kama uraibu tu.

Bangi kuanzia mizizi mpaka majani hakuna kinachotupwa na hakuna kisichokuwa na kazi yenye faida.
 
He kumbe zao la bangi linamatumizi mengi hivi?
Ndiyo, tena nime-summarize tu, mfano ukija kwenye vipozi utakuta kuanzia vipodozi vya ngozi mpaka uturi (perfumes) zile za ghali, zina extracts za bangi.

Kwa ufupi, bangi inatunika kila sehemu, kuanzia kwenye dawa za matumizi ya kila siku mpaka dawa za kuandikiwa rasmi na daktari, kwenye vyakula, kwenye ujenzi, kwenye nguo.

bangi ni zao muhimu sana kwa uchumi, hususan wa nchi zetu zinazoendelea, maana nchi zilizoendelea tayari huko wana sheria, viwanda, wakulima wa bangi kwa miaka mingi sana.

Kwetu tutapiga bao sana kwa sababu, zao la bangi kwa hali yetu ya hewa (tropical) linastawi kila sehemu na kila aina.

Tunachohitaji ni vituo vya utafiti na sheria na plan ya nini kifanyike, mbegu ipi kwa mkoa upi na upi, kiwanda kipi kwa mkoa upi na upi.

Bashe asilaze damu.

Bashe kwa kukujuza tu, kwa kuwa wewe ni Muislam mwenzangu, zao la bangi siyo haramu, mtumiaji akiharibu (abuse) matumizi yake, yeye ndiye anaefanya haramu.
 
Nafahamu wengi wakisikia "bangi" akili zao zinakwenda katika kilevi cha bangi. Kilevi cha bangi ni matumizi duni ya bangi, ingawa na yenyewe inaweza kufanyiwa tafiti ikapatikana mbegu isiyo na madhara na ikauzwa kihalali kuliko hivi sasa tunaletewa mbegu za kutia watu wazimu. Mpaka skanka limejaa sasa hivi linaumiza vijana.
Nan amekwambia skanka linaumiza watu wewe mama?
 
Mheshimiwa Hussein Bashe, natumai na Rais wetu mama Samia Suluhu Hasan na washauri wake wengine utawafikia ujumbe huu.

Zao la bangi za aina tofauti tofauti (different varieties of hemp) linastawi vizuri sana Tanzania. Ni wakati muafaka, tena tumechelewa sana, kuanzisha zao la bangi kwa faida. Zao la bangi linaweza kututowa kwenye umasikini kwa haraka sana.

Baadhi ya faida zinazotokana na zao la bangi ni pamoja na:

Dawa aina mbali mbali, zinazotumika hivi sasa mahospitalini na dawa mbadala.

Pia bangi inaweza kutengeza karatasi, inaweza kutengeza mbao, inaweza kutengeza, "vigae" vya kuezekea, "boards" mbali mbali za kujengea na kuundia fanicha, inaweza kutengeza bodi za magari ambazo ni bora kuliko za mabati.

Licha ya hayo, inaweza kutengeneza virutubisho mbali mbali vya kutumika na binadam, wanyama na mimea. Pamoja na madawa ya kuzuia wadudu wa mimea.

Pia bangi inaweza kutengeneza mafuta ya kutumika kwenye magari ambayo ni bora kuliko ethanol na methanol.

Kinachotakiwa kufanywa ni kuanza na aina moja au mbili ya bidhaa muhimu na kufunguliwa kituo maalum cha utafiti na kuzalisha mbegu bora kwa biashara.

hatuna haja ya kutegemea mataifa ya nje kwenye hili, tunaweza kuzalisha mali ghafi zetu wenyewe na kuwauzia nje bidhaa zinazotokana na bangi. Ni kujipanga tu.

Nafahamu Bashe utaweza hili kwa ufanisi mkubwa ukilivalia njuga. Weka legacy kijana kupitia bangi.

Nafahamu wengi wakisikia "bangi" akili zao zinakwenda katika kilevi cha bangi. Kilevi cha bangi ni matumizi duni ya bangi, ingawa na yenyewe inaweza kufanyiwa tafiti ikapatikana mbegu isiyo na madhara na ikauzwa kihalali kuliko hivi sasa tunaletewa mbegu za kutia watu wazimu. Mpaka skanka limejaa sasa hivi linaumiza vijana.

Tuondokane na ujinga na kufata watu wa magharibi. Tumepata elimu ili itukombowe siyo tuendelee kuwa wajinga wa kuburuzwa kama misukule, wanachotaka mabwana wakubwa ndiyo tukifate, ni wakati Tanzania tukajifanyia yetu wenyewe na hao wakubwa tuwaimbishe nyimbo tunazotaka sisi. Rasilimali tunazo, kwanini watuendeshe na mali zetu?

Uchumi tunao lakini tunaukalia, Nyerere. Kwa kudanganywa tu na nchi za magharibi tutaendelee kuwa watumwa wao daima.

Naamini ndani ya miaka mitatu ya kuruhusu zao la bangi na tafiti zake za kina, hatutakopa tena nje, sisi tutakuwa wakopeshaji.

Nawasilisha.
Kongole dada.
Usipoingiza "upofu" wako wa CCM na dini, unakuwa vyema sana kichwani na kuwa na hoja za msingi.
Ubarikiwe sana. Pita hapo Panone Supermarket chukua Sprite lita 2 nakuja kulipa.

Uachane na upofu kwa CCM na dini ili uache legacy ya kuweka mawazo bora ya namna ya kutoka kwenye huu mkwamo tulionao kama taifa kwa maslahi ya Watanzani wote.

Uliyoyaandika ni sahihi sana na kwa kweli sina cha kuongeza zaidi ya kuweka msisitizo kwa serikali kulibeba hili wazo bora na kulifanyia kazi.
 
Tuna madini,

Tuna gesi

Tuna misitu

Tumeshindwa kupata maendeleo huku kwenye vitu vya thamani kubwa tuje kupata maendeleo kwenye bangi??
 
Kongole dada.
Usipoingiza "upofu" wako wa CCM na dini, unakuwa vyema sana kichwani na kuwa na hoja za msingi.
Ubarikiwe sana. Pita hapo Panone Supermarket chukua Sprite lita 2 nakuja kulipa.

Uachane na upofu kwa CCM na dini ili uache legacy ya kuweka mawazo bora ya namna ya kutoka kwenye huu mkwamo tulionao kama taifa kwa maslahi ya Watanzani wote.

Uliyoyaandika ni sahihi sana na kwa kweli sina cha kuongeza zaidi ya kuweka msisitizo kwa serikali kulibeba hili wazo bora na kulifanyia kazi.
Dini yangu ni Uislam, najivunia sana kuwa Muislam.

Nisingeyajuwa yote haya nje ya Uislam. Uislam haujazi watu ujinga.

Halafu wacha ujinga wa kuanza kujadili watu, jadili mada iliyopo.

Kumbuka hilo.

Umeziona faida chache za bangi nilizoziweka?
 
Ukisoma huelewi basi hata kuona huoni?

Nenda sober haouse za unga ukaone wavute skanka wanavyojaa siku hizi.

Fanye r"esearch" japo ndogo ya kwenye mtandao ujisomee.

Dunia ya leo unangoja uambiwe wakati unayo kiganjani?
Ukishaona imemuathiri mtu basi ujue haimfai,nimeanza kutumia since 2003 kipindi nabalehe na sijaona madhara yake japo wapo watu nimeona wametumia na imewaletea matokeo hasi,ni kama pombe tuu sio wote wana vichwa vya pombe
 
Tuna madini,

Tuna gesi

Tuna misitu

Tumeshindwa kupata maendeleo huku kwenye vitu vya thamani kubwa tuje kupata maendeleo kwenye bangi??
Bangi ni zao lenye thamani kubwa sana kuliko ujuavyo.

Sikushangai, shule zenyewe mnazokwenda ndiyo hizo za kusomea ujinga.
 
Sikushangai
twende kwenye soko, gram moja ya bangi na gram moja ya dhahabu,
Unatakiwa uwe na akili ya kibiashara,
Sigara na pombe vinauzika sana sigara ina thamani kuliko pombe lkn pombe inauzika sana kuliko sigara na ktk pato la taifa pombe inachangia pakubwa kuliko sigara, sasa , lkn pombe haijaifikia madini,
Bunda moja la sigara penda linauzwa sh 26,000, pakiti moja sh 2600, mtu mmoja kama atajitahidi sanaaaa kwa siku atamaliza pakiti moja,
Lkn hii bia ya sh 2000 mtu anaweza kunywa hata kumi kwa siku,
Ukichukua sigara za milioni moja ukampelekea muuzaji wa reja reja anaweza kuuza hata wiki ndio akamaliza,
Ukichukua pombe ukampelekea muuzaji wa reja reja anamaliza ndani ya siku moja au mbili,
Cc tupo sokoni, hatuzungumzii vitu hewa,
Kingine bangi ikihalalishwa itapungua thamani , afrika nchi zaid ya 40 zao la bangi lipo haijalishi imeruhusiwa au la.,??
Swali je kuna nchi ngapi afrika zenye madini?
Misitu ya kutosha
Bandali
nk??
 
Back
Top Bottom