JamiiTalks
JF Advocacy Team
- Aug 7, 2018
- 685
- 1,124
DAR: Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, (Zanzibar) Riziki Pembe Juma ametembelea Ofisi za JamiiForums jijini Dar, leo Oktoba 28, 2024.
Ziara yake ililenga kujenga mashirikiano katika maeneo anuai ikiwemo kuwalinda na kuwajengea uwezo Watoto na Wazazi wao hasa katika Digitali.
Waziri Riziki amewapongeza Uongozi wa JamiiForums, kwa shughuli na miradi inayoilenga jamii inayoendeshwa na taasisi na kutaka kuwepo kwa mashirikiano katika shughuli za kijamii hasa kampeni ya “MTOTO NI MBONI YANGU” na Wizara ya Maendeleo kwa kushirikiana na Taasisi ya “Ndoto Ajira” itakayofanyia Novemba na Desemba 2024 katika Mikoa mitano ya Zanzibar (Unguja na Pemba).
Ziara yake ililenga kujenga mashirikiano katika maeneo anuai ikiwemo kuwalinda na kuwajengea uwezo Watoto na Wazazi wao hasa katika Digitali.
Waziri Riziki amewapongeza Uongozi wa JamiiForums, kwa shughuli na miradi inayoilenga jamii inayoendeshwa na taasisi na kutaka kuwepo kwa mashirikiano katika shughuli za kijamii hasa kampeni ya “MTOTO NI MBONI YANGU” na Wizara ya Maendeleo kwa kushirikiana na Taasisi ya “Ndoto Ajira” itakayofanyia Novemba na Desemba 2024 katika Mikoa mitano ya Zanzibar (Unguja na Pemba).