Waziri wa Mambo ya Ndani, Innocent Bashungwa alipongeza Jeshi La Polisi kwa "kusimamia" vizuri mkutano wa CCM na Uchaguzi wa CHADEMA

Waziri wa Mambo ya Ndani, Innocent Bashungwa alipongeza Jeshi La Polisi kwa "kusimamia" vizuri mkutano wa CCM na Uchaguzi wa CHADEMA

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Wakuu,

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amelipongeza jeshi hilo kwa kusimamia ulinzi na usalama kwa weledi katika mkutano mkuu wa CCM uliofanyika Dodoma pamoja na wa Chadema uliofanyika jijini Dar es Salaam.

Bashungwa amesema hayo leo Januari 22, 2025 wakati alipofanya ziara ya kikazi Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Dodoma na kusisitiza kuwa, vyama vya siasa kutimiza wajibu wa kutii sheria bila shuruti ili kuepuka kulazimishwa kutii sheria.

“Matarajio yangu ni kwamba haki hii mnayoitenda Jeshi la Polisi kwa kutoangalia itikadi, pia vyama vya siasa kwa jumla, haki hii ije na wajibu kwa wao kutii sheria bila shuruti, hakuna haki bila wajibu”
amesisitiza Bashungwa.

 
Kwani Polisi walifanyaje kwenye lile genge la wahuni pale Dodoma na kwenye uchaguzi wa CHADEMA? Hoja ziwe fupi fupi!
 
Eti Vyama vya Upinzani
Shubaaaaaaaamit
 
Ana accent huyo, hata mimi niliekaa ulaya miaka 30 nina afadhali kwenye lafudhi.
 
Wakuu,

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amelipongeza jeshi hilo kwa kusimamia ulinzi na usalama kwa weledi katika mkutano mkuu wa CCM uliofanyika Dodoma pamoja na wa Chadema uliofanyika jijini Dar es Salaam.

Bashungwa amesema hayo leo Januari 22, 2025 wakati alipofanya ziara ya kikazi Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Dodoma na kusisitiza kuwa, vyama vya siasa kutimiza wajibu wa kutii sheria bila shuruti ili kuepuka kulazimishwa kutii sheria.

“Matarajio yangu ni kwamba haki hii mnayoitenda Jeshi la Polisi kwa kutoangalia itikadi, pia vyama vya siasa kwa jumla, haki hii ije na wajibu kwa wao kutii sheria bila shuruti, hakuna haki bila wajibu” amesisitiza Bashungwa.

Mkutano wa ccm? Kisha wakajiteua?
 
Back
Top Bottom