Waziri wa Ulinzi Dkt. Stergomena atoa angalizo kwa wananchi wanaovamia maeneo ya Jeshi

Waziri wa Ulinzi Dkt. Stergomena atoa angalizo kwa wananchi wanaovamia maeneo ya Jeshi

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Stergomena Lawrence Tax (Mb) ametoa wito wananchi kuacha kuvamia maeneo ya jeshi na kuweka makazi kwa kuwa ni hatari kwa usalama kwao na nchi kwa jumla.

“Ili Jeshi liweze kutekeleza majukumu yake linahitaji maeneo, na maeneo hayo yanakuwa ni ya kimkakati, kwanza ni hatari kwao na hatari kwa usalama.

“Wanapofanya mazoezi wanatumia vitu vingi, unaweza kuona ni eneo kubwa ukaweka mizigo yako mwisho ukasababisha madhara, tunaomba waache maeneo ambayo yametengwa kwa ajili ya jeshi,” anasema Dkt. Stergomena.

Aidha, ameelezea kufurahishwa na mwenendo wa Utendaji kazi wa Watumishi walio chini yake upande wa Wizara pamoja na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) chini ya Uongozi Mahiri wa Mkuu wa Majeshi Jenerali Venance Salvatory Mabeyo.

Waziri Stergomena Tax ameyasema hayo Jijini Dar es Salaam alpokuwa akihojiwa katika kipindi cha TWENDE PAMOJA kinachoandaliwa na Kurushwa na Channel Ten.


 
Panya road na Jeshi lenye kumiliki mizinga vifaru na Meli vita ulihusishe na Panya road babuu kah....

Sasa anaposema amani tuliyonayo ni kutokana na kazi kubwa ya jeshi, anamaanisha amani Gani na Hilo jeshi kazi yake ni ipi kwenye hiyo amani ya wananchi?
 
All Shabab waliwaonya ishieni huko huko Congo ole wenu mtie pua zenu Somalia.......
 
Vipi wahuni wanaojiita panya road wanaovamia wananchi na kujeruhi na kupora, ananeno gani kwao?
Panya road wapo chini ya Siro tena wengine ni majirani zake Chanika.
Tafuta video alipoenda Chanika na Waziri Masauni, Siro aliongea kwa uchungu sana, majirani wanamungusha.
 
Sasa anaposema amani tuliyonayo ni kutokana na kazi kubwa ya jeshi, anamaanisha amani Gani na Hilo jeshi kazi yake ni ipi kwenye hiyo amani ya wananchi?
ndohapo kutofautisha utulivu na amani hawajui AMANI inasifa yake bwana
 
Back
Top Bottom