Waziri wa Ulinzi na JKT afanya ziara Wilayani Monduli kuzungumza na viongozi wa jamii ya wafugaji

Waziri wa Ulinzi na JKT afanya ziara Wilayani Monduli kuzungumza na viongozi wa jamii ya wafugaji

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
WhatsApp Image 2025-01-26 at 01.22.43_5368381b.jpg
Januari 24, 2025, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt Stergomena Tax (Mb) amefanya ziara ya Kikazi katika Wilaya ya Monduli mkoani Arusha na kufanya mazungumzo na Viongozi wa Kimila wa jamii ya Kimasai, Viongozi wa Vijiji na Madiwani, katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli.

Mkutano huo wa Waziri wa Ulinzi na JKT ulikuwa na lengo la kujadili matumizi bora ya ardhi kati ya jamii ya Wafugaji wa Monduli pamoja na kujadili changamoto mbalimbali za matumizi ya ardhi wilayani hapo, ambazo zimejitokeza katika siku za karibuni, aidha Waziri Tax alipata fursa ya kupata taarifa zinazohusu Mafunzo ya Kijeshi katika eneo hilo.

Akimkaribisha Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, kuzungumza, Mbunge wa Jimbo la Monduli, Fred Lowassa amemshukuru Waziri wa Ulinzi na JKT kwa kufika Monduli kwa haraka baada ya kuombwa kufanya hivyo naye, kuja kujadiliana na viongozi wa kimila wa jamii ya wafugaji na wakulima, na namna bora ya kutatua changamoto zinazohusiana na matumizi ya ardhi na kuimarisha uhusiano wa muda mrefu baina ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania pamoja na wananchi.
WhatsApp Image 2025-01-26 at 01.22.43_6536d14e.jpg

WhatsApp Image 2025-01-26 at 01.22.44_6193df1a.jpg

WhatsApp Image 2025-01-26 at 01.22.44_a8f6cf7e.jpg
Akizungumza katika kikao hicho cha viongozi wa kimila wa jamii ya wafugaji pamoja na uongozi wa halmashauri ya Monduli, Waziri Tax amewahakikishia wananchi wa hapo kuwa matumizi salama ya ardhi yataendelea kuwepo kama ilivyokuwa awali katika maeneo yanayomilikiwa na JWTZ na akawataka wananchi wa eneo hilo kuhakikisha mahusiano mahusiano mazuri yaliyopo kati yao na Jeshi la Wananchi yanaendelea kudumu na kuimarishwa.

Pia, Waziri Tax amewaambia wananchi wa eneo la Monduli kuwa taratibu zote za kisheria ili kila mtu apate haki yake na kwa usawa zitafuatwa.

Mkutano huo wa Waziri wa Ulinzi na JKT ulihudhuriwa pia Mkuu wa Wilaya ya Monduli, Festo Shem Kiswaga pamoja na viongozi wa jamii ya wafugaji wa jamii ya Kimasai, Halmashauri ya Mji wa Monduli na viongozi waandamizi toka Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.
WhatsApp Image 2025-01-26 at 01.22.44_97564372.jpg
 
Back
Top Bottom