Wazo Gomvi: Kabla ya Kujitoa CHADEMA Ingeeleza Hili Kwanza...

Wazo Gomvi: Kabla ya Kujitoa CHADEMA Ingeeleza Hili Kwanza...

Mzee mwanakijiji unauliza maswali ya kisomi kwenye mchakato wa uchaguzuzi wa kiprimitive. Sio kweli kwamba ccm wanajua kujaza fomu kuliko wapinzani. Elimu ya kibongo wewe unaijua uelewa hauna huyu ni chadema au ccm. Kwanza elewa kwamba fomu haziko pale kutuchagulia kiongozi, fomu zimewekwa kutupa taarifa zamgombea tutakaye mpigia kura. Msimamizi au msimamizi msaidizi wa uchaguzi sio msimamizi wa mtihani ni mwelekezaji wa fomu anayotoa kama ilivyo kwa afisa uhamiaji anapokupa fomu ya kuomba passport. Fomu ni mchakato wa kupata taarifa za mwombaji wa nafasi ya uongozi sio paper ya kutuchagulia wa kuingia kidato cha kwanza. Hii ndio demokrasia tunayotaka itupeleke kwenye uchumi wa kati.
Asikudanganye mtu ccm haijatoa semina elekezi yoyote kwa wagombea wao kilichowasaidia ni wasimamizi wa uchaguzi kuwaelekeza jinsi ya kujaza na sehemu nyingine kuwajazia fomu zilizokosewa. Kwa upande wa wapinzani fomu zao nyingi zilihujumiwa ikiwa ni pamoja na kujaziwe zingine zenye makosa ya makusudi kwa wale waliojaza kwa usahihi.
Kurudisha fomu mapema hakuwasaidii wapinzani kwa sababu wasimamizi wanapata muda mzuri wa kuzihujumu fomu na ndio maana zinaporejeshwa dakika za mwisho wanafunga ofisi na kukimbia kwa kuhofia kwamba wakizipokea hawatapata muda wa kuzihujumu zitakuwa sahihi hivyo wanaona ni afadhali kukwepa kuzipokea kuliko kupokea halafu ukampitisha mpinzani. Watendaji wa vijiji na mitaa walipewa maelekezo ya kuwafyeka wapinzani mapema ili watu wasiingie kwenye uchaguzi. Hivyo theoretically utaona wapinzani ni wazembe lkn practically wapinzani kukwepa hujuma za ccm na watendaji wa serlikali ni vigumu sana.
 
Kwanini kanunu ziwe mpya sio zilizotumika 2014?

Kwanini watendaji waitwe Ikulu mwezi kabla ya uchaguzi?

Kwanini mpaka leo Mbowe ana kesi ya kujibu baada ya kutaka haki itendeke kwenye uchaguzi wa Kinondoni? Wewe uelewi chochote kinachoendea Tanzania bora ungenyamaza tu.

Eti Ccm ambayo inaongoza kwa mbumbumbu imeweza kujaza form halafu vyama vingine vyote wameshindwa ayo maneno uliyoandika waambie wapumbavu tu ndio watakuelewa.
Bravo kaka
 
Chadema hawapo tayari kushika dola,

Tunawapima kwenye mambo kama haya na kuwaona kuwa hamtoshi,

Sasa Chama kina wagombea ambao hata kujaza fomu hawawezi??
 
Binafsi sina tatizo la kinadharia kwa CHADEMA kujitoa kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Na hata sitakuwa na shida ya msingi hata wakijitoa Uchaguzi Mkuu. Tangu zamani nilikuwa naamini kuwa kama unaona hutendewi haki ni lazima uoneshe kuwa kweli unaamini hakuna haki. Baadhi ya matatizo ambayo yametokea mara kwa mara - na sijui kama watu wamesahau au la - ni kuwa mara nyingi CHADEMA wanajikuta wanabanwa kwenye "masuala ya kiufundi" (technicalities).

- Kuchelewa kurudisha fomu hadi siku ya mwisho, saa ya mwisho
- Kuchelewa kula kiapo, au kula kiapo kisicho sahihi (nakumbuka sana kilichotokea Mbeya Vijijini mwaka uleeee)
- Kutokujua wanarudisha fomu kwa nani (Korogwe)
- n.k

Sasa, ni lazima tujue kuwa CCM na Serikali yake hawajawahi kuwa na mpango wa kutengeneza mazingira ya Upinzani kufanikiwa. Hili nimeliandika mara nyingi huko nyuma haifai kulirudia. Sijui kwanini wapo wanaofikiria kuwa Papa atajikata, atoe mafuta yake, akuwekee moto na sufuria, halafu ajitumbukize wewe kazi yako iwe kumkaanga tu! Sikumbuki mahali popote hili limewahi kutokea. Kutegemea CCM kuwasaidia wapinzani kuja kuwaondoa madarakani ni ndoto za Alinacha.

Baada ya kusema hilo, kufuatia uamuzi huu wa Chadema kujitoa kwenye kushiriki binafsi nilitarajia mambo kadhaa yangeelezwa kwanza, maana tusije tukawalaumu wasimamizi wa uchaguzi n.k kwa makosa ambayo yangeweza kuepukika. Kwa anayejua naomba atusaidie:

1. Ni nani alikuwa Mratibu wa CHADEMA wa wagombea wa nafasi mbalimbali serikali za mitaa kitaifa?

2. Huyo mtu/watu alitoa maelekezo gani kwa wanachama wa CDM kuhusiana na ujazaji wa fomu, kurudisha fomu n.k?

3. Je, CDM kitaifa ilitoa mwongozo gani kuhusiana na wagombea wake; kwamba wanahitaji nini na wajazaje fomu? Hii inaitwa "covering all your bases)

4. Hata mahali ambapo mikutano ya ndani isingewezekana CDM kitaifa ilifanya juhudi gani hata kupitia mitandao ya kijamii (Facebook, Youtube, au hata hapa JF) kuwajulisha wagombea wake jinsi ya kujaza fomu n.k Yaani, Freeman Mbowe au Katibu Mkuu Mashinji wameshindwa kuanzisha hata thread moja yenye maelekezo na nakala za fomu za mfano za nini kinatakiwa zikawekwa hapa?

5. CDM iliwaandaa watu wake vipi kubanana na wale wasimamizi ambao walikuwa wanaonekana kweli kuwakwepa. Hivi kweli CDM na vijana wake hakuna watu wenye kusema "hatutoki hapa hadi mpokee fomu zetu"? Ni upinzani gani huu!

Haya ni baadhi tu ya maswali yangu kwa sababu tusije kuwalaumu ama wagombea na wale watia nia au wasimamizi. Tujiulize kidogo CDM inawajibika vipi kuwandaa wagombea wake maana msipojibu maswali haya mtakutana tena 2020 na mambo yale yale.

Pendekezo Moja: CDM ije na sera ya wazi na maelekezo ya wazi kuwa wagombea wake wote wahakikishe wanarudisha fomu siku tano kabla ya mwisho wa siku iliyowekwa. Mtashangaa tofauti itakuwa nini hapa.
Mzee unasikitisha Sana...wakati mwingine uwe unatuoia tu...hata ukiwashwa
 
Mzee Mwanakijiji, nimekuheshimu sana muda wote tangu nimekufahamu.

Hivi katika tathmini yako ya haya yanayotokea wewe unaona lawama ielekee kwa victim wa udhalimu?

Huyo mdhalimu Una neno gani kumhusu ?
 
5. CDM iliwaandaa watu wake vipi kubanana na wale wasimamizi ambao walikuwa wanaonekana kweli kuwakwepa. Hivi kweli CDM na vijana wake hakuna watu wenye kusema "hatutoki hapa hadi mpokee fomu zetu"? Ni upinzani gani huu!


Mkuu unahabari hadi sasa hivi vingozi wa upinzani wanaendelea kuwajibika mahakamani kwa kifo kilichosababishwa na askari kufyatua risasi wakati wa uchaguzi wa Kinondoni?

Unaongeleaje faulo walizofanyiwa wagombea kabla hata ya kujadili jambo la ujazaji na urudishaji wa hizo form?
 
Wangetumia mbinu gani katika mazingira haya ya awamu hii?

Je hakuna faulo za wazi zinazofanyika? Faulo zinapofanyika na kulindwa na nguvu ya dola, ungekuwa wewe kiongozi ungefanya nini?
Wapinzani wanapigwa ngumi zile zile, kutokea mkono ule ule na mtu yule yule na wao wanalia kilio kile kile kila ngumi inapotua usoni kwao! Mnajisumbua kuwashauri hawa! Hii nchi itakuja kuwekwa sawa na wananchi wenyewe na si watu ambao mindset zao zimeji tune kuwa wapinzani wa kudumu!
 
Mzee una habari kuwa ACT ilikuwa na watu 173,593 walioomba kugombea kwenye serikali za mitaa lakini kati yao watu 166,649 Wameenguliwa, yaani 96% ya waliogombea kupitia ACT wameenguliwa je unalijua hilo?

Je una habari kuwa 97% ya waliotaka kugombea kupitia Chadema wameenguliwa?

Mzee una habari kuwa watu wote walioomba kugombea kupitia NCCR-Mageuzi katika wilaya ya Vunjo wameenguliwa?

Mzee Mwanakijiji acha kulaumu Victim, usishiriki karamu ya uonevu na udhalimu wa ajabuajabu, wewe ni mtu mzima achana na habari hizi mbofumbofu!

Hujasema sababu za kuenguliwa.
 
Binafsi sina tatizo la kinadharia kwa CHADEMA kujitoa kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Na hata sitakuwa na shida ya msingi hata wakijitoa Uchaguzi Mkuu. Tangu zamani nilikuwa naamini kuwa kama unaona hutendewi haki ni lazima uoneshe kuwa kweli unaamini hakuna haki. Baadhi ya matatizo ambayo yametokea mara kwa mara - na sijui kama watu wamesahau au la - ni kuwa mara nyingi CHADEMA wanajikuta wanabanwa kwenye "masuala ya kiufundi" (technicalities).

- Kuchelewa kurudisha fomu hadi siku ya mwisho, saa ya mwisho
- Kuchelewa kula kiapo, au kula kiapo kisicho sahihi (nakumbuka sana kilichotokea Mbeya Vijijini mwaka uleeee)
- Kutokujua wanarudisha fomu kwa nani (Korogwe)
- n.k

Sasa, ni lazima tujue kuwa CCM na Serikali yake hawajawahi kuwa na mpango wa kutengeneza mazingira ya Upinzani kufanikiwa. Hili nimeliandika mara nyingi huko nyuma haifai kulirudia. Sijui kwanini wapo wanaofikiria kuwa Papa atajikata, atoe mafuta yake, akuwekee moto na sufuria, halafu ajitumbukize wewe kazi yako iwe kumkaanga tu! Sikumbuki mahali popote hili limewahi kutokea. Kutegemea CCM kuwasaidia wapinzani kuja kuwaondoa madarakani ni ndoto za Alinacha.

Baada ya kusema hilo, kufuatia uamuzi huu wa Chadema kujitoa kwenye kushiriki binafsi nilitarajia mambo kadhaa yangeelezwa kwanza, maana tusije tukawalaumu wasimamizi wa uchaguzi n.k kwa makosa ambayo yangeweza kuepukika. Kwa anayejua naomba atusaidie:

1. Ni nani alikuwa Mratibu wa CHADEMA wa wagombea wa nafasi mbalimbali serikali za mitaa kitaifa?

2. Huyo mtu/watu alitoa maelekezo gani kwa wanachama wa CDM kuhusiana na ujazaji wa fomu, kurudisha fomu n.k?

3. Je, CDM kitaifa ilitoa mwongozo gani kuhusiana na wagombea wake; kwamba wanahitaji nini na wajazaje fomu? Hii inaitwa "covering all your bases)

4. Hata mahali ambapo mikutano ya ndani isingewezekana CDM kitaifa ilifanya juhudi gani hata kupitia mitandao ya kijamii (Facebook, Youtube, au hata hapa JF) kuwajulisha wagombea wake jinsi ya kujaza fomu n.k Yaani, Freeman Mbowe au Katibu Mkuu Mashinji wameshindwa kuanzisha hata thread moja yenye maelekezo na nakala za fomu za mfano za nini kinatakiwa zikawekwa hapa?

5. CDM iliwaandaa watu wake vipi kubanana na wale wasimamizi ambao walikuwa wanaonekana kweli kuwakwepa. Hivi kweli CDM na vijana wake hakuna watu wenye kusema "hatutoki hapa hadi mpokee fomu zetu"? Ni upinzani gani huu!

Haya ni baadhi tu ya maswali yangu kwa sababu tusije kuwalaumu ama wagombea na wale watia nia au wasimamizi. Tujiulize kidogo CDM inawajibika vipi kuwandaa wagombea wake maana msipojibu maswali haya mtakutana tena 2020 na mambo yale yale.

Pendekezo Moja: CDM ije na sera ya wazi na maelekezo ya wazi kuwa wagombea wake wote wahakikishe wanarudisha fomu siku tano kabla ya mwisho wa siku iliyowekwa. Mtashangaa tofauti itakuwa nini hapa.
Hivi unaongea nini wewe?
 
Mtu aliyezoea kupiga mawe nyumba ya vioo dawa yake ni kumwekea vyuma ili akirusha jiwe kizembe lidunde na kurudi kwake.

Hao wasimamizi hawataacha kufanya hivyo mpaka watakapoona malipo ya matendo yao maovu kuwa ni hasara kwao.
Kwa sasa malipo ya matendo yao ni furaha na anasa wanazopata baada ya kupandishwa vyeo.
 
Bado mnahaingashana na hizi siasa za bongo?toka 2000 mi mshabiki tu
 
Siku hizi ninapata shida sana kukusoma MMK; kiasi kwamba hadi nimefikia mahali nikiona mada yako, nasita kuisoma.
Hii mada nimeiona tokea mwanzo ilipowekwa hapa. Nikaghaili kuifungua.
Mwisho wa siku, uvumilivu ukanishinda, nikafungua kuchungulia kuna nini.

Baada ya kuanzia kusoma mwisho wa mada na kufikia maswali uliyouliza, nikajikuta nikiunga mkono maswali yale.

Kiufupi, ningependa sana CHADEMA waeleze, wajibu maswali hayo moja baada ya jingine.
Haya maswali ndio msingi imara wa uimara wa CHADEMA, na ndio hayo hayo wengi tunaopenda upinzani wa kweli na wenye nguvu wawe na uwezo wa kusema tulifanya hiki na hiki kuwafikia wananchi huko waliko, sio kwa mikutano tu, zipo njia nyingi za kufanya hivyo.

CHADEMA, au kama wapo wawakilishi wao hapa, wekeni majibu juu ya maswali aliyouliza Mkuu Mwanakijiji, haya ni maswali ambayo nasi wengine tunayo shauku kubwa kujua majibu yake.

Sikusoma hadi mwanzo wa mada, kwa hiyo sijui huko juu mada inaeleza nini. Kama anawashabikia CCM, na hasa mtu wake kama kawaida yake, hayo nayapinga, hata bila kuyasoma.
 
Binafsi sina tatizo la kinadharia kwa CHADEMA kujitoa kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Na hata sitakuwa na shida ya msingi hata wakijitoa Uchaguzi Mkuu. Tangu zamani nilikuwa naamini kuwa kama unaona hutendewi haki ni lazima uoneshe kuwa kweli unaamini hakuna haki. Baadhi ya matatizo ambayo yametokea mara kwa mara - na sijui kama watu wamesahau au la - ni kuwa mara nyingi CHADEMA wanajikuta wanabanwa kwenye "masuala ya kiufundi" (technicalities).

- Kuchelewa kurudisha fomu hadi siku ya mwisho, saa ya mwisho
- Kuchelewa kula kiapo, au kula kiapo kisicho sahihi (nakumbuka sana kilichotokea Mbeya Vijijini mwaka uleeee)
- Kutokujua wanarudisha fomu kwa nani (Korogwe)
- n.k

Sasa, ni lazima tujue kuwa CCM na Serikali yake hawajawahi kuwa na mpango wa kutengeneza mazingira ya Upinzani kufanikiwa. Hili nimeliandika mara nyingi huko nyuma haifai kulirudia. Sijui kwanini wapo wanaofikiria kuwa Papa atajikata, atoe mafuta yake, akuwekee moto na sufuria, halafu ajitumbukize wewe kazi yako iwe kumkaanga tu! Sikumbuki mahali popote hili limewahi kutokea. Kutegemea CCM kuwasaidia wapinzani kuja kuwaondoa madarakani ni ndoto za Alinacha.

Baada ya kusema hilo, kufuatia uamuzi huu wa Chadema kujitoa kwenye kushiriki binafsi nilitarajia mambo kadhaa yangeelezwa kwanza, maana tusije tukawalaumu wasimamizi wa uchaguzi n.k kwa makosa ambayo yangeweza kuepukika. Kwa anayejua naomba atusaidie:

1. Ni nani alikuwa Mratibu wa CHADEMA wa wagombea wa nafasi mbalimbali serikali za mitaa kitaifa?

2. Huyo mtu/watu alitoa maelekezo gani kwa wanachama wa CDM kuhusiana na ujazaji wa fomu, kurudisha fomu n.k?

3. Je, CDM kitaifa ilitoa mwongozo gani kuhusiana na wagombea wake; kwamba wanahitaji nini na wajazaje fomu? Hii inaitwa "covering all your bases)

4. Hata mahali ambapo mikutano ya ndani isingewezekana CDM kitaifa ilifanya juhudi gani hata kupitia mitandao ya kijamii (Facebook, Youtube, au hata hapa JF) kuwajulisha wagombea wake jinsi ya kujaza fomu n.k Yaani, Freeman Mbowe au Katibu Mkuu Mashinji wameshindwa kuanzisha hata thread moja yenye maelekezo na nakala za fomu za mfano za nini kinatakiwa zikawekwa hapa?

5. CDM iliwaandaa watu wake vipi kubanana na wale wasimamizi ambao walikuwa wanaonekana kweli kuwakwepa. Hivi kweli CDM na vijana wake hakuna watu wenye kusema "hatutoki hapa hadi mpokee fomu zetu"? Ni upinzani gani huu!

Haya ni baadhi tu ya maswali yangu kwa sababu tusije kuwalaumu ama wagombea na wale watia nia au wasimamizi. Tujiulize kidogo CDM inawajibika vipi kuwandaa wagombea wake maana msipojibu maswali haya mtakutana tena 2020 na mambo yale yale.

Pendekezo Moja: CDM ije na sera ya wazi na maelekezo ya wazi kuwa wagombea wake wote wahakikishe wanarudisha fomu siku tano kabla ya mwisho wa siku iliyowekwa. Mtashangaa tofauti itakuwa nini hapa.
Tatizo Hawa watu wamegoma kujua kuwa siasa ni Game Of Timing. Kwenye siasa unapokosea ni furaha na ushindi kwa mpinzani wako. CCM walijiandaa kuwachinja wapinzani wao kwa style hii. Ndio maana wao CCM hakuna mgombea aliyejaza form nyumbani kwake. Wote walijaza chini ya uangalizi wa wanasheria wa chama walio sambazwa nchi nzima.
 
Mzee Mwanakijiji

Hoja zako zina mantiki katika mazingira fulani, haya yaliyopo zinakosa nguvu

1. Wapinzani wanaweza kutekeleza yote uliyosema lakini hali ikabaki kama ilivyo
Dahamira ya uovu ambayo haiwezi kukosa sababu halali au za kutunga

2. Polisi anaposimama akisema ''CCM watembee kifua mbele ndiyo wenye dola'' ,unategemea nini?

Mgombea anaweza kurudisha fomu siku 5 kabla na ikatungwa sababu analeta vurugu, Polisi wakatenda yao.

Ndiyo hayo hayo ya vijana kukusanyika wakimtaka msimamizi awepo, wataishia kupigwa mabomu

3. Hivi makatibu kata walioitwa nani atathubutu kuwaambia wanafanya makosa?

3. kuchukua Fomu watu wamekatwa mapanga na hakuna hatua, hivi hapo kuna dhamira njema?

4. Mgombea anaweza kurudisha fomu na msimamizi akakaa nazo na muda ukifika akasema majibu hayo hayo

Orodha inaendelea, na kwahilo hata uzembe wa Wapinzani unapata utetezi! Uhuni unazidi uzembe

Hivi unakubaliana na hoja kwamba CCM waliweka wanasheria kila kitongoji n.k.!!

Katika uongo wa namna hii hivi tunahitaji darubinu kubaini kuwa Dhamira imetimizwa kwa uzuri na ubaya

Nafsi zinawasuta hadi kusema uongo wakiangalia kamera, nini kinawashinda?
 
Maswali ya kipumbavu. hv unaishi Tanzania kweli?Hakuna technical zilizojitokeza ni uhuni mtupu wa CCM na serkali yake. Achana na na hoja za kitoto. Nyambafu
Nikiacha hilo la "maswali kuwa ya kipumbavu", ninakubaliana nawe kabisa katika hayo mengine uliyoyaandika kuhusu "kuwepo na technical zilizojitokeza...."

Lakini, pamoja na kukubaliana nawe katika hilo, je wewe huoni kwamba kama CHADEMA waliyafanya maandalizi ambayo Mzee Mwanakijiji kayawekea maswali, kwamba hiyo ni kwa faida ya CHADEMA yenyewe?

Mimi ningependa CHADEMA wawe wameyatimiza yote hayo yaliyowekwa kwenye maswali ya mleta mada, kwa sababu kuu mbili:

Mosi, huo ndio ungekuwa ushahidi usiopingika kwamba CHADEMA wamehujumiwa kwa sababu watu wao waliandaliwa ipasavyo, na wasingeweza kufanya makosa yanayodaiwa waliyafanya na kutopitishwa kuwa wagombea. Tungejua bila ya shaka yoyote, kwamba hizi ni hujuma zinazofanywa na watumishi wa serikali.

Pili, kufanya yote yale yaliyoulizwa kwenye maswali ni kuiimarisha CHADEMA yenyewe, hadi katika ngazi za chini kabisa. Ni mpuuzi gani atakyechezea CHAMA chenye wanachama walioiva barabara na kuzijua haki zao ipasavyo. Hao wanaofunga ofisi na kukimbia wasingethubutu kamwe kufanya upuuzi huo.

Naomba CHADEMA wayajibu maswali yaliyowekwa na Mzee Mwanakijiji.
 
Binafsi sina tatizo la kinadharia kwa CHADEMA kujitoa kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Na hata sitakuwa na shida ya msingi hata wakijitoa Uchaguzi Mkuu. Tangu zamani nilikuwa naamini kuwa kama unaona hutendewi haki ni lazima uoneshe kuwa kweli unaamini hakuna haki. Baadhi ya matatizo ambayo yametokea mara kwa mara - na sijui kama watu wamesahau au la - ni kuwa mara nyingi CHADEMA wanajikuta wanabanwa kwenye "masuala ya kiufundi" (technicalities).

- Kuchelewa kurudisha fomu hadi siku ya mwisho, saa ya mwisho
- Kuchelewa kula kiapo, au kula kiapo kisicho sahihi (nakumbuka sana kilichotokea Mbeya Vijijini mwaka uleeee)
- Kutokujua wanarudisha fomu kwa nani (Korogwe)
- n.k

Sasa, ni lazima tujue kuwa CCM na Serikali yake hawajawahi kuwa na mpango wa kutengeneza mazingira ya Upinzani kufanikiwa. Hili nimeliandika mara nyingi huko nyuma haifai kulirudia. Sijui kwanini wapo wanaofikiria kuwa Papa atajikata, atoe mafuta yake, akuwekee moto na sufuria, halafu ajitumbukize wewe kazi yako iwe kumkaanga tu! Sikumbuki mahali popote hili limewahi kutokea. Kutegemea CCM kuwasaidia wapinzani kuja kuwaondoa madarakani ni ndoto za Alinacha.

Baada ya kusema hilo, kufuatia uamuzi huu wa Chadema kujitoa kwenye kushiriki binafsi nilitarajia mambo kadhaa yangeelezwa kwanza, maana tusije tukawalaumu wasimamizi wa uchaguzi n.k kwa makosa ambayo yangeweza kuepukika. Kwa anayejua naomba atusaidie:

1. Ni nani alikuwa Mratibu wa CHADEMA wa wagombea wa nafasi mbalimbali serikali za mitaa kitaifa?

2. Huyo mtu/watu alitoa maelekezo gani kwa wanachama wa CDM kuhusiana na ujazaji wa fomu, kurudisha fomu n.k?

3. Je, CDM kitaifa ilitoa mwongozo gani kuhusiana na wagombea wake; kwamba wanahitaji nini na wajazaje fomu? Hii inaitwa "covering all your bases)

4. Hata mahali ambapo mikutano ya ndani isingewezekana CDM kitaifa ilifanya juhudi gani hata kupitia mitandao ya kijamii (Facebook, Youtube, au hata hapa JF) kuwajulisha wagombea wake jinsi ya kujaza fomu n.k Yaani, Freeman Mbowe au Katibu Mkuu Mashinji wameshindwa kuanzisha hata thread moja yenye maelekezo na nakala za fomu za mfano za nini kinatakiwa zikawekwa hapa?

5. CDM iliwaandaa watu wake vipi kubanana na wale wasimamizi ambao walikuwa wanaonekana kweli kuwakwepa. Hivi kweli CDM na vijana wake hakuna watu wenye kusema "hatutoki hapa hadi mpokee fomu zetu"? Ni upinzani gani huu!

Haya ni baadhi tu ya maswali yangu kwa sababu tusije kuwalaumu ama wagombea na wale watia nia au wasimamizi. Tujiulize kidogo CDM inawajibika vipi kuwandaa wagombea wake maana msipojibu maswali haya mtakutana tena 2020 na mambo yale yale.

Pendekezo Moja: CDM ije na sera ya wazi na maelekezo ya wazi kuwa wagombea wake wote wahakikishe wanarudisha fomu siku tano kabla ya mwisho wa siku iliyowekwa. Mtashangaa tofauti itakuwa nini hapa.
Zamani wewe Mwanakijiji ulikuwa angalau na busara kidogo, Lakini sasa tangu Magufuli aingie madarakani unaonekana umepoteza mwelekeo. Unachojua ni kumtetea Magufuli na serikali yake na yote mabaya ambayo anayoyafanya unaona ni sawa. Hivi ufikiri wako umehamia wapi? Wewe kwa akili yako unaona ni sawa CDM kukatwa wagombea wake kwa asilimia 96%, ACT wanaambiwa hakitambuliki na msajili na malaki ya wagombea wa vyama hivyo viwili wameenguliwa, watendaji wa serikali wanachana forms za wapinzani waziwazi na wagombea wanaambiwa wakashtaki popote! Forms zingine za wagombea za wapinzani zimeongezwa sifuri, hivi kweli kuna mtu anayeweza kuandika 19790 na watu zaidi ya elfu moja wakosee hizo numbers??? Acheni utani, mkitaka kuiba basi muwe na akili kidogo! Tanzania hakuna DEMOKRASIA wala uchaguzi uliofanyika kihalali na huyu Magufuli sasa anafanya waziwazi...KAMA ANAPENDWA ANAOGOPA NINI KUFANYA UCHAGUZI WA HALALI? Kwanini anakamata watu kwa kutoa mawazo yao? Kusema tu vyuma vimekaza unapaswa ukamatwe??? Serikali ya Magufuli ni duni na primitive kuliko serikali zote zilizopita. Wewe Mwanakijiji unatetea uovu au ni hulka ya Wasukuma kutetea home ports wao? Tumia angalau sense kidogo....uonevu wa wazi lakini unabwabwaja tu...unataka vyama vingine vifanye nini zaidi? Mwambie Magufuli na serikali waache uonevu na kuua watu....Watanzania wanahitaji kuheshimiwa asituletee mambo ya Usukumani. Mmezoea kuua watu wasio na hatia....Mnaua wazee(Mababu na Mabibi zenu), Mnaua Albino, mnachuna ngozi watu na mnaongoza kwa kubaka watoto huko Geita na sasa mnaanza kuleta matatizo nchi nzima...BAKINI HUKO HUKO NA MATATIZO YENU!
 
Hivi unakubaliana na hoja kwamba CCM waliweka wanasheria nchi nzima, yaani kwa idadi ya wanasheria tulio nao wote wakiajiriwa hata wilaya moja haitoshi, I mean kuanzia vitongoji n.k.
Hapa tunaweza hata kuanza kuuliza swali.
Je, ni jukumu la nani kuelimisha walengwa (wagombea).
Hili sio jukumu la Tume ya Uchaguzi kwa Vyama vyote? Kama fomu ina mambo ya kisheria ambayo sio rahisi kwa mtu wa kawaida kuielewa, kwa nini liwe jukumu la vyama vya siasa kutoa tafsiri ya fomu hizo?

Kwa nini fomu zenye lugha rahisi, inayoeleweka na mtu wa kawaida hadi huko vijijini isitumike?

Je, CHADEMA wanaweza kwenda mahakamani kudai/kupinga hili na wakasikilizwa?
 
Back
Top Bottom