Wazo Gomvi: Kabla ya Kujitoa CHADEMA Ingeeleza Hili Kwanza...

Wazo Gomvi: Kabla ya Kujitoa CHADEMA Ingeeleza Hili Kwanza...

Hapa tunaweza hata kuanza kuuliza swali.
Je, ni jukumu la nani kuelimisha walengwa (wagombea).
Hili sio jukumu la Tume ya Uchaguzi kwa Vyama vyote? Kama fomu ina mambo ya kisheria ambayo sio rahisi kwa mtu wa kawaida kuielewa, kwa nini liwe jukumu la vyama vya siasa kutoa tafsiri ya fomu hizo?

Kwa nini fomu zenye lugha rahisi, inayoeleweka na mtu wa kawaida hadi huko vijijini isitumike?

Je, CHADEMA wanaweza kwenda mahakamani kudai/kupinga hili na wakasikilizwa?
Unajua hadithi ya mwanakondooo!
Ukiwa na dhamira mbaya hutakosa sababu za kuhalalisha dhamira hiyo.
Huwezi kuaminisha umma wasiojua kujaza fomu ni Wapinzani tu!

Hivi huoni unajifunga goli la Nape!
 
[="Kalamu1, post: 33416287, member: 494040"]
Mimi ningependa CHADEMA wawe wameyatimiza yote hayo yaliyowekwa kwenye maswali ya mleta mada, kwa sababu kuu mbili:

Mosi, huo ndio ungekuwa ushahidi usiopingika kwamba CHADEMA wamehujumiwa kwa sababu watu wao waliandaliwa ipasavyo, na wasingeweza kufanya makosa yanayodaiwa waliyafanya na kutopitishwa kuwa wagombea. Tungejua bila ya shaka yoyote, kwamba hizi ni hujuma zinazofanywa na watumishi wa serikali.
Wasimamizi kukimbia vituo nalo unalisemaje?
Hao Chadema wangefanya maandalizi kwa njia gani ikiwa mikutano imepigwa marufuku!
Kuna maandalizi gani ya uchukua Fomu? Mbona watu walikatwa mapanga! Nalo unasemaje

Pili, kufanya yote yale yaliyoulizwa kwenye maswali ni kuiimarisha CHADEMA yenyewe, hadi katika ngazi za chini kabisa. Ni mpuuzi gani atakyechezea CHAMA chenye wanachama walioiva barabara na kuzijua haki zao ipasavyo. Hao wanaofunga ofisi na kukimbia wasingethubutu kamwe kufanya upuuzi huo.
Mikutano ya siasa ni marufuku, Polisi wanasimamia vema na wapo watu mahabusu! Hujui hilo?

Unaimarishaje chama kama huwezi kuwafikia wanachama hadi 2020?

Unahitaji ushahidi gani wa watumishi wa umma ikiwa Polisi wanasema CCM watembee vifua mbele
Polisi wamekuwa sehemu ya mikutano ya ndani ya CCM
Polisi wanalazimishwa wasalimie kwa salam za chama?

Tusikwepe ukweli kwa kutafuta sababu rahisi kama zile za mwenezi wetu.

Mwenezi ambaye ni kijana tu kwa umri bila haya wala soni anaaminisha umma CCM wameweka wanasheria kila kijiji na kitongoji. Tena anasema bila kupepesa macho wala aibu! Imesikitisha sana! inatia simanzi

Mwenezi anajua Tanzania imejaa majuha, yeye na kundi lake ndio wajuvi! Bila aibu yoyote anaangalia kamera

Hizi mbinu ndizo unazotaka kuzifanya sababu! semeni ukweli tu kwani ukweli haufichwi , unajdhihiri
 
Hapa tunaweza hata kuanza kuuliza swali.
Je, ni jukumu la nani kuelimisha walengwa (wagombea).
Hili sio jukumu la Tume ya Uchaguzi kwa Vyama vyote? Kama fomu ina mambo ya kisheria ambayo sio rahisi kwa mtu wa kawaida kuielewa, kwa nini liwe jukumu la vyama vya siasa kutoa tafsiri ya fomu hizo?

Kwa nini fomu zenye lugha rahisi, inayoeleweka na mtu wa kawaida hadi huko vijijini isitumike?

Je, CHADEMA wanaweza kwenda mahakamani kudai/kupinga hili na wakasikilizwa?

Miongoni mwa maswali mazuri sana haya; maana upande wa swali hilo ni kuwa inawezekana vipi wale wa CCM "waonekane" wamejaza fomu zao kwa usahihi yaani hata mmoja asienguliwe?
 
Mzee Mwanakijiji, nimekuheshimu sana muda wote tangu nimekufahamu.

Hivi katika tathmini yako ya haya yanayotokea wewe unaona lawama ielekee kwa victim wa udhalimu?

Huyo mdhalimu Una neno gani kumhusu ?

Mbona nilichoandika siyo lawama; ni maswali tu na hayajajibiwa.
 
Pendekezo Moja: CDM ije na sera ya wazi na maelekezo ya wazi kuwa wagombea wake wote wahakikishe wanarudisha fomu siku tano kabla ya mwisho wa siku iliyowekwa. Mtashangaa tofauti itakuwa nini hapa.

Mwanakijiji naona kwa baadhi ya watu ulitenda dhambi isiyosameheka kwa kutokumuunga mkono mgombea wa CHADEMA 2015! Licha ya kwamba mgombea mwenyewe alisharudi kwao, kurudi huko hakujazipoza hasira za hao watu.

Jina lako linaamsha hisia kali miongoni mwa watu kiasi kwamba nahisi walionapo tu jina lako hata hawasomi kwa utulivu ulichoandika na kukielewa. Hisia zao kali zinawasukuma kuku-dismiss tu. Hahahaa.

Kuhusu mada, nina nyongeza moja hapo kwenye pendekezo lako. Sina hakika kama CDM wana idara ya 'Compliance' iliyo na compliance officers.

Kama hawana, ni vyema wakafikiria kuanzisha idara kama hiyo itakayohakikisha kuwa chama na wagombea wake wa ngazi zote wanakuwa in full compliance with election law.

Idara kama hiyo pia inaweza kutoa mafunzo kwa watendaji wa chama kuhusu chaguzi na mambo mengine yahusuyo sheria kwa ujumla katika sehemu mbalimbali nchini hata nyakati ambazo si za uchaguzi.

Umezungumzia kuhusu chama ku cover all the bases. Ni kweli. CDM hawawezi kabisa ku afford kutenda 'unforced errors'.

La sivyo kila mara watakuwa ni watu wa kulalamika kuwa wanaonewa [jambo ambalo laweza kuwa na ukweli], licha ya kwamba baadhi ya matatizo wanajisababishia wenyewe kwa kutokuwa makini.

CDM inapaswa kuifanya kazi ya CCM/ serikali kuinyanyasa iwe ngumu sana. Lakini siyo kuwarahisishia CCM na serikali yake kuwanyanyasa kupitia makosa yao madogo madogo ya kiufundi.
 
Mimi nilishawahi kufanya kazi kama election observer Tanzania huko nyuma. Mwanakijiji you know nothing about the dangers of fighting a ruling party at the grass-root level in a repressive regime such as Tanzania. Hizo stories unazosoma mitandaoni kwamba wapinzani eti walikuwa wanaongoza kwa kukosea kujaza form, kuchelewa kurejesha forms asilimia kubwa ni "fake news" zilizotengenezwa na chama tawala kuwafanya wapinzani waonekane walikiuka taratibu ndogondogo. Akili za kuambiwa changanya na za kwako. We all know all your analyses are based on flawed secondhand information. You are not in the country. Ndiyo maana wenye akili wanapotezea threads zako nyingi tu sikuhizi. You don't get it, because you are out of touch with the reality on the ground.
 
Mzee Mwanakijiji,
Kama uliyajua hayo yote ulikuwa wapi kutoa msaada mpaka unavizia vizia cha kuandika hapa. Huu unafiki ni dhambi mbaya sana tumuogope Mungu. Kwa nini hizo technicalities hukuziweka mapema kama unawapenda sana wapinzani kwa huo ushauri wako?
 
Uhuni huu una uhalisi wake huko ofisi za watendaji. Hakuna siri ya watu woote wale wanasema wanatekeleza maelekezo.
 
Mzee Mwanakijiji,
Upinzani wa Tanzania ni wa kujitajirisha wapinzani binafsi. Hawana hata chembe ya mkakati wa kuongoza nchi bali kuangalia matumbo yao. Mbowe leo hii kaifilisi Chadema, sasa kiongozi kama huyo ukimpa aongoze nchi itakuwaje? Hatuwezi kurudia makossa yaliyopita ya marais wa kujifunza, Mwinyi, Mkapa na Kikwete. JPM amekata mzizi wa fitina, Tanzania tunaweza tena sana tu. Don't waste your time and money kwa wapinzani wa Tanzania. Zito kajitajirisha kupitia NSSF, Lisu anakwenda kulialia kule marekani kuwachangisha Watanzania masikini aibu!
Ona akili matope hii! Budogo o mbehi!
 
Hii mada si mpya, tulishwahikuijadili wakati wa Ubunge. Nipo katika rekodi nikihoji mantiki ya kurudisha fomu dakika za mwisho.

Tukasema kuna technical issues ambazo Wapinzani lazima wajue namna ya kuzikwepa.

Katika mazingira ya leo hilo haliwezi kutatua matatizo wanayoyapata
"Nyani Ngabu, post: 33416398, member: 188"]
Sina hakika kama CDM wana idara ya 'Compliance' iliyo na compliance officers.

Kama hawana, ni vyema wakafikiria kuanzisha idara kama hiyo itakayohakikisha kuwa chama na wagombea wake wa ngazi zote wanakuwa in full compliance with election law.
Mbunge hawezi kufanya kampeni nje ya eneo lake.

Akiwa ndani ya jimbo lake haruhusiwi kuongelea jambo lolote isipokuwa ''shida''
Huyo compliance officer atafanya nini?

Mwenyekiti wa chama cha upinzani haruhusiwi kufanya maikutano nje ya jimbo lake.
Iwe ni ACT au Chadema! Compliance officer atafanya kazi kitongoji gani?

Shughuli za siasa hadi 2020, compliance officer atafanya kazi lini na wapi?
I mean tuweni wakweli wa nafasi zetu
Idara kama hiyo pia inaweza kutoa mafunzo kwa watendaji wa chama kuhusu chaguzi na mambo mengine yahusuyo sheria kwa ujumla katika sehemu mbalimbali nchini hata nyakati ambazo si za uchaguzi.
Mwenyekiti wa chama haruhusiwi mikutano, huyo compliance office atatoa mafunzo wapi?
Umezungumzia kuhusu chama ku cover all the bases. Ni kweli. CDM hawawezi kabisa ku afford kutenda 'unforced errors'.
NCCR? ACT?
Kuna unforced error lakini tusifumbie macho uhuni unaoendelea kwa kisingizio hicho.

Unaamini kabisa CCM wamejaza fomu kwa usahihi nchi nzima na kwamba walikuwa na Wanasheria kila kitongoji!
CDM inapaswa kuifanya kazi ya CCM/ serikali kuinyanyasa iwe ngumu sana. Lakini siyo kuwarahisishia CCM na serikali yake kuwanyanyasa kupitia makosa yao madogo madogo ya kiufundi.
Kuchukua fomu kunahitaji ufundi gani?

Watu walikatwa mapanga kuchukua fomu! Hawa waliokatwa mapanga walifanya makosa gani ya kiufundi?

Kuna makosa ya Upinzani na moja nimelieleza katika uzi wa Mwanakiji wiki moja kabla.

Kwamba mazingira yaliyopo yalitengenezwa watu wajiandikishe kujenga uhalali wa uchaguzi

Watu wamejiandikisha ,kilichofuata ni kuengua wagombea ili ushindi wa asilimia 99 upatikane
Hili mbona wengine tuliliona hata kabla ya juzi au jana.
Tuliwaambia Wapinzani wanachokifanya ni jaribio la kuhalalisha madhaifu.

Leo nashangaa wanalalamika!

Nasi wananchi tuna shea yetu. Tumekuwa ''partisan'' au washabiki sana kiasi kwamba tunadanganywa na akina Mwenezi na kukubali kuwa kuna makosa wamefanya wapinzani

Hatujishughulishi kuangalia kama kuna ukweli, tunalaumu tukifumbia macho mapanga vichwani

''Nione umamtangaza mpinzani''! halafu leo tunadhani kuna matatizo ya ufundi!
 
Hakuna Mwenye ishu na chadema sio mwanzo wa VYAMA vya upinzani kuondoka kwenye status ya kuwa chama kikuu cha upinzani

State agent
Jamaaa unatumia Nguvu nyingi saaana kumuaminisha alioko Nyuma yako Upo Active but michango yako na ya Darasa la Pili B haitofautiani.
Nawasilisha.
 
Hii mada si mpya, tulishwahikuijadili wakati wa Ubunge. Nipo katika rekodi nikihoji mantiki ya kurudisha fomu dakika za mwisho. Tukasema kuna technical issues ambazo Wapinzani lazima wajue namna ya kuzikwepa.

Katika mazingira ya leo hilo haliwezi kutatua matatizo wanayoyapata
Mbunge hawezi kufanya kampeni nje ya eneo lake.
Akiwa ndani ya jimbo lake haruhusiwi kuongelea jambo lolote isipokuwa ''shida''
Huyo compliance officer atafanya nini?
Mwenyekiti wa chama cha upinzani haruhusiwi kufanya maikutano nje ya jimbo lake.
Iwe ni ACT au Chadema! Compliance officer atafanya kazi kitongoji gani?

Shughuli za siasa hadi 2020, compliance officer atafanya kazi lini na wapi?
I mean tuweni wakweli wa nafasi zetu Mwenyekiti wa chama haruhusiwi mikutano, huyo compliance office atatoa mafunzo wapi? NCCR? ACT? Kuna unforced error lakini tusifumbie macho uhuni unaoendelea kwa kisingizio hicho. Unaamini kabisa CCM wamejaza fomu kwa usahihi nchi nzima na kwamba walikuwa na Wanasheria kila kitongoji! Kuchukua fomu kunahitaji ufundi gani? Watu walikatwa mapanga kuchukua fomu! Hawa waliokatwa mapanga walifanya makosa gani ya kiufundi?

Kuna makosa ya Upinzani na moja ya hayo nimelieza katika uzi wa Mwanakiji wiki moja kabla.
Kwamba mazingira yaliyopo yalitengenezwa watu wajiandikishe ili kujenga uhalali wa uchaguzi

Watu wamejiandikisha , kilichofuata ni kuengua wagombea. Hili mbona wengine tuliliona hata kabla ya juzi au jana. Tuliwaambia Wapinzani wanachokifanya ni jaribio la kuhalalisha madhaifu.

Leo nashangaa wanalalamika!

Nasi wananchi tuna shea yetu. Tumekuwa ''partisan'' au washabiki sana kiasi kwamba tunadanganywa na akina Mwenezi na kukubali kuwa kuna makosa wamefanya wapinzani
Hatujishughulishi kuangalia kama kuna ukweli, tunalaumu tukifumbia macho mapanga vichwani

Hivi kazi za compliance officer kutoa mafunzo kwa watendaji wa chama ni sawa na mwenyekiti kufanya mkutano wa kisiasa?

Nauliza tu ili niweze kujua kama kuna utofauti?

Lakini, licha ya changamoto zilizopo, my suggestion/ idea is worth a try!
 
Kama hukai na kupata riziki zako Tanzania basi usiwe na kiherehere kuchagia kitu. Mwanakiiji uliiimbia Tanzania basi kwenye mambo yao magumu wewe nenda kanunue baga uvimbiwe.
 
Vp Mzee Mwanakijiji imeingia Nini, mbona Kama sio akili zako. Hebu ichomoe usome upuuzi uloandika
 
Hivi kazi za compliance officer kutoa mafunzo kwa watendaji wa chama ni sawa na mwenyekiti kufanya mkutano wa kisiasa?

Nauliza tu ili niweze kujua kama kuna utofauti?

Lakini, licha ya changamoto zilizopo, my suggestion/ idea is worth a try!
Inaweza kuwa tofauti kwa sisi, kwa sababu dhamira ni mbaya hiyo ni sababu tosha

Kama Mbunge haruhusiwi kuongelea jambo jingine ila shida za wananchi! compliance officer je!

Kuna watu wa upinzani ambao si Wabunge na ''designated'' kama compliance officer, wamesweka ndani.

Hivi NN hujui kwamba dhamira ni kunyamazisha Wapinzani ikiwezekana kuwafuta?

Kama Bashe na Msukuma waliwekwa ndani ili kutovuruga uchaguzi iwe compliance officer!

Mbunge mwenye Jimbo hafurukuti leo iwe compliance officer!

Unaamini habari kwamba CCM wameweka Wanasheria kila kitongoji!
Please
 
Binafsi sina tatizo la kinadharia kwa CHADEMA kujitoa kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Na hata sitakuwa na shida ya msingi hata wakijitoa Uchaguzi Mkuu. Tangu zamani nilikuwa naamini kuwa kama unaona hutendewi haki ni lazima uoneshe kuwa kweli unaamini hakuna haki. Baadhi ya matatizo ambayo yametokea mara kwa mara - na sijui kama watu wamesahau au la - ni kuwa mara nyingi CHADEMA wanajikuta wanabanwa kwenye "masuala ya kiufundi" (technicalities).

- Kuchelewa kurudisha fomu hadi siku ya mwisho, saa ya mwisho
- Kuchelewa kula kiapo, au kula kiapo kisicho sahihi (nakumbuka sana kilichotokea Mbeya Vijijini mwaka uleeee)
- Kutokujua wanarudisha fomu kwa nani (Korogwe)
- n.k

Sasa, ni lazima tujue kuwa CCM na Serikali yake hawajawahi kuwa na mpango wa kutengeneza mazingira ya Upinzani kufanikiwa. Hili nimeliandika mara nyingi huko nyuma haifai kulirudia. Sijui kwanini wapo wanaofikiria kuwa Papa atajikata, atoe mafuta yake, akuwekee moto na sufuria, halafu ajitumbukize wewe kazi yako iwe kumkaanga tu! Sikumbuki mahali popote hili limewahi kutokea. Kutegemea CCM kuwasaidia wapinzani kuja kuwaondoa madarakani ni ndoto za Alinacha.

Baada ya kusema hilo, kufuatia uamuzi huu wa Chadema kujitoa kwenye kushiriki binafsi nilitarajia mambo kadhaa yangeelezwa kwanza, maana tusije tukawalaumu wasimamizi wa uchaguzi n.k kwa makosa ambayo yangeweza kuepukika. Kwa anayejua naomba atusaidie:

1. Ni nani alikuwa Mratibu wa CHADEMA wa wagombea wa nafasi mbalimbali serikali za mitaa kitaifa?

2. Huyo mtu/watu alitoa maelekezo gani kwa wanachama wa CDM kuhusiana na ujazaji wa fomu, kurudisha fomu n.k?

3. Je, CDM kitaifa ilitoa mwongozo gani kuhusiana na wagombea wake; kwamba wanahitaji nini na wajazaje fomu? Hii inaitwa "covering all your bases)

4. Hata mahali ambapo mikutano ya ndani isingewezekana CDM kitaifa ilifanya juhudi gani hata kupitia mitandao ya kijamii (Facebook, Youtube, au hata hapa JF) kuwajulisha wagombea wake jinsi ya kujaza fomu n.k Yaani, Freeman Mbowe au Katibu Mkuu Mashinji wameshindwa kuanzisha hata thread moja yenye maelekezo na nakala za fomu za mfano za nini kinatakiwa zikawekwa hapa?

5. CDM iliwaandaa watu wake vipi kubanana na wale wasimamizi ambao walikuwa wanaonekana kweli kuwakwepa. Hivi kweli CDM na vijana wake hakuna watu wenye kusema "hatutoki hapa hadi mpokee fomu zetu"? Ni upinzani gani huu!

Haya ni baadhi tu ya maswali yangu kwa sababu tusije kuwalaumu ama wagombea na wale watia nia au wasimamizi. Tujiulize kidogo CDM inawajibika vipi kuwandaa wagombea wake maana msipojibu maswali haya mtakutana tena 2020 na mambo yale yale.

Pendekezo Moja: CDM ije na sera ya wazi na maelekezo ya wazi kuwa wagombea wake wote wahakikishe wanarudisha fomu siku tano kabla ya mwisho wa siku iliyowekwa. Mtashangaa tofauti itakuwa nini hapa.
We ni kibaraka wa ccm
 
Leo tunaona Wapinzani wan matatizo, walipokuwa wanakatwa mapanga tulikuwa kimyaa!

Pamoja na fyongo na kubofoa kwa Wapinzani, kuna wakati kuwe na ka-aibu ka kuwasema!
Fyongo zao ni nyingi lakini haziwezi kufanyiwa ''trade'' na uhuni

Tumekubali kabisa maneno ya Katibu mwenezi wa chama kwamba CCM wameweka wanasheria kila kitongoji na mtaa na kwahiyo tatizo ni Wapinzani!

Tunajadili propaganda kwa dhati kabisa hata kama akili zetu zinatunong'oneza kuwa katibu mwenezi kadhalilisha chama na Taifa! kawatia aibu vijana na kizazi hiki

Katibu mwenezi hana sababu za kueleza fyongo ! angekaa kimya kusingeharibika jambo
Kutufanya mazuzu ni kulidhalilisha Taifa hasa kutoka kwa mtu anayetoka chama cha Nyerere

Tumeacha kuongelea madhila ya uchaguzi tunashadidia propaganda za mwenezi

Please ifike mahali tuzisikilize nafsi zetu na kuheshimu fahamu zetu!
 
Maswali haya naona yanahusu hata ACT Wazalendo... ni katika kuelewa masuala ya upinzani hasa kwenye mazingira ambayo wanajua kabisa hawawezi kutendewa kwa haki.
izo njaa zitasababisha muoelewe wanaume, yaan watendaji kutokufungua ofisi ujaliona hata kidogo, we hamnazo kwakwel
 
Wazo Gomvi: Kabla ya Kujitoa CHADEMA Ingeeleza Hili Kwanza...

Hivi kweli CDM na vijana wake hakuna watu wenye kusema "hatutoki hapa hadi mpokee fomu zetu"? Ni upinzani gani huu!
Mzee mwenzangu, huyu kweli ni wewe? Napata wakati mgumu sana kuamini ninayoyasoma hapa yameandikwa na Mzee Mwanakijiji! Kitu gani kimekusibu mwenzangu? Kweli binadamu hujafa hujaumbika!
 
Nikiacha hilo la "maswali kuwa ya kipumbavu", ninakubaliana nawe kabisa katika hayo mengine uliyoyaandika kuhusu "kuwepo na technical zilizojitokeza...."

Lakini, pamoja na kukubaliana nawe katika hilo, je wewe huoni kwamba kama CHADEMA waliyafanya maandalizi ambayo Mzee Mwanakijiji kayawekea maswali, kwamba hiyo ni kwa faida ya CHADEMA yenyewe?

Mimi ningependa CHADEMA wawe wameyatimiza yote hayo yaliyowekwa kwenye maswali ya mleta mada, kwa sababu kuu mbili:

Mosi, huo ndio ungekuwa ushahidi usiopingika kwamba CHADEMA wamehujumiwa kwa sababu watu wao waliandaliwa ipasavyo, na wasingeweza kufanya makosa yanayodaiwa waliyafanya na kutopitishwa kuwa wagombea. Tungejua bila ya shaka yoyote, kwamba hizi ni hujuma zinazofanywa na watumishi wa serikali.

Pili, kufanya yote yale yaliyoulizwa kwenye maswali ni kuiimarisha CHADEMA yenyewe, hadi katika ngazi za chini kabisa. Ni mpuuzi gani atakyechezea CHAMA chenye wanachama walioiva barabara na kuzijua haki zao ipasavyo. Hao wanaofunga ofisi na kukimbia wasingethubutu kamwe kufanya upuuzi huo.

Naomba CHADEMA wayajibu maswali yaliyowekwa na Mzee Mwanakijiji.
Unataka cdm waoneshe ulaghai kama walivyofanya Ccm Kwamba walipeleka mawakili elf moja ili kuhálalişha uhuni. Kukubaliana na hoja za Polepole ni kukubali ujuha.
Lakin pia umesau kuwa CDM wanakatazwa na polisi mpaka vikao vya ndani,,hyo sensatization wañgefanyiá wapi?Tusijifanye hatujui kwa kuuliza maswali yaliyojaa upofu mtupu
 
Back
Top Bottom