Wazo Gomvi: Kabla ya Kujitoa CHADEMA Ingeeleza Hili Kwanza...

Wazo Gomvi: Kabla ya Kujitoa CHADEMA Ingeeleza Hili Kwanza...

Mapendekezo ya wagombea ni suala la wananchi husika ku propose kiongozi wanayemtaka.

Hizo technicalities lazima ziwe rafiki kwa uchaguzi, kwa mfano kama mtu ni jambazi na ana record hiyo ni automatic rejection.

Lakini kuongeza vipengele utafikiri mtihani wa form IV , hiyo ni kuua demokrasia.

Mimi CCM damudamu lakini nisingependa kushindana na ombwe.
Paragraph yako ya tatu, umetoa utumbo na firigisi badala ya hoja,. Kwahiyo kama mwenyekiti wa serikali za mtaa hana uwezo wa kuandika vizuri anakuaje kiongozi katika karne hizi ambazo kila mtaa una DIGRII za kutosha.

Technicalities haziwezi kukimbiwa kwakua ndizo zinazoibeba tasnia ya Sheria duniani, namna vifungu vinavyo tafsiriwa, na ndipo tunapoweza kumpima mwanasheria.

Hivyo ukikutwa na kosa la "technicalities" usilalamike tafuta sheria inayothibitisha kinyume na hicho walichosema.

CCM waliangalia udhaifu wenu na kuufanyia kazi, ni wakati nanyi kuangalia udhaifu wao ili muwapige bao.
 
Uongo utakusaidia nini ?
Unajua kabisa nasema ukweli
Hiyo nafasi bora wangekupa wewe,tatizo unatoka nyanda za juu kusini
Sisi ccm tunajua shughuli yako pale temeke,hulali unahaha kuhakikisha wagombea wako wamejaza fomu vizuri,na kuhakikisha wanapata wadhamini wasio mamluki.nakumbuka ulikua mpaka unawanunulia chai na chapati wagombea ili tu wasiwe njaa wakarubuniwa.
Huyo mrema hajui kazi hata wewe unajua hilo
 
Hata kama Chadema wangekubali kushiriki uchaguzi, Mimi nisinge nyanyua mguu wangu kwenda kupiga kura.

Maneno ya huyu mzee yana ukakasi sana na yeye yupo behind na yale wanayofanyiwa wapinzani.

Sijui kwanini CCM mlimpitisha huyu firauni na hatimaye amekuja kuwa rais .View attachment 1257938
Hata kama umesema kweli bro heshima iwepo basi...
 
Hii ndio aina ya watu wenye ndoto za kuitoa ccm madarakani, SILIONI HILO LIKITOKEA ANGALAU KWA MIAKA HII YA KARIBUNI.

KWANINI
Malalamiko sio hoja. Hoja unatakiwa kujibiwa je? Mlijipanga vipi na mliwapanga vipi wagombea wenu, kuhusu taratimu na hoja za kifundi zinazoweza kuwaondoa wagombea wenu?.

Hivi wewe ungekua mwalimu umemwambia mtahiniwa kuandika kuandika sentensi ya kiswahili alafu akaandika NAOMBA KUGOMBEA SERIKALI ZA MITAA ungelimpa vema?

Je! Ungeenda kituo cha polisi au mahakamani ukaulizwa unafanya kazi gani ungemjibu hakimu kwamba wewe Ni MPAMBANAJI?

Ifike wakati tujifunze kuheshimu taratibu kwakua muhusika anahiari ya kukuonyesha huruma au kukuchinjilia mbali na usipate pa kwenda kushitaki.

Mzee Mwanakijiji, hawa watoto na wazee wenzio pia watakukashifu, watakutusi na mbali ya yote watasema unatumika.

Na kama utakua unatumika kweli utakua unaitumikia akili na Muumba wako na si chengine.

Unachekesha walionunua, kwa taarifa yako kulikuwa na zoezi la uchaguzi sio mtihani wa kujaza fomu, maana hata kama kungekuwa na mtihani wa kujaza fomu basi kungeendeshwa somo hilo kisha mwishoni kuwe na huo mtihani. Tueche hayo, je ile mizengwe ya kutoa fomu dhidi ya wapinzani na kujificha kama mchezo wa watoto, ilikuwa ni sehemu ya huo ushenzi? Watu wameshaamka zamani bado nyie mna mbinu za kizee zenye kutegemea mitulinga ya vyombo vya dola?
 
Lumumba wanajitoa akili makusudi
wewe mzee unazidi kuwa mjinga kadri siku zinavyozidi kwenda, mbona hujahoji kwann watu walikua wanafunga ofisi? mbona hujahoji kwann walikua wana-edit fomu za wagombea wa upinzani?....


hv huu ndio uchaguzi wa kwanza kufanyika tanzania? mbona 2014 haikua hivi?..... hebu punguza ujinga mzee
 
To hell with technicalities,demokrasia haijengwi juu ya technicalities zisizo na logic bali juu ya uwakilishi unaokubalika na wengi na imani kwamba wengi wam, baesikilizwa.
Technicalities zako zinasaidia au zinafanikisha nini i, kiwa zinamuondoa mtu ambaye alikuwa apate asalimia 60 ya kura na kumbakisha aliyekuwa apate asalimia 20 ya kura?
waambie wenzako kujifunza kufuata sheria kanuni na taratibu.. hatutaki kupita kwa kuhurumiwa noooooo...taratibu zooote zipo wazi kwa nini hazifuatwi kama sio hujuma tu ni nini....lakini nasema wananchi tunajua, baada ya kuona Magufuli na serikali yake wapo kila angle ya nchi, wapinzani wakaona hakuna watakapochomokea..wakaona waunde mkakati wa kujaribu kupata huruma kwa wananchi. hahahaha mnatyfanya wananchi wajiiiiinga hawajielewi......tafyteni mkakati mwingine huu umefeli
 
Maswali haya naona yanahusu hata ACT Wazalendo... ni katika kuelewa masuala ya upinzani hasa kwenye mazingira ambayo wanajua kabisa hawawezi kutendewa kwa haki.
maswali yako yote uliyoandika ni ya kipuuzi kwasababu watendaji wakipokea hata form ambayo imejazwa vizuri wanaongeza maneno yao kwenye form husika ili kuiharibu kama walivyoagizwa kwenye semina elekezi Ikulu.

Mzee mahaba ya kisukuma yamekuzidi nguvu hadi umekua unajenga hoja dhaifu kuliko hata Nabii Tito.
 
Mzee una habari kuwa ACT ilikuwa na watu 173,593 walioomba kugombea kwenye serikali za mitaa lakini kati yao watu 166,649 Wameenguliwa, yaani 96% ya waliogombea kupitia ACT wameenguliwa je unalijua hilo?

Je una habari kuwa 97% ya waliotaka kugombea kupitia Chadema wameenguliwa?

Hizo percentage na idadi ya watu ndio inaleta utata, Inawezekana kati ya watu 173593 ukasema 166649 eti hawana vigezo, hapo ratio inakataa anagalau ingekuwa hata 20% lakini zaidi ya 90% wote hawana vigezo. Pia nafikiri lilikuwa jukumu la Tamisemi kutoa elimu kwa wagombea namna ya kujaza fomu kama kuna hali hii imejitokeza, Bado Tamisemi hawajachelewa kama wana nia ya dhati ya kutenda haki wasitishe zoezi na kutoa elimu kwa wagombea ikiwezekana watoe hata msaada kwenye kuzijaza..

Si vyema watanzania tukashabikia haya yanayoendelea, kama jambo ni jema huwa ni jema tu na kama jambo ni ovu huwa ni ovu tu hakuna lugha nyingine ya kugeuza zaidi ya jamii ya watu wanaojitambua na walioendelea kukuona ni mjinga pale unapoita spade nyundo.. Ujinga ukiachwa ufanywe kwa kuwa anayetendewa hakuhusu au ni adui yako basi elewa tu kuna siku ujinga utafanywa pia kwako na mtu mwingine.
 
Wagombea zaidi ya 150000 wa ACT wameshindwa kujaza fomu kwa usahihi halafu wagombea wote wa CCM wamepatia kujaza hizo form kwa usahihi.

Hapa Mkuu umepotoka jaribu kufikiri tena, Tuache ushabiki usio na maana sote ni Watanzania..
 
Paragraph yako ya tatu, umetoa utumbo na firigisi badala ya hoja,. Kwahiyo kama mwenyekiti wa serikali za mtaa hana uwezo wa kuandika vizuri anakuaje kiongozi katika karne hizi ambazo kila mtaa una DIGRII za kutosha.

Technicalities haziwezi kukimbiwa kwakua ndizo zinazoibeba tasnia ya Sheria duniani, namna vifungu vinavyo tafsiriwa, na ndipo tunapoweza kumpima mwanasheria.

Hivyo ukikutwa na kosa la "technicalities" usilalamike tafuta sheria inayothibitisha kinyume na hicho walichosema.

CCM waliangalia udhaifu wenu na kuufanyia kazi, ni wakati nanyi kuangalia udhaifu wao ili muwapige bao.
Acha mihemuko.
Soma na uelewe mchango wangu kwenye mada.
Hii mihemuko ndio inawafanya watu wasiwaheshimu kwa vile unafikiri Tanzania ni ya watu Fulani.
Nimekuambia mimi ni kada, tena wa siku nyingi tu.
Tanzania hii ni ya watu wote na usifikiri ndani ya CCM nd kuna watu wenye akili.
Kama wewe ni mfano wa watu kama hao basi chama ni kama kuku aliyechinjwa na kichwa hakipo.
Na kwa taarifa yako ninakuhesbu kama mtu usiye na akili sana maana umeniquote katika paragraph ya tatu wakati nina mistari michache tu, hapo usomi una kasoro.

Ushindani mzuri ni kushindana na wenye akili, tusitake kushindana na ombwe tunalolitengeneza kwa makusudi.
 
Miaka haigandi; kwani kabla ya 2014 watu walikuwa hawaenguliwi? au 2014 wagombea wote wa upinzani walipitishwa? Au mmeshasahau?


Dah!
we jamaa ni empty kabisa na hasa apo uliporudia tukio la Korogwe, naamini unafanya makusudi na unajua unalolifanya,
kifupi Ukatoliki na Ukanda unakumaliza.
 
Wewe mzee unazeeka vibaya Sana... Au ndo ushaula ubalozi Kama ndugu yako Dr. Slaa??
 
Maswali haya naona yanahusu hata ACT Wazalendo... ni katika kuelewa masuala ya upinzani hasa kwenye mazingira ambayo wanajua kabisa hawawezi kutendewa kwa haki.

Mzee Mwanakijiji,
Sasa wazeeka vibaya…!
Hoja ulizotoa hapa ni dhaifu sana,hazina mashiko wala hazijengi! Kazi ya kuelimisha wapiga kura na wagombea ni ya Tume ya Uchaguzi kwa Uchaguzi Mkuu au Tamisemi na Wakurugenzi wake kwa Uchaguzi SM ambao ndio WASIMAMIZI au marefa wa mchezo!
Hapa ndipo chanzo cha vurugu zote hizi! Haiwezekani refa asimamie mchezo ambao timu yake(CCM) ndiyo inacheza na timu shindani(UPINZANI)…halafu utegemee FAIR GAME……never ever!a
Iwe ni CHADEMA,ACT Wazalendo,CUF etc hata wangeendesha elimu ya Uchaguzi mwaka mzima usiku na mchana bado wange enguliwa tu kwa namna yeyote ile!
Unategemea nini mgombea wa upinzani anaenda kuchukua au kurudisha fomu anakuta ofisi zimefungwa? Unategemea nini hata baada ya kuwasilisha fomu inachakachuliwa kwa kubadilishwa baadhi ya vipengele kama KE na ME zinawekwa TICK zote maksudi eti ionekana kwamba mgombea ana jinsia zote 2.....! Haiwezekani ati wapinzani wote katika vitongoji,mitaa na kata zote wakosee kujaza fomu kisa chama hakikuwaelimisha jinsi ya kujaza fomu......!! Hii ni hoja mfu na inanuka uvundo!
 
Wewe lizee hovyo sana ulitaka warudishe wapi form wakati watendaji walikuwa mafichoni kuwajazia wagombea wa ccm?

Kwani CHADEMA ni mara yao ya kwanza kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa?

Ni kwanini wagombea wa vyama vya upinzani tu ndiyo wameenguliwa kwenye uchaguzi ?

Hivi unataka kusema kwamba wagombea wa chadema wameenguliwa kwa uzembe wa chama ?

Kifupi wewe mzee unazeeka vibaya. Nasikitika sana kuwahi kupoteza muda wangu takribani 6 years nikisoma makala zako magazetini.

Mh!? Huyu kumbe ni mwandishi? Dah!? Mungu wanguuuu
 
Yaan mkuu huoni kilichofanyika?...waru kunyimwa.haki makisudi na waziwazi...?
Siku hizi umekuwaje...yaan na akili zako hizo unaona ni kosa chadema..kwamba wagombea asilimia 90 walioenguliwa walikiwa hawazijui taratibu?..real!?...

Msameheni inatosha
 
Back
Top Bottom