Wazo la biashara kwa 100m

Habar ndugu. Kwanza niwie radhi kwa neno la posho ya kikao limeleta sura ya kujimwambafai na kukosa humbleness, na nimefuta tayar, umenisuta kwa akili.
Pili, naomba idea ambayo ni sustainable. Kwa vile itakuwa kwa mfumo wa kampun uwe shareholder.
Hapana wala sijakusuta mkuu ila kweli nitaimic hiyo posho. Si unajua jinsi hela ya posho ilivyo tamu. Hizo zote mbili ni sustainable na ni promising kulingana na country's growth factors.
 
ekari 500? Shubhaaaamit watu mko na vision za mbali sanaaaaa
 
Wazo zuri.
Tangawizi pia zinalimwa Madaba,Ruvuma na Same .
 
Yakigoma mwana si Kala hasara
 
Nenda Morogoro, possibly Mlimba au maeneo mengine yanayolima mchele. Nunua mchele weka stock. Ndani ya miezi kadhaa tu, possibly baada ya miezi sita, hiyo mil 100 itakuwa imegeuka na kuwa mil 300!. Kama sivyo, basi the minimum ni mil 250+
Ubarikiwe
Sio rahisi kihivyo
 
Ngoja nikushauli ujinga ukiona umekosa cha kufanya anzisha mirad ya mashine za kusaga tafuta sehem nzuri iwe kukodi chumba au kujenga kibanda ukifanikiwa kuweka sehem 4 unauhakika wa kulaza kima cha chini laki 6 kwa kila wiki hadi uzeeni kwako na hiyo ni faida tu haina makato wala ushuru

Ukiona hiyo ishu ni pusi njoo tufanye biashara ya makaa ya mawe ruvuma to mwanza au mtwara to kenya toka kukod gar kuyanunua, vibari mpaka kuyapeleka sehem husika itakugharim m2 faida yake ni kama laki nne hivi yaani we ni kupakia mzigo sokoni kutokana na speed yako na mtaji kama unauwezo wa kufikisha sokoni gar tano zenye ujazo wa tan30 basi fanya laki nne mara tano hiyo ni faida kwa siku uliyopeleka soko uhakika kama hujaelewa nitafafanua
 
Habari Mkuu;
1. Spice, Herbs and Fruits value addition/processing.
a. Extracts (Spices, herbs and fruits)
Extract maarufu kuliko zoteni Vanilla, ingawa zinaweza andaliwa nyingine nyingi kama mango, apple/cider, tamarind, pineapple, orange, lime, lemon, lemongrass, cinnamon, mint, rubber vine fruit, ginger etc. Tanzania matunda yapo mengi(moja ya marketing ideas ni ku-provide a taste of ''exotic"). Malighafi zote zipo, na vitendea kazi vyote vinapatikana hapa bongo. M
Masoko ni mtu binafsi, mama/baba ntilie, bakery zinazofunguliwa kila siku, restaurants, hotels etc.

b. Essential Oils(Spices, herbs and some fruits(parts of a fruit(s)))
Essential oils ni mafuta yatokanayo na viungo na mitishamba mbalimbali, kama ganda la chungwa, limao(lime, lemon), cinnamon, cardamom, lemongrass, mint, eucalyptus leaves, pine needle leaves, ginger, garlic, rosemary, rose(the flower), na serikali ikija kuufikiria bangi(CBD essential oil) etc.
Matumizi ni Aromatherapy, Pharmaceutical na Food&Beverage sectors.
Masoko ni watu binafsi, vituo vya massage, wellness and relaxation Spa, kama ingrident ya sabuni na perfume (Essential oil tutakayozalisha ikiwa Aromatherapy grade).
Makampuni ya dawa(kama essential oil tutakayozalisha itakuwa Pharmaceutical grade).
Makampuni ya vyakula na vinywaji(food and beverage) kama essential oil tutakayozalisha itakuwa Food grade.

c. Oleoresins( Spices and herbs)
haya ni mafuta-mgando(semi-solid) yatokanayo na uchakataji wa viungo na mitishamba. Yanasifa ya kuwa na vitu vingi zaidi ya essential oils.
matumizi yake ni mengi kuanzia utengenezaji wa mabomu ya machozi (vurugu zitokeapo, yanatumika sana kote duniani) mpaka kwenye mapishi,vinywaji, rangi za chakula na vinywaji.
Mfano ni ginger, turmeric, garlic, onion, cinnamon, cardamom etc.

NB; Kama utakuwa huru na kukubaliana na uwekezaji katika maeneo mengi tanzania, nitatoa idea nyingi zaidi.
NB: Mtaji wangu ni idea(wazo), bado sijafanikiwa pesa.
Ahsante.
 
Makaa ya mawe ungedadavua kidogo ingependeza mkuu
 
Kiwanda kidogo cha kutengeneza trays za (box/karatasi) za mayai.
Malighafi ni mabox yaliyokwisha tumika.

Hapo kwenye hiyo 100M na "chenji" inabaki.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…