Wazo la kuanzisha public library hapa green city-Mbeya mjini


Hatuwezei kusogea mbele kama ujinga utaendelea kututawala. Naamini sote tukionyesha kwa mifano umuhimu wa kupenda kujisomea, tutabalika na kubadilisha na wengine pia.
 
NDUGU UNAELEWA KWA HABARI YA Social Enterprise? PROPOSAL NINAYO MIMI, EVERYTHING IN DOUBT KIMEJIBIWA HUMO. WADAU WAKE WAPO!!


Tunakueleza humu ni kwa "GOOD FAITH", so usichukulie kama ni watu ambao wanakupinga ili tu waonekane wanakupinga, hatujuani humu!! sasa tupingane for the sake ya kupinga ili iweje?mwisho wa siku ni wewe utakayeenda kuapply hilo wazo utakayenufaika au kuathirika na uamuzi huu, ni vizuri yachukue mawazo hayo positively, japo mwisho wa siku muamuzi ni wewe.
 

sioni good faith hapo, kama lazima kunishauri basi iwe positive kweli sio kudhihaki, maneno ya ovyo nk. Kuna wengine wameshauri vizuri nimeona.
 

sas haya ndio mawazo chanya ambayo kwakweli kama msomi nzweza kuyachukua na kufanyia kazi. Pia demand unaipateje kama hujafan yua analysis na study ya uhakika? Mimi sijaanzisha, niko na wazo na ndio nafanyia utafiti wake, mwishoni nitaamua vyema, i am a good planner, hata hivyo sianzishi ili kuanzisha tu, nimekwambia ni proposal, i need to test my hypothesis. Naona baadhi ya wachangaji wanaelewa wazo langu, hata kama halitaishia kufanyia utekelezaji, ila naamini change ya mindset za watu hutokea endapo social enterprise zitakuwepo. Na katika hii proposal sijasema kuwa niko profit oriented au la kwanini wengi mnadhani nimelenga profit tu?
Kwakweli kuna watu hawajanielewa; hili ni wazo sio utekelezaji.
 
Comment hii lazima imetoka kwa mtu asiye msomi, na kama msomi, hajaelimika!!!! asiye jua maana ya proposal, wala kuelewa content ya hoja husika. Poor msomi!!!

Huyu Utingo atakuwa si mzima kichwani .Aiwezekani mtu alete mada nzuri kama hii harafu umpe shutuma hizo hauko sawa kabisa.

msitukane bila kuwa na facts. Mtu wangu wa karibu alitaka kuanzisha hiyo biashara dodoma, wakati wa kutafit akapita central Library Dar...akakata tamaa.

Ninyi wenyewe ni mara ngapi mmeingia makataba kujisomea kama si nyakati zenu na kujiandaa kwa mitihani? Achane kumdanganya mwenzenu waapuumbavu ninyi
 

kweli utingo ni utingo tu hajui hata kushauri lazima atukane ktk ushauri wake.
 
sioni good faith hapo, kama lazima kunishauri basi iwe positive kweli sio kudhihaki, maneno ya ovyo nk. Kuna wengine wameshauri vizuri nimeona.

Mkuu wangu, hatulazimishi upokee mawazo yetu, ila ni kwa faida yako kwani itakusaidia kwenye SWOT(Strength, Weakness, Opportunity and Threats) analysis yako.

Kingine, kwenye kugenerate wazo la biashara usiwe rigid, be open-minded, ndio maana brain storming, hii stage ni very important na hauwezi kuifanya vizuri kama tayari umejilimit kwenye majibu ambayo tayari unayo, maana kama ulikuwa na majibu yote then umeileta hapa ya nini?usiwe kama wale wanasiasa wanaotaka kupigiwa makofi tu, pokea na majibu tofauti positively.

Kwa faida ya wote watakaosoma na kwa vyovyote utakavyotafsiri, hili wazo kwa Tanzania halilipi na haliwezi ata kuifanya hiyo biashara ijiendeshe, na yeyote atakayefanya hii kama biashara atakuwa disappointed sana maana anaenda kutupa pesa yake.

Best Wishes.
 

Ukitoa hiyo sentensi ya mwisho, hayo uliyaongea ni kweli kabisa.Atakayebisha ni kwa sababu hataki kuuona ukweli.
 
kweli utingo ni utingo tu hajui hata kushauri lazima atukane ktk ushauri wake.

Hizi sio lugha kwa mtu uliyeleta mada unayeomba ushauri.

Ukimsoma vizuri huyu kaongea kwa uchungu kwa sababu anaona huruma kuwa labda utaathirika kwa uamuzi huu.

Kumbuka sio wazo lolote la kitabuni linatekelezeka kila sehemu na kwa kila wakati, japo hilo haliondoi ukweli kuwa ni wazo zuri bali tatizo tu ni kuwa sio wazo sahihi kibiashara kwa mazingira yetu na kwa wakati huu.
 

I can understand now.

Ni wazi kuwa hii biashara hauendi kuimplement wewe mwenyewe bali unataka kuiuza kwa mtu au watu akafe nayo mbele ya safari, na ndio maana huwezi kupokea mawazo negative kwa sababu ya hofu tu ya kuwakatisha tamaa watu kununua hii plan au kuona kampuni yako imetoa business idea/ushauri ambao hautekelezeki kwa mazingira yaliyopangwa kutekelezwa.

Lakini, ni muhimu sana pamoja na proposal tunazoweza washauri watu hizi zinazofanyika nchi nyingi tu za ulaya, Amerika na Asia ni vizuri tujizatiti sana kwenye SWOT analysis vizuri na tuangalie sana uendelevu wa wazo hilo kwa kuangalia mazingira yetu.Sio kila wazo la ulaya na Amerika linafaa Afrika.

Ungejikita hapo vizuri usingeweza kumshauri mtu afanye hiyo biashara iwe Mbeya au Mkoa wowote Tanzania, otherwise ndio ile ya kuwa out-of-touch of the real situation on the ground.

Ila kama unaiweka kama reference tu, it is well and good.
 

hakuna tabu, hili ni wazo langu, nikimaliza kuliandalia bplan ndo litanipa jibu halisi;nashukuru kwa michango yenu japo, mmechangia as if nimemlazimisha mtu kuelewa proposal yangu, japo liko ktk idea tu. Huwezi mtu ukakata tamaa kwa kuwaza tu bila facts and figures kuwekwa wazi. Mtu anazungumzia swot ya mradi huu bila kufanya kihalisia.
 
kweli utingo ni utingo tu hajui hata kushauri lazima atukane ktk ushauri wake.

Asante sana kwa matusi yako....lakini inaonekana hujui na hujafanya utafiti kuhusu kile unachotaka kuanzisha, means ya income na kadhalika...kwa kukushauri nenda British council Library na makataba ya taifa na hata za mikoa uulize watakueleza ikiwa mapato ya uanachama wa maktaba unatosha kuendesha maktaba bila ruzuku? fuata ushauri wa vipofu wenzako...utarudi humu unalia.

ningekuona wa maana kama una mpango wa kuanzisha bookshop ya vitabu pillar ikiwa vitabu vya shule za msingi na secondary maana biashara hiyo inalipa na hasa ukijiconnect na headmasters.

Kumbuka kuwa siku hizi watu wanasoma Undergraduate na hata Graduate kwa kudownload materials kwneye linternet (ambazo ni latest)....usifute ushauri wa kike...be a man face the fact...biashara ya maktaba ni ndoto. Membership ya tsh 20,000 kwa mwaka tu watu hamwingii na maktaba inapata ruzuku, wewe utaweka membership fee iwe ngapi ili ulipe mishahara, kodi, ununue vitabu etc....acha upofu dogo
 

Hili ndio tatizo la business idea za kucopy na kupaste.Hili sio wazo la biashara kwa Tanzania bali ni kwa Ulaya, Asia na America.

Sasa ukimkuta mtu maskini wa Mungu asiyejua A wala B ataingia kichwakichwa, analipa pesa kuchukua wazo ambalo sio applicable kwa mazingira yetu.

Ungefanya SWOT analysis ndogo tu, ili wazo ata usingelileta hapa, kwenye preliminary tu ungeshapata jibu.Na hili ndilo lilelile tunalolisema, ata wanaokwemda vyuo hawasomi vitabu wanaishia kusoma vitini na kudesa na matokeo yake ata wakitoa ushauri wanaishia kucopy na kupaste bila kuadopt kwenye mazingira husika.

Namuonea huruma utakayemshauri.
 

Mkuu, huyu jamaa hana mpango wa kuanzisha hiyo biashara, Huyu eti ni CONSULTANT WA BIASHARA anayeibua mawazo ya biashara na kusimamia uendeshaji wa biashara.

Yaan nchi hii ilivyojaa vishoka kila sehemu mpaka unachoka kabisa, sasa huyu NDIYE CONSULTANT eti na hawezi kudesign wazo bali ANACOPY NA KUPASTE bila kujua kuwa mazingira ya alipodesa na Tanzania ni tofauti, ata SWOT analysis kama aliifanya basi ilimshinda.

Sasa kama huyu ndio Consultant je huyo Client wake yupoje?atamfikisha wapi?ivi kipofu anapomuongoza kipofu mwenzake wataishia wapi?

Inasikitisha sana.
 

cha ajabu kuna mijitu humu inamsupport kuwa inawezekana....unajua humu kuna watu akili zao ni finyu sana kutokana na mazingira waliyokulia.

Chukulia scenario hii, mtu amezaliwa kariakoo, akasoma shule ya msingi mnazi mmoja, Secondary olevel na high school akasoma jangwani, au zanaki, au azania na au tambaza, chuo akasoma CBE dar campus....unategemea nini? Ndiyo kama huyu. Unakuwa na watu unawaona wasomi lakini mazingira walimokulia yamewaficha bongo zao they can not think beyond the box.
 

Yaan ni matatizo makubwa sana haya, watu wanakurupuka tu kucopy na kupaste kutaka kuwauzia watu mbuzi kwenye gunia bila ata kujua kuwa mazingira na demand ya huko walikocopy sio mazingira na demand ya hapa kwetu.

Wakiona kwenye internet jinsi library zinavyojaa huko Ulaya na Amerika na kuwa ni biashara ya uhakika basi nao anakurupuka tu bila ata kujua kuwa huko sio hapa na kuwa demand ni tofauti kabisa.


Picha: Wananchi wa Mbeya wakubwa kwa wadogo, wanaume kwa wanawake wamejazana library(NDOTO ZA MCHANA)


Eti kafanya analysis kuwa kuna demand, watu watakuwa wanakusanyika kwenye hiyo library kujisomea na kukutana na kufanya discussion ya masuala ya kitaalam?really?


Picha: Wananchi/wasomi/vijana wa wamekutana jioni/weekend wakijadialiana masuala ya Kitaalam, na ndivyo wanavyofanya kila siku jioni baada ya kazi na kila weekend.
(NDOTO ZA MCHANA)

Hivi kwani hao wasomi na wataalam walioko Mbeya kwa sasa uwa wanakusanyika wapi kujadiliana hayo mambo yao ya kitaalam??

Kumbuka hapa hazungumzii makongamano, warsha, semina au mikutano ambayo uwa inafanyika kwenye kumbi na wala hatuzungumzii vikao vya harusi ambavyo kwa Tanzania hufanyika pia kwenye ma-bar bali hapa anazungumzia ENEO LA KUJADILIANA MAMBO YA KITAALAM.

Sasa je tatizo hilo lipo? maana ni lazima kwanza kuwe na tatizo la eneo la hao watu kukutana ndio hiyo library sasa ije kutatua hilo tatizo, maana huwezi kubini mbinu ya kutatua tatizo ambalo halipo.

Picha: Wananchi/wasomi?vijana wamekutana jioni/weekend wakijadialiana masuala ya Kitaalam, na ndivyo wanavyofanya kila siku jioni baada ya kazi na kila weekend.(NDOTO ZA MCHANA)

Huu ni ukanjanja tu huu, kaona nchi za wenzetu watu wanakusanyika library kudiscus basi anadhani na hapa Tanzania basi ikiwekwa hii watakuwa wanakusanyika KUJADILIANA MAMBO YA KITAALAM, alafu eti ndio Consultant mwenyewe.

Akimkuta hapo mtu asiyejua atamwambia nimeishafanya analysis, mimi ni msomi, nimeishaona kitaalam, wewe anzisha tu hii ina soko sana, kumbe soko kaliona kwenye net huko Ulaya na Amerika alafu anawauzia wajinga mbuzi kwenye gunia yeye anachukua pesa yake anaishia wateja wanaenda kuimplement wateja wanazama na kufilisika, yeye hawatamuona tena.


Saiz vishoka hawapo tanesco na waganga wa jadi, sikuhizi kila aliyeweza kudesa huko chuo na anayejua kucopy na kupaste kutoka kwenye internet nae anataka aitwe Consultant na awalie pesa wasiojua.
 

mkuu, msamehe bure...huyu jamaa,si tu kuwa ni bingwa wa kudesa na kutofikiri pia kutokana na kudesa hawezi kutofautisha kati ya academic research na business research....academic research unaweza ukadesa na ukatwist data si business research inayohitaji genuine thinking, data and fact. ....huyu ni kanjanja! nawapo pole wanaojipeleka kwake kama wateja.
 
Utingo fani yako ni kwenye madaladala ,gereji na kukusanya nauli umu hapakufai kwanza una mdomo mchafu yani wewe kushauri hadi utukane huwezi ukashauri au kutoa mawazo bila matusi.

waombe uongozi wakuwekee jukwaa la utingo/kelele
 
Last edited by a moderator:
Utingo fani yako ni kwenye madaladala ,gereji na kukusanya nauli umu hapakufai kwanza una mdomo mchafu yani wewe kushauri hadi utukane huwezi ukashauri au kutoa mawazo bila matusi.

waombe uongozi wakuwekee jukwaa la utingo/kelele
Maneno ya busara ya Utingo yazingatiwe na matusi yasamehewe/yaachwe. Hii sio biashara kwa tanzania. Watu wanasoma wako undergraduate/graduate lakini hawaingii library halafu eti nyi mumshauri wazo hili aendelee nalo. mweeeeh...
 
Last edited by a moderator:
Utingo fani yako ni kwenye madaladala ,gereji na kukusanya nauli umu hapakufai kwanza una mdomo mchafu yani wewe kushauri hadi utukane huwezi ukashauri au kutoa mawazo bila matusi.

waombe uongozi wakuwekee jukwaa la utingo/kelele

wewe ni mpuuzi usiye jua matusi ni nini...mjinga akiambiwa mjinga hajatukanwa, ni kiwakilishi tu...utingo is just an ID si ajabu Utingo ni mwalimu wako chuoni. so shut the hell up!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…