WCB na mikataba ya ajabu: Ndio maana muziki wa Tanzania hauendelei

WCB na mikataba ya ajabu: Ndio maana muziki wa Tanzania hauendelei

Kwa hiyo wewe kinakuuma nini? Hukutaka aelimike? Kila mtu huwa ana pa kuanzia kabla ya kufikia mafanikio. Na yeye Harmonize pa kuanzia kwake palikuwa WCB, sasa kapata uzoefu kwa nini asisimame mwenyewe? unataka amtegemee Diamond mpaka lini? Nenda Harmonize kapambane kivyako. Jua tu kuna kushinda na kushindwa. ukishindwa basi tafuta tena pa kuanzia bila kujali maneno ya watu.
We ni Mpuuzii...Hujui Chochoto kuhusu Mikataba ndio maana mnafanana na hyu Harmo
 
Tatizo lipo wapi.
Music ni biashara kila mtu analenga faida
Kwani harmonize alijua kama angefik hapo alipofika leo..??
Kwan wcb kipnd wanainvest kwa harmo waliona angefika hapo ...??
Msanii gani wa wcb amepewa promo kuliko harmo..??

Na harmo alipewa promo ili mond awaprove watu wote wrong kwamba anaweza mtengeneza mtu akawa mkubwa.

Tatizo harmo anajiona big kwasababu ni mwaka sasa mond alikua hajatoa nyimbo
Mond akawa anadeal na media
Tobo kwa harmo likaonekana
Akapita
Alaf pia wale mashabik wa kiba ndo wanaosupport huu ujinga
Wale wale waliomkataa kipind cha aiyola leo ndo wanaona anakandamizwa
WCB waliona na walisha jua Atafika apo alipo na bado kuna long way to go ndio maana wali invest...uyu bwege alikua hajui chochote saiv ndo anajikuta mjaaanja asa ngoja
 
Najaribu kushangaa Leo wanaoona Hamo kutaka WCB ni kosa wakati hata huyo Mond alitoka sehemu na tukashangalia kabisa kuwa ni Bora walikuwa wanamnyonya nikwambie vijana wenzangu anayeijua tamu au Chungu ya ndoa ni Yule aliyemo kwenye ndoa kwa hiyo Hamo anajua kwanini ameamua kuondoka hapo
 
Hisia wakati ndio ukweli mwenyewe,kijana naijua Tasnia ya Bongo Movie kuliko unavyozani,kwani nipo nao karibu sana na najua kila kinachoendelea sizungumzi kumfurahisha mtu Music is Bussiness ambayo inahitaji mbinu ili kuikuza biashara yako,acha KUKURUPUKA KWANI HATUJUANI.

Najua detail nyingi za Wolper na kuna nyingine nikiziweka hapa nitakuwa namdhalilisha yy na mwanamke kiujumla.

Kama ulizani Drake na Nick Minaj au Mbosso na Queen Darleen au Harmonize na Wolper walikuwa wana date basi futa hilo akilini mwako,hayo mahusiona yalikuwa mbele ya TV na Social Media ili kutengeneza KIKI na biashara zifanyike watu waingize hela.

Neno HATUJUANI ndiyo jambo la maana zaidi uliloandika hapo juu, hayo mengine ni porojo za kujifanya unajua usivyovijua, na kama tungekuwa tunajuana usingeweza kuandika hicho ulichokiandika.
 
Ndio leo kausoma huo mkataba kauelewa kwani? siku zingine ilitumika ki spanish kwenye huo mkataba? Amepata wa kumtafsiria sio?

Kama anaondoka aondoke kwa amani,kujitetea kwa ujinga kama huu hakumfanyi apande juu ila ataonekana Punguani alie elimika after get into relation with sarah na huyo jembe ni jembe.
Ni sawa na kupigika na njaa halafu uone sahani ya chakula. Utakula tu, hata kama sio favorite yako. Unaamini usipokula njaa itakuua. Baadae ukizoea mazingira ukajua pa kujitafutia lazima ule unachokipenda sio unachokiona.
 
Hii comment nayo siyo rational kwani hata Diamond naye alihama hivyo hivyo kutoka label moja hadi nyingine, kubadilisha maproducers na mameneja kadhaa kabla hajawa hivyo alivyo leo; ndiyo process yenyewe. Siyo kuwa yeye ndiye atakayewamiliki wasanii wote wajao kwa vile amefikia levo hiyo; kuna watakaopita kwake na kwenda kijisimamai wenyewe na inawezekana wakaja ambao hawakupita kwake labda wakawa zaidi yake. Ndivyo nature ilivyo!
Kama ni hivyo kwanini mtoa mada analalamika harmo kupewa mkataba wa miaka 10 na WCB? je angepewa mkataba wa maisha huyu mto
Kwa hiyo wewe kinakuuma nini? Hukutaka aelimike? Kila mtu huwa ana pa kuanzia kabla ya kufikia mafanikio. Na yeye Harmonize pa kuanzia kwake palikuwa WCB, sasa kapata uzoefu kwa nini asisimame mwenyewe? unataka amtegemee Diamond mpaka lini? Nenda Harmonize kapambane kivyako. Jua tu kuna kushinda na kushindwa. ukishindwa basi tafuta tena pa kuanzia bila kujali maneno ya watu.
Ulichojibu na jamaa alichoongea ni vitu viwili tofauti mwenzako ana ongelea mkataba ambao mtoa mada anasema wa kinyonyaji ndo jamaa anasema Kama muhusika ameusaini yeyemwenyewe kwann alaumu uongozi wa Wcb? wewe unaongea kuondoka
 
Neno HATUJUANI ndiyo jambo la maana zaidi uliloandika hapo juu, hayo mengine ni porojo za kujifanya unajua usivyovijua, na kama tungekuwa tunajuana usingeweza kuandika hicho ulichokiandika.
Hata wewe tungekuwa tunajuana usingeandika ulichokiandika hapo.
 
Drake ameshajitoa YMCMB
Lil Wayne nae alishajitoa chini ya Birdman a.k.a Baby
Screenshot_20190826-135419.png
Screenshot_20190826-135419.png
Screenshot_20190826-135419.png
 
Kwa nini unakimbilia post za magazeti kwenye internet usisome makaratsi ya mahakamni yenyewe? Yanaanza hivi

View attachment 1190262
Ni karatsi 50, kwa hiyo ukitaka kutafsiriwa kwa lugha rahisi kutoka lugha za kisheria itakuwa ni vigumu kwa leo.


Halafu kama hujui malalamiko ya Kanye (niliyaandika huko nyuma) ni kuwa mkataba huo unatumia muda unaitwa "contract year" ambayo siyo miezi kumi na mbili bali ni kipindi ambacho Kanye anafikisha kutoa nyimbo kadhaa. Akifikisha idadi hiyo ndani ya miezi 12, basi mwaka inakuwa ni miezi 12, na asipotoa nyimbo zinazotakiwa kwa miaka minne, basi miaka yote minne hiyo inahesabiwa kuwa ni mwaka mmoja. Malamiko yake ni kutaka definition ya mwaka iwe wazi siyo hiyo ya kubadilikabadilika. Soma makaratasi ya kisheria ambayo nimekuwekea siyo hayo maneno ya Yahoo ambako mtu yeyote anaweza kuandika. Kwanza kesi yenyewe hata haijaamuliwa bado iko mahakamani halafu wewe unakurupuka na upupu hapa kwamba ameamuliwa na new York City wakati kesi yenyewe iko California.


Hata hiyo link ulyoweka ya Yahoo nadhani uliokoteza tu bila hata kuisoma kwani haipo. Ni tabu kweli kuelimisha graduates wa shule za kata (no offense).
Mimi wakusoma shule za kata? Goddamn 😠
.
Case ya Kanye aliyoifungua yeye mwenyewe apate uhuru kutoka kwa EMI (California) under labour code 2855 which mandate kwamba mtu atakuwa na mkataba wa huduma with a maximum 7yrs akitumia kigezo cha he's aforementioned contract since 2003.
.
Unajua kwaninu case ilipohamia New york alishindwa mr broke?
.
He was in love with the yte gaze, also it explains why he released scoop diddy woop.
He got no OG contract EMI got it that why they won a case stop talking oldest shi.t's here.
.
Kanye has it forever
 
Tatizo lipo wapi.
Music ni biashara kila mtu analenga faida
Kwani harmonize alijua kama angefik hapo alipofika leo..??
Kwan wcb kipnd wanainvest kwa harmo waliona angefika hapo ...??
Msanii gani wa wcb amepewa promo kuliko harmo..??

Na harmo alipewa promo ili mond awaprove watu wote wrong kwamba anaweza mtengeneza mtu akawa mkubwa.

Tatizo harmo anajiona big kwasababu ni mwaka sasa mond alikua hajatoa nyimbo
Mond akawa anadeal na media
Tobo kwa harmo likaonekana
Akapita
Alaf pia wale mashabik wa kiba ndo wanaosupport huu ujinga
Wale wale waliomkataa kipind cha aiyola leo ndo wanaona anakandamizwa
Mkuu wale mashabiki wa kiba eti leo ndo wamekuwa mashabiki wa kundeboy. [emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] mazezeta kweli
 
Naona siku hizi baada ya kutoka kwa Mange kimambi mpo na Mwijaku.....!
Ukiambiwa Harmonize alikuwa amesainiwa kwa miaka 15 masikio yatapokea hiyo sauti lakini akili itakataa kuamini au kuelewa hicho ilichopokea toka masikioni. Yani mkataba wa kazi wenye muda wa MUONGO NA NUSU? Tungekuwa ulaya tungeuita ni "CONTRACT FROM HELL".

Tuseme alisainiwa ana miaka 20, ina maana mpaka anafikisha miaka 35 lazima awe chini yao. Hapo katikati akiwa na miaka 22 mpaka 30 ndio muda wa kupiga kazi kwa nguvu na kutengeneza future yake. Sote tunajua lifespan ya soko la muziki huwa ni ndogo, huwezi kuwika zaidi ya miaka 10. Usipotumia muda vizuri ndani ya miaka hiyo basi ishakula kwako.

Kibaya zaidi boss wao pia anafanya kazi ileile ya kuimba, na hawezi kukubali hao alowaajiri wampite. Kwa maana hiyo msanii hawezi fikia ile maximum peak yake kwa sababu yuko limited na masharti ya kutompita boss wake.

Mikataba ya namna hii ni mibovu kwa sababu inamgeuza msanii husika kuwa mwajiriwa wa lebo husika. Yani mkataba unakuwa haumruhusu kujiendeleza yeye kama yeye bali kuiendeleza lebo.

Hii inafanya kama mko wengi kwenye lebo wote mbweteke na kuondoa ushindani na ubunifu kwa sababu hata ufanye kazi kwa bidii vipi mafanikio yote inabeba lebo wewe unabaki ni ile % mloandikiana tuu.

Pia hii inaleta mgongano wa kimaslahi kwenye lebo kwa sababu anayefanikiwa ataona kama wenzie wanamnyonya jasho lake.

Ndani ya WCB bosi mmojawapo ambaye ni Diamond Platnumz pia ni msanii. Kwa hiyo kusainiwa pale ni kama mchezaji kucheza na kocha wake uwanjani na wote wanataka kila mmoja afunge. Yani ni sawa na wewe uajiriwe kwenye kampuni halafu baadae ufungue kampuni kama ile uloajiriwa. Lazima mchukiane na boss kwani hatopenda kupitwa hasa akigundua unampiku mbinu za kibiashara.
Ndio maana vijana wa WCB wamepigwa pini hakuna kumpita boss wao DP.


Katika dunia ya sasa ni ujinga wa hali ya juu kusaini wasanii kwa kufuata mfumo wa miaka. Wenzetu waliondelea wanamanage kazi za wasanii hawamanage wasanii. Yani the more unavyopiga kazi kubwa na kutoa kazi kali kali ndio unajikuza wewe sio lebo yako.

Sasa hapa bongo eti unawasaini wasanii na kuwalipa mshahara kwa mwezi, unawatafutia na nyumba za kupanga na ki-premio cha 10M ili kuwazuga.

Ndio maana kazi za WCB zikitoka wanaipigia promo weeeeh, mpaka kwa kutumia kiki za ajabu ajabu zinazokinzana na maadili yetu ili tuu kuipa nguvu kazi yao. Lakini unakuta hiyo kazi haivuki hata mpaka wa Namanga pale.

Ndio maana tumeshuhudia hata Diamond mwenyewe akiporomoka kwenye soko la muziki Afrika. Hapati nominations tena kwenye tuzo mbalimbali sababu hakuna kipya alichonacho kulinganisha na mwanzo alivyokuwa anafanya kazi kwa kujituma.

Yani mikataba ya lebo za muziki tanzania haina tofauti na ule mkataba wa bandari ya bagamoyo. Kwa hali hii sijui sekta gani itapiga hatua kwa haraka Tanzania kama urasimu wa mikataba umekamata sekta zote[emoji24][emoji24][emoji24]


View attachment 1190044
 
Mkuu hao wanamsikiliza Mwijaku unategemea yule jamaa ataongea zuri kutoka dabuliusibii?
Nakala ya mkataba ipo wapi au hisia?

Drake yupo YCMB zaidi ya miaka 10 ,Kanye West yupo chini ya Roc Nation ya Jay Z zaidi ya miaka 10,Emininem yupo chini ya label ya Dr Dree zaidi ya miaka 20 kwa hiyo mimi sioni ajabu.

Mimi naona swala la Harmonize,tuliache muda utaongea ,maanake hizi nyingine ni Chai tu.
 
Ukiambiwa Harmonize alikuwa amesainiwa kwa miaka 15 masikio yatapokea hiyo sauti lakini akili itakataa kuamini au kuelewa hicho ilichopokea toka masikioni. Yani mkataba wa kazi wenye muda wa MUONGO NA NUSU? Tungekuwa ulaya tungeuita ni "CONTRACT FROM HELL".

Tuseme alisainiwa ana miaka 20, ina maana mpaka anafikisha miaka 35 lazima awe chini yao. Hapo katikati akiwa na miaka 22 mpaka 30 ndio muda wa kupiga kazi kwa nguvu na kutengeneza future yake. Sote tunajua lifespan ya soko la muziki huwa ni ndogo, huwezi kuwika zaidi ya miaka 10. Usipotumia muda vizuri ndani ya miaka hiyo basi ishakula kwako.

Kibaya zaidi boss wao pia anafanya kazi ileile ya kuimba, na hawezi kukubali hao alowaajiri wampite. Kwa maana hiyo msanii hawezi fikia ile maximum peak yake kwa sababu yuko limited na masharti ya kutompita boss wake.

Mikataba ya namna hii ni mibovu kwa sababu inamgeuza msanii husika kuwa mwajiriwa wa lebo husika. Yani mkataba unakuwa haumruhusu kujiendeleza yeye kama yeye bali kuiendeleza lebo.

Hii inafanya kama mko wengi kwenye lebo wote mbweteke na kuondoa ushindani na ubunifu kwa sababu hata ufanye kazi kwa bidii vipi mafanikio yote inabeba lebo wewe unabaki ni ile % mloandikiana tuu.

Pia hii inaleta mgongano wa kimaslahi kwenye lebo kwa sababu anayefanikiwa ataona kama wenzie wanamnyonya jasho lake.

Ndani ya WCB bosi mmojawapo ambaye ni Diamond Platnumz pia ni msanii. Kwa hiyo kusainiwa pale ni kama mchezaji kucheza na kocha wake uwanjani na wote wanataka kila mmoja afunge. Yani ni sawa na wewe uajiriwe kwenye kampuni halafu baadae ufungue kampuni kama ile uloajiriwa. Lazima mchukiane na boss kwani hatopenda kupitwa hasa akigundua unampiku mbinu za kibiashara.
Ndio maana vijana wa WCB wamepigwa pini hakuna kumpita boss wao DP.


Katika dunia ya sasa ni ujinga wa hali ya juu kusaini wasanii kwa kufuata mfumo wa miaka. Wenzetu waliondelea wanamanage kazi za wasanii hawamanage wasanii. Yani the more unavyopiga kazi kubwa na kutoa kazi kali kali ndio unajikuza wewe sio lebo yako.

Sasa hapa bongo eti unawasaini wasanii na kuwalipa mshahara kwa mwezi, unawatafutia na nyumba za kupanga na ki-premio cha 10M ili kuwazuga.

Ndio maana kazi za WCB zikitoka wanaipigia promo weeeeh, mpaka kwa kutumia kiki za ajabu ajabu zinazokinzana na maadili yetu ili tuu kuipa nguvu kazi yao. Lakini unakuta hiyo kazi haivuki hata mpaka wa Namanga pale.

Ndio maana tumeshuhudia hata Diamond mwenyewe akiporomoka kwenye soko la muziki Afrika. Hapati nominations tena kwenye tuzo mbalimbali sababu hakuna kipya alichonacho kulinganisha na mwanzo alivyokuwa anafanya kazi kwa kujituma.

Yani mikataba ya lebo za muziki tanzania haina tofauti na ule mkataba wa bandari ya bagamoyo. Kwa hali hii sijui sekta gani itapiga hatua kwa haraka Tanzania kama urasimu wa mikataba umekamata sekta zote[emoji24][emoji24][emoji24]


View attachment 1190044
Nominations amepata kama zote eboooooh gubu litakuuua shubamit!!!
 
Mimi wakusoma shule za kata? Goddamn 😠
.
Case ya Kanye aliyoifungua yeye mwenyewe apate uhuru kutoka kwa EMI (California) under labour code 2855 which mandate kwamba mtu atakuwa na mkataba wa huduma with a maximum 7yrs akitumia kigezo cha he's aforementioned contract since 2003.
.
Unajua kwaninu case ilipohamia New york alishindwa mr broke?
.
He was in love with the yte gaze, also it explains why he released scoop diddy woop.
He got no OG contract EMI got it that why they won a case stop talking oldest shi.t's here.
.
Kanye has it forever
Sijui wewe unapata wapi habari zako; unaandika pumba kweli na tena hujui unaloandika. Kesi zenyewe hazijaamuliwa bado ziko mahakamani halafu wewe unakurupuka eti alishindwa New York. Leta basi hiyo hukumu ya New York utuonyeshe hapa.

Malamiko ya EMI dhidi ya Kanye hapo US District Court Southern New York ni haya.

Kesi zilizokwisha tolewa hukumu na mahakama hiyo ni hizi hapa

Sasa wewe umetoa wapi hukumu yako kama siyo mambo ya kijiweni kutoka shule za kata
 

Attachments

Mkuu acha kupambna na mapoyoyo.

Nguvu zako bora uzitumie kwenye vitu vya msingi.
Sijui wewe unapata wapi habari zako; unaandika pumba kweli. Kesi zenyewe hazijaamuliwa bado ziko mahakamani halafu wewe unakurupuka eti alishindwa New York. Leta basi hiyo hukumu ya New York utuonyeshe hapa.

Malamaiko ya EMI dhidi ya Kanye hapo US District Court Southern New York ni haya.

Kesi zilizokisha htolewa hukumu ni hizi hapa

Wewe umetoa wapi hukumu yako kama siyo mambo ya kijiweni kutoka Shule za Kata
 
Back
Top Bottom