WCB walipwa bilioni 2 na Universal music, TRA walamba mil 35

Duuuuu..guitar???


Man usicheze na TRA hata ukimuagizia mtu simu ya mkononi tu kupitia posta kama inatoka nje ya nchi basi ujue hiyo kodi yake itakuwa kainunua Mara mbili.
 
baba J atamwambia leta hizo hela tukakarabati mamiradi ya serikali
 
mkuu ni kodi nzima ya wcb kama kampunisio kwa huo mkataba

Mkuu asante ingawa bado sijaelewa vizuri. Kampuni huwa wanapaswa kulipa asilimia ngapi kwani ukilinganisha na mtu binafsi
 
me nisingekubali mil 35! kwa hali hii! kha! naanzajeanzaje lbd😀
hata mimi kwakweli nisingekubali...
huo ninuonevu
hio mil35 bora wangesema nifanye jambo lolote la maana kwakweli... kodi hio vipi?
 
Mkuu asante ingawa bado sijaelewa vizuri. Kampuni huwa wanapaswa kulipa asilimia ngapi kwani ukilinganisha na mtu binafsi
Mkuu asante ingawa bado sijaelewa vizuri. Kampuni huwa wanapaswa kulipa asilimia ngapi kwani ukilinganisha na mtu binafsi
ambacho nafahamu tra huwa wanaangalia biashara yako,kama kunauwezekano wa kuingiza kiasi gani?
baada hapo ndio wanakukadiria kodi yao
 
Swala la kodi halikwepeki, siku ukiingia kwenye reli ya TRA huna ujanja lazima ulipe. Kuna siku niliingiza guitar jipya kutoka Sweden nikapigiwa mahesabu nikaambiwa nililipie laki nne mi mwenyewe nilichoka.
kumbe ww ni bongo flavour
 
Yale yale
Mwenzao alisign na sony wakamdhihaki leo wao wameangukia kule kule
Kuna tofauti kubwa sana tu!Wanamuziki wengi wajanja huwa huwa hawataki kusaini label wao kama wao ili hatimae kila kitu kisimamiwe na label owner (sawa na mkataba wa Kiba + Sony) bali huwa wanaingia mkataba wa kusambaziwa kazi zao au mkataba kati ya label (kubwa) na label ndogo ya msanii husika! Na ndio maana hata ukiangalia Sony, kuna utitiri wa labels ambazo wameingia nazo mkataba... kwa sababu msanii husika hakutaka individual contract ambayo ni full unyonyaji!!
 
ambacho nafahamu tra huwa wanaangalia biashara yako,kama kunauwezekano wa kuingiza kiasi gani?
baada hapo ndio wanakukadiria kodi yao
Asante mkuu, mimi nilijua ipo fixed rate. Basi sawa.
 
billioni2 kodi iwe millioni35
tibaijuka alipokea bilioni1.2 ya escrow akaombwa kodi mil200..!!
 
Formula gani wametumia hiyo?
Billion 2 ulipe kodi 35M?

Siyo chini ya milioni miangapi hivi!!
Huenda kama nalo ni dili la TRA.
 
Ni malipo ya aina gani hayo 2bn unalipa 35m tax? VAT?
Shangaa wewe... VAT ni 18%, Income Tax 30%.. Sasa 2 billion kulipa 35 M yaani sawa na 2% ya alichoingiza sijui ni TRA ya wapi wamefanya huo upumbavu
 
Hehehehehe vilaz.a wao hawahoji wanarusha mikono na kushangilia..

It is either hajalipwa hiyo 2 Billion au yeye kodi amelipa zaidi ya 35 Million..
 
Hii habari imekaa kijanja janja mno ukiuliza ili upate majibu sahihi na uelewe kiundani utaitwa hater.

Ila poa kwa hiyo hizo milioni 35 halizolipa kodi ndio 18% za bilioni 2?!
 
ambacho nafahamu tra huwa wanaangalia biashara yako,kama kunauwezekano wa kuingiza kiasi gani?
baada hapo ndio wanakukadiria kodi yao
Kama unafanya biashara yenye turnover ya 20+ Million lazima uandae vitabu vya mahesabu na vikaguliwe na auditors. Hao wasafi wanafanya biashara mbalimbali, ni kampuni.. Na kama wamelipwa 2 Billion hapo lazima 18% iende TRA ambayo ni Millioni 360.. Sasa million 35 ndio tunashangaa hapo muamala umefanyikaje
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…