We mwanaume usikubali kufilisika kwa ajili ya mke na watoto (family) utakufa na kinyongo

We mwanaume usikubali kufilisika kwa ajili ya mke na watoto (family) utakufa na kinyongo

Ni kweli lakini ndoa isiwe adhabu kwa mwanaume fanya kwa kujua kuna maisha nje ya familia yako baada ya kustaafu.......samahani mkuu sitaki unichukulie kua personala nikuulize swali marehemu baba ako alifariki kwa umri gani?
50 mkuu
 
Mada imewekwa mezan huru kwa yeyote kutoa maoni acha kujipendekeza kwake. Hujajiuliza kwanini yeye kakaa kimya ila wewe unarukaruka kama maharage jikon
Ni kama wewe ulivonipa haya maoni🤣🤣,Hongera sana
 
Mimi nakubaliana na wewe 100% ila sio kumpeleka mtoto kusoma ST ksyumba kule ni mauuwaji ya kimbali tu hamna elimu kati ya wanafunzi 100 walio maliza darasa la saba kijijini kwetu 40 wameolewa early marriage 15 bodaboda 30% wakulima 5. ndo wameenda sekondari, wengine ni vibarua mjini kuna shule za English mediam zina ada nafuu kati ya 150k kwa 300k day kwanini nisimpeleko huku ni mpeleke ya 2m?
Your to general without specific details, taja hizo shule za ada ya laki na hamsini hadi laki tatu kwanza.
 
Mimi nakubaliana na wewe 100% ila sio kumpeleka mtoto kusoma ST ksyumba kule ni mauuwaji ya kimbali tu hamna elimu kati ya wanafunzi 100 walio maliza darasa la saba kijijini kwetu 40 wameolewa early marriage 15 bodaboda 30% wakulima 5. ndo wameenda sekondari, wengine ni vibarua mjini kuna shule za English mediam zina ada nafuu kati ya 150k kwa 300k day kwanini nisimpeleko huku ni mpeleke ya 2m?
Your to general without specific details, taja hizo shule za ada ya laki na hamsini hadi laki tatu kwanza.
 
C unaona alikufa mapema kwasbb alibeba majukumu mengi kuwakuza hakjiachia akiba.
Watu wanakufa at 40 wakiwa wameachiwa urithi wa mamilioni na baba zao waliokufa at 80. Binafsi naona kila mtu afanye analoona linafaa akiwa hai, anayeona bora afe na kiatu kimoja kuliko kuona familia yake ikikosa na afanye, anayeoona bora ajiwekee fedha watoto wasome kayumba afanye, anayeona vyovyote afanye. Wanajeshi wanakufa at 30 huko mipakani wakilinda raia wasio ndugu zao kwa jina la nchi ishindikane mwanaume kufa masikini sababu ya watoto wake? Dunia ina watu wenye mitazamo ya kipekee sana linapokuja suala la ni nini kipaumbele chake.
 
Watu wanakufa at 40 wakiwa wameachiwa urithi wa mamilioni na baba zao waliokufa at 80. Binafsi naona kila mtu afanye analoona linafaa akiwa hai, anayeona bora afe na kiatu kimoja kuliko kuona familia yake ikikosa na afanye, anayeoona bora ajiwekee fedha watoto wasome kayumba afanye, anayeona vyovyote afanye. Wanajeshi wanakufa at 30 huko mipakani wakilinda raia wasio ndugu zao kwa jina la nchi ishindikane mwanaume kufa masikini sababu ya watoto wake? Dunia ina watu wenye mitazamo ya kipekee sana linapokuja suala la ni nini kipaumbele chake.
Mkuu ni kweli ila usijiumize maisha yako kisa unataka mkeo na watoto wako waishe maisha ya high class, suala la kufa ni jingine na suala la kuishi kwa maumivi ni jingine, usijasahau mkuuu hata kama unapenda familia yako.
 
Your to general without specific details, taja hizo shule za ada ya laki na hamsini hadi laki tatu kwanza.
Mkuu hizo shule zipo nyingi ila wengi hutafuta majina makibwa na magari ya shule, just showoff kwanini mtoto aende shule ya mbali wakati kuna shule jirani.
 
Mkuu ni kweli ila usijiumize maisha yako kisa unataka mke wo na watoto wako wsishe maisha ya high class, suala la kufa nijingine na suala la kuishi kwa maumivi ni jingine, usijasahau mkuuu hata kama unapenda familia yako.
Nakuelewa boss ila unajua mkuu binadamu ni kiumbe cha pekee linapokuja suala la mapenzi na vipaumbele esp pesa zinapokuwa hazitoshi, kwa wale wenye pesa hakuna tatizo sababu zipo. Ni kwamba binadamu ambaye pesa hazitoshi atateseka na kile anachokipenda, hapa tunapojadili usishangae kuna mtu kichwa kinamuuma ila haendi hosp kufanya checkup lakini anahangaika na kumlipa fundi juma atengeneze nissan xtrail yake isiyopona. Binafsi naona linapokuja suala la mapenzi ni kupoteza muda kumshauri mtu asiwekeze kwenye anachokipenda sababu atawekeza huko mahaba yake yalipo. Suluhisho ni kuwa na pesa ufanye yote, yale unayoyapenda yasiyo ya lazima na yale ya lazima kama akiba ya uzeeni n.k
 
Nakuelewa boss ila unajua mkuu binadamu ni kiumbe cha pekee linapokuja suala la mapenzi na vipaumbele esp pesa zinapokuwa hazitoshi, kwa wale wenye pesa hakuna tatizo sababu zipo. Ni kwamba binadamu ambaye pesa hazitoshi atateseka na kile anachokipenda, hapa tunapojadili usishangae kuna mtu kichwa kinamuuma ila haendi hosp kufanya checkup lakini anahangaika na kumlipa fundi juma atengeneze nissan xtrail yake isiyopona. Binafsi naona linapokuja suala la mapenzi ni kupoteza muda kumshauri mtu asiwekeze kwenye anachokipenda sababu atawekeza huko mahaba yake yalipo. Suluhisho ni kuwa na pesa ufanye yote, yale unayoyapenda yasiyo ya lazima na yale ya lazima kama akiba ya uzeeni n.k
........" usishangae kuna mtu kichwa kinamuuma ila haendi hosp kufanya checkup lakini anahangaika na kumlipa fundi juma atengeneze nissan xtrail yake isiyopona".......[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Kweli mapenzi ya kitu ukichanganya na ignorance ni hatari, hao watu wapo kweli.
 
Ndoa haina shida. Shida ni wanawake wa kisasa waliokosa mafunzo nyeti ya utumishi wa ndoa na kuitunza. Wanawake wa sasa ni material oriented na bila mali wanaona ndoa ni adhabu na mzigo kwao sababu wanazingatia maokoto.

Wanaume kwa muda mrefu wamechagua wao kwa hiyari yao kuwa ng'ombe wa kafara na matokeo yake ni kufa na kuteketea kama karatasi juu ya moto.

Watoto wa kiume hawaoni maisha nje ya mahusiano na mwanamke/ndoa/uchumba/mahusiano. Kijana wa wastani mpatie milioni 10 kama zawadi bila masharti yoyote ya namna ataitumia. Baada ya muda utagundua ameiwekeza kwenye mahusiano na mwanamke kwa namna ambayo hiyo pesa haitarudi hata mia. Mpe mtoto wa kike hata million 100, atatumia kidogo sana kwenye mahusiano na ataidai irudi kama sehemu ya uwekezaji wa kibiashara na sio upendo kama wa mwanaume.

Hii ni matokeo ya msisitIzo wa muda mrefu na upotoshaji ambao jamii imekuwa ikiubeba vichwani na kurithisha vijana na mabinti kuamini mwanaume pekee ndie anatakakiwa kurisk na kutoa vyake hadi senti ya mwisho hata kama hana. Asipofanya hivyo basi sio mwanaume kamili matokeo yake vijana wa kisasa wanaendesha maisha yao na huu upuuzi vichwani. Mtu hana hela anafosi kuazima gari aonekane yupo vema, anakutana na binti anabidi kupretend kuishi kwa madeni ili kumfurahisha mtu ambaye lolote likimkuta hatoweza endelea nae.

Mapenzi/ndoa/uchumba ni investment kama zinginezo tu,unachowekeza kinatakiwa kuzalishwa na kukua na kuletea mafanikio kwako kama kiongozi na sio kuburutwa na mtu kihisia.
Vijana wabadili priority. Hili pori /msitu wa miaka 20 hadi 50 unatakiwa kuendesha kwa mipango yako binafsi na kwa kujiamini,ndivyo ilivyokuwa miaka ya uanaume ambapo wanaume walikuwa na kidali cha maamuzi na sio wasasa kazi kulia lia na kuomba kuonewa huruma na wanawake ambao kwanza hawajajitunza,miili ni used,hawana bikra,adabu zero,hawatambui mamlaka ya kiume kwenye maisha yao,viburi, ujuaji, wafujaji wa pesa na mali za mwanaume wake,hawana huruma,nyumba za ibada wanakwenda kuzuga tu ila hawamtambui MUNGU kwa namna yoyote, hawa sio sampuli ya kukufanya ukose muelekeo.

Ule wakati unahisi kuchanganyikiwa,hofu,upweke,wasi wasi, na kukosa uelekeo wa maisha ndio tafsiri halisi ya kusimama mwenyewe,yaani ndio muda vijana wengi hukimbilia mapenzi kama sababu ya kuishi (purpose) na kuzika akili,mali,fikra,vipaji walivyopewa na MUNGU na kila kitu huko matokeo yake ni mwisho wao hutokea mara tu uzee ukiwafika.

Vijana wengi wanaamini wakishaoa then kilichobakia ni kuzeeka na kusubiria kuitwa babu na wajukuu kumbe muda huo mwanamke anapanga mawili ni aidha ufe umuachie kila kitu, hutaki then ufyate yeye ashike hatamu na rasilimali zote wakiwamo watoto. Matokeo yake mwanaume anakuwa kama ng'ombe tu,kuzunguka zunguka bila plan hatimae magonjwa ya utu uzima yanamuwahi sababu ya kukosa utulivu wa mwili na akili.

Rekebisheni hii life style vijana. Ukiwa umri huo wa miaka 15 ingia YouTube na kwenye website jifunze namna ya kufanys biashara na kuhifadhi pesa zako. Mwanamke akija muonyeshe hela zako ila akizitaka then yupo entitled kushare na wewe 10% ya pesa tena mnatumia nyote. Akija usimkubali akileta uvivu bali kaa nae kimkakati yaani awe investment kwako kama Msaidizi.

Akikushauri pokea ila usimuachie awe na final say. Ni heri kuanzisha jambo kwa fikra zako na likafeli kuliko kupokea ushauri wa mwanamke halafu jambo likafanikiwa,utafurahia mwanzoni na mtasheherekea subiria huko mbeleni kitakachokutokea hadi utatamani urudishe siku nyuma umwambie mama ,naomba ushauri wako kaa nao ni mzuri ila wacha tufanye hili langu,likifeli hasara ni yangu. Hayati Reginald Mengi na matajiri wa Marekani Jeff Bezos na Bill gates wamepitia hii kitu na wamejifunza kwa gharama kubwa sana.
 
Mwanaume kama wewe ni husband material tunza akiba tunza akiba!! yako dont restrain all your resource kwa ajili ya kusomesha watoto wako kwenye shule za ada ya juu au ufurahisha mke kwa kumpa 100k za saluni kila wiki au kumpeleka holidays kila wikend.

Jitahidi kua modorate katika bajeti zako kuna maisha itakao kua yako peke yako yanao kusubilia hamna atakae kuepo kwa ajiri yako, au watu sio marafiki wako wa kudumu.

Jitahidi almauti akukute usiwe frusrated man. Utujakata hiyo familia yako unaipenda mpaka unakopa benki au Vicoba kumudu na kilipa ada za English medium wana kupenda ila swali lina bakia kwamba for how long watakua na wewe?

Husband material wengi elites wamekufa mapema miaka 55 hadi 65yrs wakati sio wa kulima wameishi mjini kwa mtu wa mjini hicho ni kifo cha mapema, kwasababu wanawekeza sanaa kwa watu wanao kua na maisha yao badaye na wana staafu bila kitu hence frusrated men thus early death.
Akiba ni muhimu uzeeni ndio ya kiinua mgongo.
 
........" usishangae kuna mtu kichwa kinamuuma ila haendi hosp kufanya checkup lakini anahangaika na kumlipa fundi juma atengeneze nissan xtrail yake isiyopona".......[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Kweli mapenzi ya kitu ukichanganya na ignorance ni hatari, hao watu wapo kweli.
Hahaha, kabisa mkuu.
 
Back
Top Bottom