Vice versa can also be true!
Nikiwa nimepata taarifa za mimba nikafurahi sanaa, sio kujifanya nimefurahiii kuzuga, No ndugu msomaji nilifurahi toka moyoni. Ikumbukwe kwa wife nina watoto wa 2 wa kike na wa kiume, so kusema labda nina hamu ya mtoto wa jinsia flani ni uongo kwa kweli sababu Mungu wetu ni wa rehema na kanipa mimi watoto wa jinsia zote.
Nilifurahia sababu kubwa moja tu, kujua kweli Mercy ananipendaaa sanaa. Maana mtu alikuwa na mchumba na kashatolewa mahari kabisaaa, inasubiriwa ndoa tu, she let that go kiroho safiii tu, kwa moyo mmoja kunizalia mimi Man of the people wenu ambae sina future nae yoyote na option ya kumuacha mke wangu na wanangu haikuwepo kabisaaa katika mahusiano yetu.
Kipindi chote cha kuchepuka alikuwa muelewa, hata siku moja hukuti akipiga simu usiku, au weekend nikimwambia leo bwana kuna ratiba na mwenzio. Anakuwa mwelewa mpaka niamue kumtafuta mie. Hana wivuuu au maneno ya kukeraaa oooh mkeo anafaidi sijui mkeo hivi, au mkeo vileee walaaaa.
Sasa kunizalia it took mye heart to all new level of respect, love and appreciation. Mke wangu kazaa cause namlea hapa mjini yeye na familia yake, kila siku nijue wamekula nini, wamekunya nini, na hafanyi kazi yoyote, hawazi kutaliwa nini, kodi za nyumba mjini za shida, gari yake mafuta itakuwa vipi, magari dukani bei gani hawaziii kabisaa. Na nilimuoa mdogo so hakupitia chujiooo la maisha ya mjini akapanga chumba, akajua kodi zinasumbua kichwa, magari hatolewi bure ukilegea unaweza kufa hujaendesha, chakula ni gharama kubwaaa, hajajua lolote so kunizalia yeye ni halali kabisaaa tena halali kabisaaa, anaishi sehemu nzuri, anakula vizuriii, ana drive kwanini sasa asizae.
Ila Mercy kwanza mwenyewe boss tu ana kitengo chake, simpi chochote cha maana, sijui kodi analipaje na namkaza huko ndani kwake mpaka basi. Sijui anakula nini, wala mafuta anawekaje yaaani sijui chochoooote. Hakuna ahadi ya future wala nini. Kamuacha aliemuahidi jua na mwezi kaja kunizalia mimi mentally. Ama kweli zali la mentaliiiiiii. Yaani sijui nisemaje i started seeing her ina new light.
Nikabadilika kabisaaa, nampeleka clinic, ndio nampeleka najua mijicho inawatoka mume wa mtu kumpeleka mchepuko clinic. Mke wangu hana makuu, alijifungulia Aghakan tu. Mercy mtoto wa mjini ooh namtaka Dr. Anna Ponna wa regency, namwambia tawire mamaaa, nampeleka clinic zote. Atleast japo hapati privillage kubwa za kuwa mke, kupata my last name, maybe mtoto ila yeye hapana, apate japo za clinic. Maana nikawaza nilivokuwa naenda na wife, kila mtu na Mr. wake sasa yeye itakuwaje.
Doubts i had many, kwamba huenda mimba si yangu ya yule BF wake, au ya jitu lingine tu nisilolijuaa, it was too good to be true, yaani anizalie tu mimi mme wa mtu, simpi chochote cha maana. Nikawa nasikilizia upepo tu. Ila sikumuonesha kama na doubt but in reality, i had many doubts.
Na amakweli kila mtoto anakuja na riziki yake, hii mimba nikapata kazi moja babuuuu kubwa East Africa Community, base station Nairobi. Ikawa rahisi sasa, naweza kukaa na Mercy hata wiki nzima ila wife asijue chochote. Sasa kuishi nae nyumba moja ile wiki nzima hata 2, nabana hapa hapa Dar an wife yuko hapa hapa na dar na hatuonani ndo ujue Dar kubwaaa sanaa hiii. Kuishi nae muda wote pamoja ndo nikazidii kumpendaaa.
Nikaacha uhuni nikaanza sasa kumuhudumia mama kijacho wangu. Ikumbukwe watu michepuko inawagharimu ma million, wanalipia makodi, mafuta, bili, mimi kitongaaaa tu mda woteee. Na wanacho kihudumia hakionekaniii. Wanawake wa wasiwasi hawana hata viwango, mimi nina mwanamke wa maana, head wa unit bank, na namla bureee tu, navojisikia navotakaaa.
Anajua kujali nyieeee, siku ya birthday yangu alifunga safari kwa gharama zake kuja Nairobiii. Akanipeleka dinner hotel ya kitalii kwa gharama zake na tumbo lake kubwaa, nili enjoy sanaaa, haramu tamu sanaa na vya kuiba vinanoga hatariii. Tuka spend the weekend together huko Nairobi. Utatujuaaaa sasa kama wachepukajiii.
Baada ya ile trip i seriously started to reconsider i seriously am letting the chance of spending the rest of my life na huyu mwanamke pass. Its just a matter of time before hajatokea mtu serious wa kumuoa na kufanya nae maisha mengine, na je ikitokea hivo mimi nabakije sasa without her.
Nikiwaza divorcing my wife, na alivojibweteka nawaza ataishijeeee? Aatakula nini, atavaa nini, atalala wapi? Na nimeshamzalisha watoto a 2 tayari, wanangu wataishije, watajua baba yao kaenda wapi? Na kwanini? Na kwanini alimuacha mama yao. Na kikubwa what about the eternity i promised and guaranteed her, can i just take that promise back easily like that. Na isitoshe i have wated best years of her life kumuweka ndani then now, amezaa, amezeeka amechoka i just get to let her out of the wild. Maybe nisingemuoa kwa kumuweka ndani angepata mtu mwingine ukute wa maana zaidi yangu. I blocked that chance for her. Nikawa cross roads.
Mecry akaenda kwao kujifngua, i wished, i wanted kwnda hospital kumuona Mercy na mwanangu, lakini naenda kama nani? Maana pale kuna wazazi wake,kuna ndugu zake, jamaa zake, atanitambulisha kama nani? Na niwadanganye ukoo mzima i am single wakati ni mtu mwenye mke na watoto wa 2. Akaniambia njoo njoo mi nikajikaza sikwenda, mpaka alivorudi kwake ndo nikaja.
Kjikosha akakuta nimenunua Nursery nzima, Mercy ungemwambia at that time, mimi ni mwanaume nisie bahili, natunza familia vizuri sanaaa asingekuamini kutokana na mfumo niliokuwa nampeleka. I guess alijua mimi ni wale wanaume wasiojulikana pesa yao inapokwendaaaa. Na akaridhikaaa kabisaaa. My daughter i was gonna take care of her no matter what. Alipokuja akasema sikwenda kumuona hospital cause yeye sio mke wangu.
Waru wakaanza uchawiii na wangu kumuuliza Mercy kama tumezaa so what next? Watu kwa kuwangaaa inawahusu nini? Mercy akawa sijui anawajibu nini maana mpaka mda huo msimamo uko pale pale, mimi mume wa mtu na kanizalia kwa mapenzi yake tu.
Upendo ndo ukazidi sasa, baada ya kuanza kumuhudumiaa. Usidanganyike mwanamke sijui ana pesa zake hapendi kuhudumiwaaa sio kweli kabisaaa. Wanapenda kuhudumiwaaa mpaka basi. Na mwanamke ukumuhudumia unammaliza hata kama ana uwezo kukuzidi hizo hizo ndogo za kwako anazitolea mate. Na dahivi nilikuwa nalipwa pesa ndefu sanaaa so sikuona shidaa, kumfanyia upgrade kidogooo.
Nikambadilishia kwanza gariiii. Nilichanikaaaaaaaaaaaaaaaa! Oooooohhhh! Nilikopa bank, kuubadilishia mchepuko gari acheni tu. Na gari alikuwa anaitumia haikuwa ya bei poa ndo kichoniongezaaa msambaaa. I just wanted to give her something big for once, kanizalia mtoto mzuriii, yes i couldnt give her my last name but i can buy her a more expensive car, and womwn always like more expensive anything all the time. Just to show my love kwa matendo sio maneno tu.
Huku mke wangu akazidi kuni pressure swala la kufunga ndoaaa. Hasikii nini wala nini anachotaka yeye ni ndoa tu. Like with everything nilikuwa bado siajmuoaa. Last name yangu anaitumiaaa anavotakaa na bado anadai ndoa. Face book yoote, instaaa kote, whatsup dp nimejaa mimi na watoto wetu ila bado roho yake haijaridhikaa kabisaa bila karatasi la ndoa. I never knew a piece of paper was worth that much especially ilioandikwa na binadamu kama sisi.
Tukaenda mtindo huu wa ndumila kuwili for 2 good years. Mercy akaanza malalamiko, the clock is ticking, nampotezea mda, yeye she has given so much kwenye hii relationship ila its about time she should be thinking about her future alone. Jamaniiiiii! Wanawakeeee! Mi nikakaa tu kimya sasa ningesemaje. Nikawa nazugaaa zuga mtu mzimaaa nauchunaaa. Akaiongea hio kauli several times. Ila mapenzi kama kawaidaaaa ananipenda kufaaaa. Na mimi nampendaaa.
Mke wangu nae anakomaa naataka ndoaaa. Nikaamuanza mbali sanaaa mke wangu, mbali sanaaaa. Kwamba mimi navoona dini kubadilisha siweziiii, na nimeridhia kabisaa yeye atafute mume mwingine, waoanae, mi nitalea watoto na kumtunza kama kawaidaa ili apatane na Mungu wake na kupata amani ya moyo.
Tofauti na nilivotarajia fujooo la kufa mtuuu, akasema tu hata wazazi wamesema hilo mara kibao maybe ndo jambo sahihi. Atakaa na familia then watanipa jibu. Baadae akasema familia imeridhia ila matunzoooo matunzooo ndo walio sisitiza wao. Kwamba hata akama ndo imekufaaa sababu nishamzalisha matumizi kama kawaida. Moyoni nilipiga vigelele.
Kwa kuanzia nikamtafutia chuo Arusha huko, cha bei ndafu nikamlipia, na familia nikaiamishia Arusha, watoto nikawatafutia shule za bei ndefuuu, sababu sahivi na mimi si diplomatic worler ada zinakuwa covered na ofisi, ila mama yao aende chuo na kutunza familia. Kikubwa niliamsiha familia ili sinibane na Mercy hapa Dar. Mara mmenda huku maana visehemu vichahce mjini ndo vya standard, nimepeleka mwanangu an Mecry marrybrown, mara nawakuta na wale perharps wako na kibuzi tu cha mama yao, unafikiri ice cream zitashuka siku hio? Weeeeeeeeeee!
Haikuwa rahisi upande wangu na ndugu zangu waliona sina msimamooo. Kwanza nilitaka kuoa mke wa mtu ikawa aibuuu tupu, likapita, nimeoa binti mdogo nimemzalisha watoto wa 2, mara nimewatambulisha binti mwingine tena na mwanamke mwingineee. Wkawa washaniona sina msimamo ni mchafuziii tu, sijielewi. Walileta upinzani mkubwaaa sanaaa. Kikubwa mimi ndo boss wao, hawawezi kunikaziaaa sanaaa. Wakakubali tu kishingo upande.
Sikutaka kumwambia Mercy fasta fasta kwamba wife nishamtwanga talaka bubu na kumdeport cause i was not sure sitobadili mawazo na kumfata nimrudisheee. Arusha sio mbaliii mjue. Nikawa kwanza nasikilizia hii transition na yeye je ataweza ku cope bila mume kwa jinsi alivokuwa kajibwetekaaa. Nikawa nimemwambia tu watoto wako kwa mama, wife nimetafutia shule Arusha kwa hio sisi ni full kujiachia tu sasa.
Katika hio hio trasition ndo nikagunduaa makubwaaaa na mazitooo sanaaa. Lichonipataaa sitokaaa nisahau. Nikagundua MERCY WA CHEATING ON ME NA MWANAUME MWINGINE. Imagineeeeeeeeeee! Mke nishamuacha tena hadharaniii kwa familia zote kuridhiaaa, alienifanya nimuache mke, ame move on ana mwanaume mwingine. Nafanyaje hapo ndugu msomajiii?What do i do? Call my former wife, najifanya bwege na kumbembeleza Mercy au naibua chepuko jipyaaaaaaaa, kitu brand new. What do i do? Familia itanionaje kama sio sieleweki? Maana nimewaambia nataka kumoa Mercy mara brand new!!!!!!!!! Nilichokaaaaaaaa. Kuchapiwaaa kunaumaaa sanaaa given everything i have just gone through! Nimevuka Pacific ocean ili nimuoe the this?!!!!!!!!! Mazafantaaaaaaaaaaa! Nikamuuuliza akasema KWELIII NDIO.
ITAENDELEA SAA 4 USIKU.