Wema afunga ndoa bomani, amficha mume wake

Wema afunga ndoa bomani, amficha mume wake

Dotto Mnzava

R I P
Joined
Mar 6, 2014
Posts
864
Reaction score
427
Staa wa filamu za Kibongo,Wema Sepetu amekiri kufunga ndoa bomani hivi karibuni ambayo ilihudhuliwa na watu wachache. Akizungumza na Clouds FM alisema kuwa aliamua kufunga ndoa ya siri kwa kuogopa kupigwa 'juju' na mumewe angeshindwa kumuoa.

Hata hivyo alipoulizwa kuhusu tatizo lake la kutoshika mimba alisema kuwa mumewe amelikubali na hana tatizo.

==============
wema4.jpg



Staa wa filamu za Kibongo,Wema Sepetu amekiri kufunga ndoa bomani hivi karibuni ambayo ilihudhuriwa na watu watano.


Akizungumza na Soudy Brown kupitia Uheard alisema kuwa aliamua kufunga ndoa ya siri kwa kuogopa kupigwa ‘juju’ na mumewe kushindwa kumuoa.


‘’Mume wangu ni Mtanzania na siyo maarufu na ndoa yangu ilihudhuliwa na ndugu zangu wachache na ndugu wa mume wangu sikutaka watu wengi niliogopa kupigwa juju na mume wangu asingenioa,’’alisema Wema.


Alipoulizwa kuhusu tatizo lake la kutoshika mimba mumewe alilichukuaje alisema kuwa hana tatizo naye na amekubali kuishi hivyo hivyo.
Chanzo: CloudsFM
 
Ngoja warumi akuje ili tupate wasifu wa huyo mume wa Wema
 
Last edited by a moderator:
whose that mume Jamii forums intelejensia mmeshindwa kuudaka mkanda huuuuu???????
 
Hongera zao,Mungu awajalie mema katika ndoa yao. Atulizane sasa
 
Huyu binti bana, Hongera yake lakini,, Kasema Mme wake sio Mbabu wala Kijana yupo kati,, Afu sababu ya kufunga Ndoa bomani ni Dini tofauti,

Akalinde ndoa yake sasa aachane na vihoja
 
Walisema haolewiii 😁😁👏👏👏
 
Huyu binti bana, Hongera yake lakini,, Kasema Mme wake sio Mbabu wala Kijana yupo kati,, Afu sababu ya kufunga Ndoa bomani ni Dini tofauti,

Akalinde ndoa yake sasa aachane na vihoja

so inamaana wema alikataa kubadili dini
 
Back
Top Bottom