Wema Sepetu kugombea Ubunge viti maalum Singida

Hahahaha naona kichefuchefu kimetawala humu ndani. jamani mbona mmetapika hivi ndani kote hamna hata pakukanyaga?? vipi ndimu zimewatosha au niongezee na vinegar?? Maumivu yakizidi wahini hospo mpate Tiba msije faint... Matola gawa vinegar ndimu hazitoshi watu wanazidi kuzirai humu.... Mheshimiwa wema sepetu mtoto Wa marehemu balozi sepetu alikuwa na hoja.....hebu waheshimiwa tumsikilize....halooo na kale kasauti sasa!! Yes politics is politics
 
Last edited by a moderator:

Tatizo watu wepesi wa kusahau haya mambo ni kama maji yanateleza kwa mkondo, Yusuf Makamba alishawaambia msishangae watoto wa viongozi kuwa viongozi maana hata mtoto wa konda ni possibly kuwa dereva. Sasa watu wanasahau kama Muheshimiwa Wema ni mtoto wa balozi ati.
 
Last edited by a moderator:
Jamani mashabiki wa diamond mna roho za kwanini???
Wema mimi sio fan wako ila nakutakia kila la heri!!
Utakuta wengine hamna mbele wala nyuma all you do is just hate!
Wema huwa anafanya mabaya sana, sasa asijaribu kitu kingine?
Why??
Acheni uchawi...
 
Bado Shishi baby na yeye sijui anatupimo lini?CCM hoyeeee
Tetesi hata Irine Uwoya naye atatangaza nia chezea Green.
 
Ma zake,
Anafikiria nchi itachukuliwa na wale wale wanaopokea hongo ya naniii?
 
Jamani mashabiki wa diamond mna roho za kwanini???
Wema mimi sio fan wako ila nakutakia kila la heri!!
Utakuta wengine hamna mbele wala nyuma all you do is just hate!
Wema huwa anafanya mabaya sana, sasa asijaribu kitu kingine?
Why??
Acheni uchawi...

Umeongea akili kubwa humu kuna watu miaka yote watabaki kama walivyo just to hate each other wakati fursa zipo wenzao wakizichangamkia wanawabeza stupid kabisa.

Hivi tuambiane ukweli katika bunge letu hili lenye wabunge 300+ je wabunge kweli hasa wenye sifa ya kuwa wabunge wanazidi hata100? Tuwe wakweli.

Kila binadamu ana past zake kama mtu kaamuwa kujitambuwa anajaribu maisha mengine kuna ubaya gani? Mbona humu jamvini kumejaa mafairule na maloser wa kutosha tu?

Mimi namuunga mkono mtu yoyote anayejiamini anaweza na mwenye uthubutu halafu watu hawajui tu kitu kimoja huyu Wema akipata hiyo nafasi na ukichukulia alikuwa miss Tanzania mimi nawajuwa vizuri wazungu pesa zao huwa wanahitaji watu wa aina gani kufund miradi, kuna watu humu watabadili ID zao.

Wema ni maarufu kuna mabar maid wastaafu wapo mule bungeni na wameolewa na watu wazito tu na walikuwa wanatufungulia viziba bar, ila sioni mantiki kuwataja majina kwa sasa maana hata mimi wameshanipiga gape kubwa tu kimaisha na siwapati kwa lolote.
 
aliyekuwa miss Tanzania mwaka 2006 na msanii maarufu nchini tanzania ameanza kujikita katika ulingo wa siasa ambapo ameonyesha nia ya kugombea ubunge wa viti maalum katika mkoa wa singida kwa tiketi ya CCM.teamdomo this will be the hardest news to them,let us see the movie.
 
dogi masta akisikia atarukaruka kwa furaha,hata awe mbunge hawezi kufikia zari kwa kila kitu
 
Wewe pia akili zako mbona unachanganya madesa.
Tangazo la Petit man aka mbeba mikoba ya Madame kasema fomu atachukua tarehe 15/7/2015 wewe unasema ameshachukua fomu tayari.Au wewe unaukaribu zaidi na muheshimiwa mtarajiwa?:madgrin:
 
Naomba niulize, Wazanzibar wanaruhusiwa kugombea viti maalum Bara? Sina nia ya ubaguzi lakini hili sioni kama sahihi.
 
Khe! Khe! Khe! Khe! Eti nini? Tuzo ya Diamond ni maslahi ya Taifa!? Can u say that again?

Ile mihela aliyochukuwa Idrisa kwenye yale mashindano ya kifirauni wewe umekatiwa ngapi?

Usipende kupewa pesa mkononi maana pesa inaisha na utabaki huna kitu, kinachodumu ni mbinu na milango ya kupata pesa maana hiyo milango ikifunguka pesa haitakuishia, wala hiyo unayopewa mkononi haitakuwa na thamani kama sawa na milango ikifunguka. Kwa hiyo tunaposema maslahi ya taifa hatusemi maslahi ya kugawana pesa, bali maslahi ya kufungua milango ya upatikanaji pesa kwa watu wengi zaidi. Tunataka fursa na sio kupewa pesa mkononi.
 

Fursa zipi hizo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…