Huku ni kutafuta huruma tuu hakuna lingine! Mimi nasema waache waendelee kutukanwa maana ndio maaisha walio chagua ya kutukanwa.
Hivi anafikiri yeye ni star wa kike pekee hasiye na mtoto? Mbona wengine hawatukanwi? Anatakiwa kujua anaponzwa na style yake ya maisha aliyo chagua kwa hiyo kulia lia hakuto msaidia labda kubadili style ya maisha.
Kuna watu wamekuwa wakitukanwa na kudhalilishwa kwa mgogo wa kumtetea yeye na wamekuwa wakiumizwa sana..na wao pengine wana dhalilishwa kwa kuwa ni style ya maisha walio chagua hivyo hawatakiwi kulialia na kumhusisha Mungu kwa mambo yao ya kipuuzi yanayo tokana na style yao ya maisha.
Mastaa wengi wa bongo na Wema akiwemo wamegeuza mitandao ya kijamii kama nyumba zao...humo ndimo kuna sebure;chumba na bafu...hivyo kila kitu wana kifanyia kwenye mitandao ya kijamii!
Kwakuwa wameigeuza mitandao ya kijamii kama ni sehemu ya maisha yao yani hawawezi kufanya jambo bila kuhishirikisha mitandao ya kijamii..kwa hiyo wana vuna wanacho panda kila leo.
Ni ajabu sana kuona mtu anashangaa kuvuna alicho panda..wanafikiri kuwa matokeo yatakuwa matamu tuu...Haya ndio matokeo ya kugeuza mitandao kama familia yao kwa hiyo waache kulialia na kutafuta huruma kwa kupewa walicho kipanda..
Kama walio kuzunguka huwatukana wengine lazima siku na wewe utatukanwa na wengine walio wazunguka wengine..Mimi simuonei huruma hata chembe anaye vuna aliyo yapanda kila leo.
Watu wanafikiri wao pekee ndio hutukanwa kwa kuwa wao nyumba zao ndio mitandao ya kijamii..wanatakiwa kujua kuwa wanatakiwa kuwa na ngozi ngumu kama watageuza mitandao ya kijamii kama nyumba zao.
Mimi nasema wataendelea kuwatukana na kuwadhalilisha kila leo kama hamtobadilika na wala hakuna atakaye waonea huruma.