Wengi wanamkubali Bob Marley ila Mfalme wa Reggae duniani ni Lucky Dube

Jah live kaimba Lucky Dube pia Kuna beat nzuri sana
 
Dogo unataka kuchekesha walionuna??? Tafuta vitoto vyenzio visivyojua mziki ndio uviambie habary hizi za kuzimu.
 
Unajua kama unaanzisha mada kwa vitu usivyovijua, ni kama story za kuchangamsha kijiwe kwenye kahawa tu. Nakupa miaka mingine mitano fuatilia Rasta And Reggae kisha mwaka 2025 ndio uje ulete thread hapa
Jamaa umebaki mwaka aje kutuomba radhi
 
Lucky dube alikuwa vizuri kwenye aina yake ya mziki ambao yeye alituaminisha kuwa ni rege sababu aliimba na kucheza kwa kurukaruka. Ni kwaito flaan hivi yenye vibe ya rege.
Boby huyu aachwe tu Kama alivyo na sidhani Kama ni busara kulinganisha Boby na mtu mwenye viwango vya Senzo
 
Bob kwa lucky ni mchumba tu, hakuna nyimbo ya bob naipenda ila za lucky mbaya ni kidogo sana tena moja tu inaitwa drakula huwa siipendi kabisa
 
Mkuu huo ni mtazamo wako unaosukumwa na mihemko
 
Nyuzi nyingine huwa mnajiaibisha kuziposti. Kama wewe ni fan wa Lucky Dube haina shida, ni uhuru wako, lakini kumfananisha na Bob ni kuonyesha jinsi gani usivyojua muziki.

Bob Marley is a global icon. Ukiacha Tupac na Michael Jackson, hakuna mwanamuziki aliyekuwa na impact kidunia kama Bob. Unamfananisha na Dube ambaye hata Sauzi kwenyewe hana impact kihivyo? Halafu kama mtu kuuawa ndiyo sababu ya kupendwa mbona Dube ndiye aliuawa? Au hata hujui star wako alikufaje?
 
Nadhani umetoa hitimisho kwa msingi wa mtazamo/hisia zako binafsi
Ukifanya utafiti kidogo tu utangundua pengine hauko sahihi.
Unaweza ukatumia vigezo vifutavyo kufanya ulinganisho, mauzo wakati wakiwa hai yapoje, baada ya vifo vyao mauzo ya kazi zao yapoje, Ni nyimbo za nani zilipigwa zaidi na vituo vya runinga na radio wakiwa hai na baada ya kufariki.
Lingine safiri kwenye bara lolote duniani nje ya africa alafu uliza kuhusu Dube au piga nyimbo za dube utaona kama hata wanamfahamu.
Ukienda club nchi yeyote hata zile ambazo siyo anglo utangundua legacy ya Nesta ni blaaa
Nesta anaweza kuwa ndiye msanii pekee ambaye mashairi na maisha yake yameandikwa sana vitabuni na vijana wanamsoma vyuoni.

unaweza ukawa haujamtendea haki sana mzee Bob



Nyimbo
 
Yaani ni sawa kumfananisha Comrade Julius Kambarage na Bashite.
Dogo, nenda YouTube tafuta video ya Bob Marley alivyofanya balaa Harare siku ya uhuru wa Zimbabwe.
Maana ile haikuwa music concert, ile ilikuwa speech.
Labda dogo huelewi hawa watu walikuwa wanaimba nini, unasikiliza tu kama singeli.
 
Kwa Upande Wangu Lucky Dube na Peter Torshi Hawana Mpinzani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…