Wenje: Nasikitika kwa sababu Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya CHADEMA ameshindwa kusimamia maadili

Cannabis

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2014
Posts
11,557
Reaction score
33,535

Mgombea wa nafasi ya makamu mwenyekiti Ezekiah Wenje amesema anasikitishwa sana na kushindwa kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili CHADEMA (Tundu Lissu).

Amesema tokea ashike nafasi hiyo hajawahi kuitisha hata kikao kimoja cha kamati hiyo ya maadili na hivi sasa kuna watovu wa nidhamu wengi ndani ya chama. Amesema hayo asubuhi ya leo akihojiwa na Radio ya Wasafi FM.
 
kwa alivyo na mdomo vile vikao vyote vingekua vinaishia njiani tu na viongozi wengi wangekua wamejiengua chadema 🐒
 
Yeye mwenyewe lissu ni mtovu wa nidhamu!
 
Kwa hiyo Lissu ndio mwenyekiti wa kamati ya maadili?

Unaweza kuona namna gani huyu jamaa akipewa kuongoza chama atafeli vibaya.

Mbowe kachoka, lakini Lissu hafai.
 
Yaani muda mwl mzuri sana. Enzi za Dkt Magufuli tuliwaasa kuwa ndugu Lisu anatumia mabeberu kuidhoofisha nchi kwenye juhudi za kujikomboa kutoma makucha ya mikataba mibovu, yaani alishirikiana na wenzake kama akina Dkt Kafuku, Mwanyika eti kutafuta weakness ya serikali ili wazungu wajiandae kwenda kushitaki serikali, na hatimaye walipata wa kushirikiana nao toka serikalini na matokeo yake waliokuwa wanamshauri Dkt Magufuli wakafanya kwa maelekezo ya akina lisu kuvunja mikaba with loophole ambayo kweli wazungu wametuweza. Leo hii huyo huyo wakala wa wazungu na mueneza ushoga karudi tena sasa kwao eti mnalalamika hahaha tulieni dawa iwangie vizuri
 
Binafsi nashukuru hajaitisha hata kikao kimoja vinginevyo angefukuza wote ambao wangefikishwa mbele yake.
 
Magufuli kashakufa achana na habari zake. Wewe Kila siku Magufuli Magufuli.
 
Hovyoooo
 
Magufuli kashakufa achana na habari zake. Wewe Kila siku Magufuli Magufuli.
Lazima tumkumbuka tulishakula kiapo kumtetea hata kama akiwa mifupa, na itakuwa hivyo siku zote. Na kwa taarifa yako hata wewe ukiwa mzalendo hivyo hivyo tutakusema yaliyo mema hata ukifa. Dkt Magufuli tupo tuliompenda sana na hatukutaka hata vyeo na bado tunampenda na kumtetea na kumsemea yaliyo mema hata kwenye umauti wake.
 
Huyo dalali,mla ruswa na mshika mkoba wa kitoto Abdul anapata wapi moral authority ya kumkemea Lissu ?
 
Wenje wewe na mwenyekiti wako tayari Abdul amewaweka mfukoni hamtudanganyi tena mumeshakuwa mateka wa CCM. Ni kichaa tu anayeweza kuwaamini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…