Wenye LINE nyingi za simu mnakera sana..!

Chanzo huwa ni kupata huduma nafuu ndg, japo mikoani pia kuna sehemu mitandao fulani fulani haisomi.
Binafsi nina line 3, mbili voda na 1 halotel japo pia nliwahi kutumia tigo na airtel miaka ya nyuma.
Ebu fikiria mwaka 2015/2016 halotel walikuwa wanatoa extreme sh. elfu 1 unatumia data saa 24 bila kikomo, ungeacha kumiliki line yao?
Usichokijua ni kuwa hata hizi ofa za voda kuna wakati hutolewa kwa code yaani mwenye 0766... na 0764... wanakuwa na ofa tofauti, ko niteseke makusudi?
Nini cha kufanya?
Siku zote mtu mwenye line nyingi huwa kuna moja au mbili ambazo ni utambulisho wake, kwa vyovyote hazikosekani hewani, ndo uzisev hizo.
Pili, simu za kisasa unaweza kusev namba nyingi sehemu moja na kwa jina moja so changamoto yako inakuwa imetatuliwa.
Mwisho, tuvumiliane na tusilazimishe kufanana maana pia tuna vipato na hobbies tofauti.
 
Tafuta pesa mkuu.
Ukiwa na pesa watasumbuka wao kujieleza..
 
Ni umasikini tu jamani, tunatafuta unafuu. Mtuvumilie tu.
 
Umeandika excuse za kitoto sana
 
tatizo sasa hivi namba mpya wanazotoa tigo airtel na voda, hata huwezi jua ni mtandao gani.

sijui kwa nini wanashindwa ku maintain namba tatu za mwanzo.
Haswaaa.. yaani kuna namba za ajabu siku izi ikikupjgia unashindwa kuelewa hii ni namba ya nchi hii au ni ya msumbiji 😀
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…