MarkHilary
JF-Expert Member
- Feb 8, 2015
- 1,813
- 2,188
Dingi angu huwa sio mchapaji ila ana sauti kama ya radi, mweusi tii na giant kiasi. Nikikosea akipiga biti nlikua najikojolea bila kuchapwa
Akirudi home kutoka kwenye mishe zake watoto tulikuwa wapole, tunaona amani imetoweka home
Mtaani tuliheshimika na watoto korofi, tulikuwa hatuchokozwi kwa sababu watoto wa mtaa walimwogopa mzee wetu mno
Kinachonishangaza ni kwamba, mzee sio katili na sio rahisi kwake kumchapa mtoto ila sisi tulimwogopa tu
Cha kushangaza zaidi, mpaka leo sijazoeana sana na mzee wangu... Mungu ampe maisha marefu!
Hahahahhaha tulipigwa hadi tukawa sugu.hhhaha mie mwenyewe nimecheka !mie had leo na utu uzima namuogopa baba vibaya mno hakawii kunibadilikia !mie had 23 yrs nilipigwa na baba !jaman yule msukuma mkali sina hamu naye jaman ! wababa wa sasa hv zero kbs !mume wangu hajawah hata mfiya mwanaye akikosea !ananimind kweli ikikong'ota toto lake !dah km kuoigwa jaman enzi zxetu tulipigwa !
live long baba
Hahahahhaha tulipigwa hadi tukawa sugu.
haahaahahaahaa hatari sanaMjerumani ndo tulikuwa tumempa jina lake! Anakwambia sitaki kuabika mbele za maadui na mbele za shetani, kama hutaki kusali jiondoe kujiita mtoto wangu,na kama ikitokea ukaleta mimba huko chuo usinijue mimi kuwa ni baba yako! Na siku ukigonga hodi ya rikizo nahitaji mitihani yote hapa mpaka quiz,maskini unajikuta home unaingia na nguo kama tano tu za adabu ya kutosha!
My ribs jamani, nimecheka mno mpaka watu walionizunguka wakawa wananishangaaMzee alikua anasema kama unajiona upo vizuri njoo tuzipange.
Alikua hapendi mtu anyoe kipara, kaka yangu akawa mbishi siku hiyo karudi home na kipara. Mzee akamwambia kimbia ukiona upo mbali sema tayari.
Jamaa akakimbia mzee anaona mdau anasogea tu hasemi tayari, akamuungia. Dakika kadhaa mbele tunaona kaka anarudishwa kabebwa begani.
Kufika home akaambiwa tuzipange, ghafla jamaa kapiga magoti analia anaomba msamaha.
Mzee akamwambia adhabu yako utakua unapaka kiwi kichwa hadi nywele ziote.
Yaani toka jana nlikuwa staki kufungua huu uzi.....hapa nimecheka mpaka wakukuu wananshangaa.....muonekano wangu km le kibamiaazz imagine hilo chekoMshua alinichapaga viboko mbele ya demu wangu alikuja kusuka.
Dingi amekuja mchana kula chakula akakuta hakuna maji hata ya kunawa mikono, kubabake alinichapa sticki hizo.
Demu wangu alikua nje anasukwa na dada yangu, dingi ananichapia sebuleni.
Kwa kuwa nilikua sitaki demu wangu ajue kama nachapwa, nikawa najikaza sipigi kelele.
Dingi akajua viboko havini umizi, akaanza kunipiga na mavibao, kubabake nilivimbaga mikononi.
Mara Paaaap nikatoka na mindoo kwenda kuchota maji, mialama ya viboko kwenye matako, mgongoni, mikononi.
2001 hiyo Kiloleni Tabora
Hahaha basi kumbe dingi ako ukauzu wake una afadhali.hahaaaaaaa jaman nacheka had nguvu sina mie !dah !bwana we babako hatoki kanda ya ziwa kweli ! hahaha alikuja last yr kwangu may hv !akakuta watoto wakitoka shule wnaangalia cartoon kweli kweli ndo ugonjwa wao !kumbe likawa linamkaba anashindwa angalia BBC na CNN ZAKE ! bwana wee !akatuita mie na hubby akanamuambia hubby , mbiti ningemruhusu aangalie mauchafu ya kihuni haya usingefikiria kumuoa ! huu ni uhuni !zuia kbs katuni kwa watoto ! hahah nammwambia baba mbn ni nzuri zinafundisha!anakukatisha fasta !upuuzi huo mbiti nisikilize mm !
but asbh akiamka anakuambia dah wajukuu wana english nzuri endelea kwenda nao vizuri wasirud nyuma !bas na mie nampaga makavu namwambia ni cartoon hizo zinawafanya wachonge ngenga !hhahahah
Mapung'o mchezaji wa kimataifa, alinifurahisha alipojisaidia kitandani baada ya kwenda mjini kukuta choo cha self.Ndio walikua na wanaitana na kujibizana hivo, kina chepe, golden boy mapung'o, njomba nchumali
Vinginevyo mkuu ungekua unashinda mortuary kule vitongojiSiku moja mimi na dogo tulirudi saa mbili na nusu hivi na hiyo ilikuwa 1999, akatuuliza kama tumeswali swala ya ishaa, tukamwambia ndio. akatuuliza kaswalisha nani na amesoma sura gani?? kudaadeki akatubana. aiseee tulikula kichapo mpaka leo sikisahau, alitufunga kamba za katani na kututandika nyaya za umeme ajabu, kipindi hicho tunaishi Pemba kwenye nyumba za serikali na ni ghorofani sasa, kutoka mbio tulishindwa halafu alivyokuwa mkaksi, alimfungia bi mother mlango kwa nje kwanza ili asije kuamua ugovi. Siisahau iile siku, but we a re who we are because of him otherwise tungekuwa ganja mtu sasa hiv. Akili yangu kipindi kile ilikuwa inaniambia dingi anatuchukia but now I understand he was/is the best dad ever in this world. Thank you papaaa
Wacha kabisa broo, alikuja kumwambia bi mama ndugu zako kama wakija hapa kwangu hawaswali basi waambie wasije hapa. Nyumba hii lazima watu waswali, kudaadeki maza wadogo wote wakawa wakija lazima waswali japo kumzuga lakini swala ni lazimaVinginevyo mkuu ungekua unashinda mortuary kule vitongoji
Sent from my SM-N910V using JamiiForums mobile app
Hahaha basi kumbe dingi ako ukauzu wake una afadhali.
Madingi makauzu/watabe hata kwa watoto wao kike hawawezi kwenda kabisaa achilia mbali kulala mpk asubuhi.Mtu yuko radhi aje kama ni dar ana inshu zake afikie hata kwa mdogo wake au lodge lkn sio kulala kabisaaa mpk asubuhi kwa binti yake.
Hahah makauzu hizo habari hawanaga kabisa aiseebaba yake sio mtata... analala mpaka alipoolewa mwanae...
wazee makauzu hiyo kitu ni mwiko
Hahaha, chief umeish sana pemba? Nimefanya kazi Al-Khamis CampWacha kabisa broo, alikuja kumwambia bi mama ndugu zako kama wakija hapa kwangu hawaswali basi waambie wasije hapa. Nyumba hii lazima watu waswali, kudaadeki maza wadogo wote wakawa wakija lazima waswali japo kumzuga lakini swala ni lazima
Miaka mitatu tu mkuu nlikuwa naishi mkoani flats za mapinduzi pale na wazee, wazee wakanihamisha maana nlikuwa sisikii ajabu mpaka mwalimu nilimpiga mawe siku moja kwa sababu alinichapa kosa halikuwa langu. aisee mzee wangu amefanya kazi kubwa sanaHahaha, chief umeish sana pemba? Nimefanya kazi Al-Khamis Camp