Wenye Tatizo la Shinikizo la Damu (High & Low Blood Pressure) Tukutane hapa

Wenye Tatizo la Shinikizo la Damu (High & Low Blood Pressure) Tukutane hapa

Kurunzi

JF-Expert Member
Joined
Jul 31, 2009
Posts
9,753
Reaction score
10,747
Habari wanajanvi, napenda kutumia fursa hii kuwasalimu, Moja kwa Moja niende kwenye Mada nimefungua uzi huu ili tupeane uzoefu wale ambao tunapbana na tatizo hili.

Mimi ni muhanga wa tatizo hili shinikizo la juu la damu - Hypertension kwa zaidi ya mwaka sasa.

Tatizo langu lilianza hivi, siku moja nikiwa kaenye shughuli zangu ghafla kichwa kiliniuma sana, nikapaatankizunguzumgunkikali sana nipata pamoja na macho kuona kama marue rue hivi, nilienda hospital kupata matibabu baada ya vipimo mbalimbali nilikutwa shinikizo la damu likiwa juu ilikuwa ni 168/110 pamoja na Colesterol ilikuwa juu sana.

Dr alishauri nianze dawa za pressure pamoja na Colesterol , binasfi sikuhafiki sana ushauri wa Dr, Pamoja ya kuwa nilichukuwa dawa nilimeza siku moja tu,sikuwahi kumeza tena baada ya kushauriana na Dr ambaye awali alishawahi nishauri nianze kudhibiti pressure yangu, mpaka leo sijatumia dawa niliamua kuanza diet na mazoezi.

Nilianza safari mpya ya kubadilisha mfumo wangu wa maisha hii sio kazi rahisi hasa ukizingatia inahitaji kujibana na kubadilisha mind set kwenye mambo uliyazoea, mimi ni mtumiaji sana wa pombe nakunywa bia sana, kwa wale wanywaji wanajua pombe inavyoshabiana na ulaji wa Nyama choma, Kitimoto na supu kwa wingi.

Maisha haya yalichangia sana kuwa na uzito uliopitilza kwani uzito ulifika kg 86 wakati urefu wangu ni 1.7m, hivyo uwiano na uzito na urefu ikawa nipo kwenye obesity line.

Baada ya kuanza hii safari mpya ya maisha miezi 2 iyopita maendeleo kidogo naona sio mbaya sana ingawa bado nahitaji kuendelea kupambana, nimepunguza uzito kutoka kg 86 - 82, na BP imeshuka mpaka 141/98 na wakati mwingine inashuka mpaka 133/89.

Nimeacha matumizi ya Carbs kwa sehemu kubwa, nimepunguza pombe nakunywa kwa wiki mara 1 au 2, nakula mboga za majani kwa wingi na matunda najitahidi angalau kwa wiki nafanya mazoezi ya kukimbia na kutembea angalau 1h au 2hrs kwa wiki mara 3-4, lengo ni kuburn calories angalau 4000kcl kwa wiki, wataalamu wansema ukiweza kuchoma calories 7700kcl kwa wikk maana yake unaweza kupunguza kg 1 ya uzito, Pia nimepunguza chumvi na niacha kutumia vitu byenye sukari na sukari kabisa.

Mgmfumo huu nataka niufanye kwa miezi sita huku naangalia maendeleo natumaini Mungu atanisaidia

Changamoto ninazokabiliana nazo, awali ilikuwa ngumu sana maana kuacha pombe inabidi upunguze marafiki, utafute activities za kufanya ule muda ambao ulikuwa unautumia kunywa hasa wikiend, nikifanya majarinio kadhaa mara tatu ya kuacha nikashimdwa jaribio la nne ndiyo nikafaulu

Upande wa maazoezi pia nilipata changamoto sana, kwanza ilinilazimu kuamka mapema sana 11 asubuhi nianze mazoezi au jioni saa 12:30 jioni baada ya mlo wa jioni, kudumisha ratiba hii ilikuwa ngumu awali lakini kwa sasa nimefaulu kwa kiasi chankuridhisha, Lakini pia awali nilipata shida ya goti kwasababubya mwili kuwa mzito hali iliyopeleka kukaa zaidi ya mwezi mmoja kuuguza goti, awali nilikuwa nakimbua sana kumbe ndiyo nikazua tatizo la goti.

Changamoto nyingine ni chakula wakati mwingine kama familia kuwa na special diet kwaajili yako inakuwa ngumu sana, inabidi ule chakula kilichopo.

Diet yangu najitahidi iwe hivi, Asubuhi, Aidha yai 1-2, kuchemsha au kukaangwa, ndizi mbivu 1, chai isiyo na sukari na punje mbili za kitunguu saaumu, maji kwa wingi.

Mchana, Matunda na mbogamboga na kaugali kadogo saba au tonge 6 an 8 ya kawaida au napiga desh nakunywa maji na ndizi 2

Jioni mbogamboga, magarage, tunda, na kama ni wali kidogo sana, kama kuna nyama nayo kidogo, maji chai ya moto na kitunguu saaumu then naenda mazoezi.

Najua wengine mnauzoefu tofauti naomba tushare wote.
 
Muhimu zaidi acha vilevi,

vilevi vinachochea sana presha na kuna muda vinafinya mpaka mishipa unaweza kupata matatizo mapya kama kusikia kelele masikioni mithiri ya mikwaruzo, upepo, miluzi, n.k.

Vilevi ni kama
  • Pombe
  • Sigara
  • Kahawa
  • Energy drinks kama redbull, energizer, mo extra, n.k.
  • Bangi
  • Ugoro
  • Mirungi
  • Madawa ya kulevya
 
Hyo hypertension inatibika, dawa ipo unapata bila malipo but utalipia baada ya kupona, tatizo ni uamninifu kwa watz ni zero, tumesambaza kwa watu zaidi ya 300 but waliolipa baada ya kupona ni chini ya 10%.
 
Naomba kujuzwa infact sijawahi Pima hizi issue lakini siku nikisema leo nakula vizuri yaani asb supu nzito mchana kitu kizito na jioni pia nikashushia hapo bia za kutosha huwa napata maumivu makali kweli upande wangu wa kushoto kwenye moyo, mpaka kwenye bega, kesho yake, what this could be friends?
 
Naomba kujuzwa infact sijawahi Pima hizi issue lakini siku nikisema leo nakula vizuri yaani asb supu nzito mchana kitu kizito na jioni pia nikashushia hapo bia za kutosha huwa napata maumivu makali kweli upande wangu wa kushoto kwenye moyo, mpaka kwenye bega, kesho yake, what this could be friends?
Kwanini usiende kupima mkuu, ni vema ukawahi mapema kwenda kupima ujue tatizo
 
Habari wanajanvi, napenda kutumia fursa hii kuwasalimu, Moja kwa Moja niende kwenye Mada nimefungua uzi huu ili tupeane uzoefu wale ambao tunapbana na tatizo hili...
Hongera sana mkuu.

Endelea na life style hiyohiyo itakusaidia sana na utakutana na faida nyingi mno hasa mwili ukishazoea hayo maisha. zaidi achana na madawa, diet ndio kila kitu punguza sana wanga na mafuta yasio mazuri kama ya wanyama tumia kwa nadra kama utaweza, ukiweza anza kitu kinaitwa intermittent fasting na fanya keto diet mara kadhaa kama utaweza ni utaona matokeo ya haraka upande wa cholesterol na uzito. Maana chakula kinamchango mkubwa sana kuliko mazoezi.

Itafika hatua ni unakula kidogo tu unahisi kutosheka na kushiba Kabisa.
 
Hongera sana mkuu.

Endelea na life style hiyohiyo itakusaidia sana na utakutana na faida nyingi mno hasa mwili ukishazoea hayo maisha. zaidi achana na madawa...
Asante ndugu, naomba ufafanuzi zaidi kuhusu hiyo intermittent fasting na Keto diet
 
Umechukua uamuzi mzuri sana, ingawa unapaswa kuchunguza kama kwenye familia yenu mna hiyo shida na hata kama mnayo je ukidhibiti hivyo vyanzo itaendelea kuwa juu, muhimu ni kuidhibiti kwa kufuata masharti yatakayokuwezesha ishuke, kama haishuki sasa anza kufuatilia sababu za kimwili na kiroho ili kuhakikisha kuwa unapona hayo maradhi...
 
Hyo hypertension inatibika, dawa ipo unapata bila malipo but utalipia baada ya kupona, tatizo ni uamninifu kwa watz ni zero, tumesambaza kwa watu zaidi ya 300 but waliolipa baada ya kupona ni chini ya 10%.
Tunakupataje mkuu/ ofisi ilipo
 
Pressure na matatizo ya Moyo,,baada ya miaka utakujaugua hivyo vitu
 
Sina uhakika sana zaidi kuna njia za asili kama kunywa chai yenye kikao, tangawizi, pilipili manga, maji, matunda, hii imekaa ki promo sana
Mkuu Kurunzi salam kwako. Nakubaliana na wewe kuwa walivyoeleza hii "Detonic" imekaa kipromo sana ikizingatiwa hawajaeleza "Side Effects' zake. ningetamani kutoka kwako na kwa wadau wengine hasa "Doctors" kuhusu hii Idea ya kusafisha mishipa na jinsi inaweza kuwa tiba mbadala ya vidonge kwa wale wenye shinikizo la damu.
Ahsante
 
Back
Top Bottom