Phillipo Bukililo
JF-Expert Member
- Dec 29, 2015
- 18,487
- 13,611
Ni katika kutafakari siasa za Tanzania na muelekeo mzima. Nikajikuta nikitafakari muda wote ambao viongozi wa vyama vya siasa wamekuwa wakishikilia hatamu za uongozi pasipo kuonyesha kuchoka, na wakiwa wepesi kurusha kila aina ya kashfa kwa chama tawala.
Freeman Mbowe aliingia katika uongozi mwaka 2004, amefikisha miaka 18 akiongoza CHADEMA na haonyeshi kupungukiwa nguvu wala hamu za kuwa mwenyekiti. Huo ni umri wa kijana anayeanza kupata haki ya kupiga kura anayefanya mtihani wa kidato cha sita.
Mbatia wa NCCR amefikisha miaka 22 akiwa kiongozi mkuu wa chama chake. Huyu ni Mzee wa matukio, anasubiri litokee janga la asili akosoe sera na mitazamo ya CCM akiwa kitaaluma ni mtu wa fani hizo za majanga. Pia husubiri upepo fulani wa kisiasa utokee ili apate cha kuongea kwa kuwaita wanahabari.
Profesa Lipumba amefikisha miaka 23 akiongoza CUF akikumbana na misukosuko ya kila aina. Huyu anajua sana kuishi na upepo wa kisiasa. Huwa anapata kazi zenye pesa nyingi za kiuchumi za Ulaya, anakaa huko miezi sita akirudi anakuwa yupo njema kabisa. Halafu anasikilizia mwito wa Hayati JPM au Mama SSH pale ikulu, kinachoongelewa wanakijua wenyewe!.
Mzee Lyatonga Mrema amefikisha miaka 23 akioongoza chama cha TLP, huyu ni mkongwe amekwepa mishale ya kila aina huko mwituni mpaka uzee umeshapiga hodi kwa sasa. Anahudhuria mikutano mikuu ya CCM na anatangaza hadharani kumuunga mkono mgombea wa CCM. Huwa naachwa na vicheko namna JK anavyomuongelea kwa vicheko kama vya masikhara.
Hao ni viongozi wakuu wa vyama vya upinzani Tanzania wanaoelekea kufikisha robo karne madarakani huku wakiikosoa demokrasia ndani ya nchi hii. Siasa ni akili kichwani mwako, ukiwa mjanja utaishi na watu vizuri huku ukizeeka na benki zikiwa zinaingia pesa ambazo ni pembeni ya kile kipato chako cha halali.
Freeman Mbowe aliingia katika uongozi mwaka 2004, amefikisha miaka 18 akiongoza CHADEMA na haonyeshi kupungukiwa nguvu wala hamu za kuwa mwenyekiti. Huo ni umri wa kijana anayeanza kupata haki ya kupiga kura anayefanya mtihani wa kidato cha sita.
Mbatia wa NCCR amefikisha miaka 22 akiwa kiongozi mkuu wa chama chake. Huyu ni Mzee wa matukio, anasubiri litokee janga la asili akosoe sera na mitazamo ya CCM akiwa kitaaluma ni mtu wa fani hizo za majanga. Pia husubiri upepo fulani wa kisiasa utokee ili apate cha kuongea kwa kuwaita wanahabari.
Profesa Lipumba amefikisha miaka 23 akiongoza CUF akikumbana na misukosuko ya kila aina. Huyu anajua sana kuishi na upepo wa kisiasa. Huwa anapata kazi zenye pesa nyingi za kiuchumi za Ulaya, anakaa huko miezi sita akirudi anakuwa yupo njema kabisa. Halafu anasikilizia mwito wa Hayati JPM au Mama SSH pale ikulu, kinachoongelewa wanakijua wenyewe!.
Mzee Lyatonga Mrema amefikisha miaka 23 akioongoza chama cha TLP, huyu ni mkongwe amekwepa mishale ya kila aina huko mwituni mpaka uzee umeshapiga hodi kwa sasa. Anahudhuria mikutano mikuu ya CCM na anatangaza hadharani kumuunga mkono mgombea wa CCM. Huwa naachwa na vicheko namna JK anavyomuongelea kwa vicheko kama vya masikhara.
Hao ni viongozi wakuu wa vyama vya upinzani Tanzania wanaoelekea kufikisha robo karne madarakani huku wakiikosoa demokrasia ndani ya nchi hii. Siasa ni akili kichwani mwako, ukiwa mjanja utaishi na watu vizuri huku ukizeeka na benki zikiwa zinaingia pesa ambazo ni pembeni ya kile kipato chako cha halali.