Wenzetu mmewezaje kuvunja 'cycle' ya umasikini wa ukoo/familia?

Wenzetu mmewezaje kuvunja 'cycle' ya umasikini wa ukoo/familia?

Anzisha ukoo wako. Yaani jihesabu wewe na mke wako kama ndio unaanza ukoo mpya, usijiassociate na mambo ya kiukoo yasiyo na maana.

Tengeneza value na system yako mpya warithishe na watoto
This is very true. Thank you.
 
Umaskini ni kuishi bila Kanuni, sheria, shabaha, malengo, Akili, juhudi, uthubutu na nidhamu

Kuondoka katika Laana ya umaskini itakupasa uzingatie hayo hapo juu.
Maskini ni MTU anayeishi Kiholela, anayelea Watoto Kiholela. Maskini Hana tofauti na mnyama
Motivational speakers bana.
 
Mkuu umasikini sio kipaji ni hari. Hari hairithishwi, ila kazi na mari zina rithishwa, ndo maana ni rahisi mtoto wa raisi kua Raisi au mtoto wamkulima kua mkulima pia. Ila hayo yote yana changiwa na Elimu na juhudi binafsi ya mtu uhusika, hata kama baba ni Raisi lakini mtoto hana elimu sio rahisi yeye kua rahisi
Andika vizuri unakera, sijui hari, mari,una shida gani? Mpaka mtu unaona kichefuchefu kusoma
 
  • Kuna familia na Koo zipo hakuna aliyemaliza form 4 wote elimu iliwashinda.
  • Kuna familia na Koo mmoja tu kafanikiwa kufika chuo na kumaliza ila kazi hana.
  • Kuna familia na Koo ndio unakuta masikini wa kukufuru, mabinti wote wamezalia nyumbani, hakuna aliyeolewa na vijana nao wote wameleta wake zao nyumbani. Hakuna hata mwenye afadhali ya maisha.
Nyumba ukiingia tu inanuka njaa. Wewe ndio umebahatika kupata vijihela, lakini hela yenyewe haikai unaenda unajikuta unarudi pale pale; ile circle ya umasikini haivunjiki.

Wenzangu mnafanyaje mliozaliwa kwenye umasikini?

View attachment 2493306
Picha kutoka maktaba

Mim ni mmoja wapo kwanza nimeishia darasa la 7 na kwenye ukoo wetu hakuna mtu alie vuka elimu hiyo baba yangu alikuwa mlevi mzuri kaka yangu pia n mnywaji mzuri ila mimi na ndugu zangu wengine wa 2 hatunywi pombe kabisa mama alikuwa mlevi japo kama miaka 13 ilio pita aliacha pombe kwa kifupi ukoo wa baba na mama wote wanywaji wa pombe baba aliishia darasa la kwanza mama aliishia la 2 baba zangu wadogo waliishia darasa la 4 wote ni wapiga pombe kupinduki na mmoja bahati mbaya alikufa kwa kutumbukia mtoni baada ya kulewa na watoto zao wote wameishia darasa la 7 wengine la 4 wengine hawaja soma kabisa hata hilo la 7 ila kwenye familia yetu wote tumefika darasa la 7 wengine wote hakuna alie faulu mitihani wa kuhitimu la 7 kama mimi ,mimi nili faulu kwa wakati huo shule za vipaji maalumu nilishindwa kwenda sekondari kulingana na umaskini kwenye uko wetu na familia yetu kwa namna fulani nilianza kujihudumia baadhi ya mahitaji ya shule nikiwa shuleni nikiwa darasa la 3 nilikopa kwa kaka yangu sh 500 nikaanzia biashara shuleni nikazalisha nikalipa deni hilo la sh 500 kwa kaka nikabaki na mtaji na nikawa najinunulia mahitaji madogo madogo ila bahati mbaya nilipo fika darasa la 6 nilifirisika mtaji wote nikaja nikafanya vibarua nikapata mtaji tena nikaendelea nao mpaka namaliza darasa la 7 nilipo faulu na kushindwa kwenda sekondari nikawa nashinda nyumbani na tukalima shamba la mahindi nyumban kama heka 4 bahati nzuri tulibarikiwa mavuno mwaka huo nikapewa gunia moja la mahind nikauza nikapata elfu 15 na nikaja nikapata kibarua dukani kwa mtu nilikuwa nikilipwa elfu 15 kwa mwez na pesa ya kula kwa siku sh 300 papo hapo baba na kaka waliondoka na kuhamia mkoa mwingine nikabaki mim mdogo wangu na mama nyumbani hivyo huyo mshahara wa elfu 15 kwa mwez pamoja na hiyo sh 300 kwa siku ilinilazimu kumlea mama yangu pamoja na mdogo wangu na kupambana kubadili maisha hakika MUNGU ni waa ajabu na ni mwema sana kwetu nilifanya kazi kwa uaminifu mkubwa kwa miaka 5 hivi sasa ninapo andika ujumbe huu ninamtaji wa zaidi ya bilion moja kwenye biashara yangu nina mashamba napangisha watu baada ya kuachana na kilimo nina apartment moja ipo kwenye jengo la ghorofa nimeinunua kariakoo watoto wangu wanasoma shule nzuri nilisha jenga home mama anakijumba kizuri zuri kwa ujumbe huu nawapa moyo watu au watoto wote mlio zaliwa familia na koo masikini msikate tamaa mtegemeeni MUNGU heshimuni wazazi wenu usimwache mama yako akiteseka hata iweje fanya kazi kwa bidii kwa mapenzi ya MUNGU wetu lazima ufanikiwe leo hii mimi naheshimiwa na vijana nilio soma nao walio kuwa na maisha mazuri kwao nimewazidi mbali mno nimesafiri nchi kadhaa hakika MUNGU ni mwema
 
Mim ni mmoja wapo kwanza nimeishia darasa la 7 na kwenye ukoo wetu hakuna mtu alie vuka elimu hiyo baba yangu alikuwa mlevi mzuri kaka yangu pia n mnywaji mzuri ila mimi na ndugu zangu wengine wa 2 hatunywi pombe kabisa mama alikuwa mlevi japo kama miaka 13 ilio pita aliacha pombe kwa kifupi ukoo wa baba na mama wote wanywaji wa pombe baba aliishia darasa la kwanza mama aliishia la 2 baba zangu wadogo waliishia darasa la 4 wote ni wapiga pombe kupinduki na mmoja bahati mbaya alikufa kwa kutumbukia mtoni baada ya kulewa na watoto zao wote wameishia darasa la 7 wengine la 4 wengine hawaja soma kabisa hata hilo la 7 ila kwenye familia yetu wote tumefika darasa la 7 wengine wote hakuna alie faulu mitihani wa kuhitimu la 7 kama mimi ,mimi nili faulu kwa wakati huo shule za vipaji maalumu nilishindwa kwenda sekondari kulingana na umaskini kwenye uko wetu na familia yetu kwa namna fulani nilianza kujihudumia baadhi ya mahitaji ya shule nikiwa shuleni nikiwa darasa la 3 nilikopa kwa kaka yangu sh 500 nikaanzia biashara shuleni nikazalisha nikalipa deni hilo la sh 500 kwa kaka nikabaki na mtaji na nikawa najinunulia mahitaji madogo madogo ila bahati mbaya nilipo fika darasa la 6 nilifirisika mtaji wote nikaja nikafanya vibarua nikapata mtaji tena nikaendelea nao mpaka namaliza darasa la 7 nilipo faulu na kushindwa kwenda sekondari nikawa nashinda nyumbani na tukalima shamba la mahindi nyumban kama heka 4 bahati nzuri tulibarikiwa mavuno mwaka huo nikapewa gunia moja la mahind nikauza nikapata elfu 15 na nikaja nikapata kibarua dukani kwa mtu nilikuwa nikilipwa elfu 15 kwa mwez na pesa ya kula kwa siku sh 300 papo hapo baba na kaka waliondoka na kuhamia mkoa mwingine nikabaki mim mdogo wangu na mama nyumbani hivyo huyo mshahara wa elfu 15 kwa mwez pamoja na hiyo sh 300 kwa siku ilinilazimu kumlea mama yangu pamoja na mdogo wangu na kupambana kubadili maisha hakika MUNGU ni waa ajabu na ni mwema sana kwetu nilifanya kazi kwa uaminifu mkubwa kwa miaka 5 hivi sasa ninapo andika ujumbe huu ninamtaji wa zaidi ya bilion moja kwenye biashara yangu nina mashamba napangisha watu baada ya kuachana na kilimo nina apartment moja ipo kwenye jengo la ghorofa nimeinunua kariakoo watoto wangu wanasoma shule nzuri nilisha jenga home mama anakijumba kizuri zuri kwa ujumbe huu nawapa moyo watu au watoto wote mlio zaliwa familia na koo masikini msikate tamaa mtegemeeni MUNGU heshimuni wazazi wenu usimwache mama yako akiteseka hata iweje fanya kazi kwa bidii kwa mapenzi ya MUNGU wetu lazima ufanikiwe leo hii mimi naheshimiwa na vijana nilio soma nao walio kuwa na maisha mazuri kwao nimewazidi mbali mno nimesafiri nchi kadhaa hakika MUNGU ni mwema
Kwa kweli maisha hayana formula shukran una miaka mingapi mkuu
 
Anzisha ukoo wako. Yaani jihesabu wewe na mke wako kama ndio unaanza ukoo mpya, usijiassociate na mambo ya kiukoo yasiyo na maana.

Tengeneza value na system yako mpya warithishe na watoto
Kabisaaaa,sihitaji tena kujihusisha na mambo ya kiukoo,nimemsomesha mdogo wangu wa kike na watoto wa dada zangu leo hii wanadiriki hata kunitukana mimi kaka yao na mjomba wao nimeamua kumchukua dada yangu anayenifuata na watoto wake nimempa nyumba na tumejitenga na ndugu hao na watoto wetu wataoana ili kijenha ukoo we uwezo na imara
 
watanzania karibia wote chimbuko lao ni umasikini tu lakini leo tunashudia watu waliotokana na familia hizo masikini wana majina makubwa mfano lipumba baba yake alikuwa mkata mkaa magufuli akulelwa na babake mzazi bana alimtelekeza sababu dhiki

nchemba waziri wa fedhe kazaliwa ilamba singida tena kwenye nyumba ya tembe hiyo ni nyumba yenye adhi ya chini kabasa

raisi wa zanziba alikuwa kuli mbeba mizigo kwenye meli

waarabu na waindi unao waona walikuja huku kukimbia njaa na dhiki huko kwao baadhi yao waliku bila hata viatu

maisha haya tafusili hakuna ajuae kesho yake
Nani Karume au Mwinyi Jr?
 
Umeuliza swali muhimu sana na hii ni elimu kabisa. Wakati tukiwa shule tulifundishwa dhana ya 'Matawi ya familia' tukawataja babu, bibi, baba, mama, watoto hatukufundishwa zaidi ya hapo.

Sasa kwenye numeriolojia ndio kuna haya mambo ya matawi ya familia, huko unahesabu vizazi vinne unavijua historia ya wazaliwa wake wote hakika utafahamu ni mzaliwa yupi au wanagapi na wanani atakuwa kama vizaliwa wa kizazi kilichotangulia.

Sasa ukishafahamu hiyo elimu (ngumu kuielezea yote hapa), utaweza kujua kabisa kuwa wewe/mimi nipo kwenye kundi gani na nitakuwa na hatma ya aina gani, kutokea hapo ndipo.unapotakiwa sasa kuchukua hatua.kurekebisha mambo yasikukute.

Kuna watu wataoa na kuolewa na kisha wenza wao kufariki baada ya miaka michache hii.huwasio bahati mbaya bali huwa ni mzunguko wa matawi ya familia, ukimchunguza vizuri huyo mtu utakuwa kuna mtu kwenye kizazi chao naye alikuw hivyo hivyo.

Au unakuta kuna wanawake hawaolewi au wakiolewa hawadumu kwenye ndoa ukiwachunguza kwenye vizazi vinne vya familia yao utakutana na mtu wa sampuli hiyo hiyo.

Sasa basi ili kuepuka haya mambo ambayo huwa pia yanaitwa laana na mikosi ni wewe sasa kujitenga na mfumo wa vizalia vyenu. Kama huwa mnaoa watu wa kabila lenu wewe nenda kaoe mtu wa kabila tofauti tena awe na historua.tofauti kabisa ya kimalezi na ya kwako

Pia hama eneomlilozoea kuishi vizazivyenu, nenda mbali kabisabafili mfumo wa maisha, hata ikiwezekana usijiitekwa jina la ukoo wenu, jitenge kabisa na hayo mambo lazima utaanzisha kizazi tofauti kisicho na balaa za kwenu.

Ila pia kumbuka kuna faida na hasara za kufanya hivyo hasa hasa unaweza kupoteza yale mazuri yanayobebana na mfumo wenu. Hivyo ni swalala kuzingatia pia kabla ya kuchukua maamuzi.
 
Mara nyingi umasikini wa familia huvunjwa kwa mmoja wao "kuthubutu". Ama kwa kucheza rafu mpaka ufunge goli au kwa namna yoyote Ile. Find money by any means.
 
Jua kwamba matatizo mengi ya kifamilia ni ya kijenetic mengine ni ya kimazingira na mengine ni ya kimalezi na mengine ni ya kiroho. Yote haya yaweza kutengeneza mzunguko usio na mwisho (vicious cycle) ambapo ni ngumu kutoka.

Chunguza vizuri kujua nini chanzo cha kushindwa kwa familia au ukoo wenu, halafu chukua hatua stahiki.
Hii hoja yako ni nzito. Tukisoma biblia tunaona hata Yesu alizaliwa kwenye ukoo ambao kizazi chake kimeanzia kwa Ibrahim then Isaka, Yakobo hadi kina Daudi na Suleman.. yaani ukoo flani hivi wenye utakatifu. Nimejiuliza sana kwanini Yesu hakuzaliwa kwenye ukoo labda ulioanzia na Kaini.. haya mambo ukitafakari pia kiroho inatisha.
 
Umeuliza swali muhimu sana na hii ni elimu kabisa. Wakati tukiwa shule tulifundishwa dhana ya 'Matawi ya familia' tukawataja babu, bibi, baba, mama, watoto hatukufundishwa zaidi ya hapo.

Sasa kwenye numeriolojia ndio kuna haya mambo ya matawi ya familia, huko unahesabu vizazi vinne unavijua historia ya wazaliwa wake wote hakika utafahamu ni mzaliwa yupi au wanagapi na wanani atakuwa kama vizaliwa wa kizazi kilichotangulia.

Sasa ukishafahamu hiyo elimu (ngumu kuielezea yote hapa), utaweza kujua kabisa kuwa wewe/mimi nipo kwenye kundi gani na nitakuwa na hatma ya aina gani, kutokea hapo ndipo.unapotakiwa sasa kuchukua hatua.kurekebisha mambo yasikukute.

Kuna watu wataoa na kuolewa na kisha wenza wao kufariki baada ya miaka michache hii.huwasio bahati mbaya bali huwa ni mzunguko wa matawi ya familia, ukimchunguza vizuri huyo mtu utakuwa kuna mtu kwenye kizazi chao naye alikuw hivyo hivyo.

Au unakuta kuna wanawake hawaolewi au wakiolewa hawadumu kwenye ndoa ukiwachunguza kwenye vizazi vinne vya familia yao utakutana na mtu wa sampuli hiyo hiyo.

Sasa basi ili kuepuka haya mambo ambayo huwa pia yanaitwa laana na mikosi ni wewe sasa kujitenga na mfumo wa vizalia vyenu. Kama huwa mnaoa watu wa kabila lenu wewe nenda kaoe mtu wa kabila tofauti tena awe na historua.tofauti kabisa ya kimalezi na ya kwako

Pia hama eneomlilozoea kuishi vizazivyenu, nenda mbali kabisabafili mfumo wa maisha, hata ikiwezekana usijiitekwa jina la ukoo wenu, jitenge kabisa na hayo mambo lazima utaanzisha kizazi tofauti kisicho na balaa za kwenu.

Ila pia kumbuka kuna faida na hasara za kufanya hivyo hasa hasa unaweza kupoteza yale mazuri yanayobebana na mfumo wenu. Hivyo ni swalala kuzingatia pia kabla ya kuchukua maamuzi.
Dawa ni damu ya YESU pekee
 
Dawa ni damu ya YESU pekee
Unaamini kuwa huyu Yesu unayemtaja hapo sio dawa pekee?

Chukua mfano mtu sio mkristu dawa itakuwa ni nini?, tuseme ni budha, au Zen au Hindu

Kuna mambo tuwe tunawaza tofauti
 
Back
Top Bottom