Wenzetu mmewezaje kuvunja 'cycle' ya umasikini wa ukoo/familia?

Wenzetu mmewezaje kuvunja 'cycle' ya umasikini wa ukoo/familia?

Kitu ambacho watu wengi hatutaki kukubali ni kwamba, dunia ni uwanja wa vita na yale mengi ya giza ambayo utandawazi unatushauri tuyapuuze ndo yenye kuamua hatima ya wengi.

Kufanikiwa sio tu shule na kufika chuo kikuu, sio mentality wala mipango na wala sio kuchapa kazi saaaana kama wengi tunavyotaja kuaminishana hapa. Wapo watu wana hivyo vitu na bado hawawezi kutoboa leo wala kesho.
Watoto hawatakuelewa
 
Watoto hawatakuelewa
Ukikaa na waliofanikiwa kisha wakaamua kutokuwa wachoyo wa njia zao kwako utayajua mengi sana, kwa bahati mbaya wengi wao huficha na kuamua kuja na ngonjera ambazo zitafanya jamii iwakubali badala ya kuwaogopa.

Hapo ndo utasikia matajiri wanakupa ngonjera zao za uongo, eti sali sana, fanya kazi kwa bidii na mentality😂.

Kuna watu wamefanya kazi kwa bidii tangu ujana wao mpaka sasa wanazeeka hawana hata 10M benki.
 
Ni jambo zito sana ila linahitaji mkakati mkubwa kwa familia katika kulitokomeza

Mama na baba wapya wajue wanapambania nini kwa ajili ya kizazi chao na si bora kuzaa kwa nia ya kuijaza dunia bila ya kupanga namna gani huyo mtoto mnataka awe, hivyo basi mkifeli ktk hilo la kujua na kumuandaa mtoto au watoto mtakao waleta wawe katika viwango vipi vya maisha basi ni wazi itakuwa ngumu kwa watoto kufikia hatua ya kuukwepa ufukara

Kikwazo ni hizo ndoa au mahusiano ya baba na mama ya kuweza kulea kwa pamoja huku mkijenga hiyo misingi kwa watoto wenu ndoa hazipo na kama zipo nyingi zinakuwa mfu au za mitikisiko mikubwa ikipelekea kila mzazi kuvutia kwake.

Kupambana na ufukara ni vita kuubwa inayohitaji imani kuu kwa muumba wako, ari kuu, nidhamu, mikakati, maelewano na uvumilivu usio kifani
Point Sana mkuu na Kumweka mbele Sana Mungu
 
Jamii nyingi za waliofanikiwa,..Wayahudi, Wahindi, Wachaga, Wakinga, Waha..etc
Hivi katika jamii zilio fanikiwa kweli ni sawa kuweka wayahudi kundi moja na Waha, wachagga na wakinga, mbona hao watu ni kawaida sana hayo mafanikio siaoni, neenda kigoma kibondo kasuru ujiji 95% wakutupwa, neenda wilaya za Moshi hamna tofauti na wilaya zingine za Tz, tofaiti iko kwenye individua basis. Sio community base, Tz is the same popote.
 
Hivi katika jamii zilio fanikiwa kweli ni sawa kuweka wayahudi kundi moja na Waha, wachagga na wakinga, mbona hao watu ni kawaida sana hayo mafanikio siaoni, neenda kigoma kibondo kasuru ujiji 95% wakutupwa, neenda wilaya za Moshi hamna tofauti na wilaya zingine za Tz, tofaiti iko kwenye individua basis. Sio community base, Tz is the same popote.
Ushirikiano/Kusaidiana kimaendeleo.
 
Baba yangu ni wa Kwanza kwao na alifika form 6.... Akapata kazi wakati wa MWINYI

Mimi wa Kwanza kwa Baba yangu nikafika chuo....Sijapata kazi mpk sasa.


Ila MIZIMU ya ukoo imeniambia nikitaka kutoboa nisifanye kazi wala kuajiriwa wamenipa UGANGA wao watanipa UTAJIRI kupitia watu.


KOO zetu zina Siri kubwa sana
[emoji23][emoji23]
 
Mkuu mimi na kupinga umasikini ni man made hauna uhusiano wowote na uumbaji au kiroho, hayo yote ni visingizio vya wale walioshinda kupambanua udhaifu wao na kuishia kumsingizia Mungu.......wa kuristo wa kimißsionary ndo walioanzisha hiyo theory ya kusema umasikini unatoka kwa Mungu, na masikini amebarikiwa kwake ataenda mbinguni, hizo kauli zilitumiwa na hao watu ili exploit mali za waafrika na kutengeneza utii kwa wafasi wao masikini, we can fight and eradicate poverty.
Naunga mkono hoja
 
Ulaya kuna umasikini mkubwa sana ila viwango hutofautiana na uko kwetu, kwao Serikali inatoa dole money kila mwezi kwa wale masikini kupata basic kama chakula na nguo, uku kwetu tuna umasikini wa kipato na wa akili ya viongozi wetu, hamna watu wenye roho ya kimasikini kama viongozi wa Africa.
Tasaf
 
Kijana una miaka 23, huna biashara/kazi yenye kukuingizia kipato cha uhakika,,,,,, unaenda kuoa binti ambae kwao yeye ni wa kwanza na ana wadogo zake sita wote wanakutegemea shemeji uwasomeshe,, uwalishe wazaz wao,,, uwape mahtaji yao ya msingi,, uwajengee nyumba n.k what do u xpect??

Baada ya mda fulan unapata mtoto wa kwanza unampeleka kusoma sant kayumba,, anafika form four anafeli, anakua boda boda(kwa sababu hujamuandalia future yyte na wala huna mtaji wa kumpa),,,, ,, na yy tena anaoa kulekule,,,, mzunguko unaendelea

Suluhisho:usianzishe familia kama ww mwenyewe hujitoshelezi,,, unaongeza idadi ya wahalifu(watoto wa mitaan+panyaroad) na kuendeleza vicious cycle.
 
Mara nyingi umasikini unasababishwa na wenyewe wa family maana full kufanyiana ushirikina hili kila mtu abaki masikini asije kutulingia unakuta mama mkubwa anamfanyia ubaya mtoto wa dada yake asifanikiwe sababu tu wa kwake hana mafanikio kwahyo afanane na wanae.
 
Kitu ambacho watu wengi hatutaki kukubali ni kwamba, dunia ni uwanja wa vita na yale mengi ya giza ambayo utandawazi unatushauri tuyapuuze ndo yenye kuamua hatima ya wengi.

Kufanikiwa sio tu shule na kufika chuo kikuu, sio mentality wala mipango na wala sio kuchapa kazi saaaana kama wengi tunavyotaja kuaminishana hapa. Wapo watu wana hivyo vitu na bado hawawezi kutoboa leo wala kesho.
BIG YESSSSSSSSSSSSSSSSSS
 
Mzee ni civilized na msomi huwa haamini hayo mambo ya giza ila kutoamini kwake hakukuzuia watu kumuharibia mipango ya kimaisha.
Hawa waS3NGE kumbe hata usipojihusisha na hizi mambo wanakudaka tu?

Kwa visa hivi vyote vya humu hivi tuwaiteje wanaosema hakuna uchawi? Kwa hiyo tunakubaliana wao ndiyo wachawi wenyewe au siyo?
 
Hawa waS3NGE kumbe hata usipojihusisha na hizi mambo wanakudaka tu?

Kwa visa hivi vyote vya humu hivi tuwaiteje wanaosema hakuna uchawi? Kwa hiyo tunakubaliana wao ndiyo wachawi wenyewe au siyo?
Hao ndio mawakala, usione mtu anapinga pinga tu kazi za giza kumbe ni wakala.
 
Ukikaa na waliofanikiwa kisha wakaamua kutokuwa wachoyo wa njia zao kwako utayajua mengi sana, kwa bahati mbaya wengi wao huficha na kuamua kuja na ngonjera ambazo zitafanya jamii iwakubali badala ya kuwaogopa.

Hapo ndo utasikia matajiri wanakupa ngonjera zao za uongo, eti sali sana, fanya kazi kwa bidii na mentality[emoji23].

Kuna watu wamefanya kazi kwa bidii tangu ujana wao mpaka sasa wanazeeka hawana hata 10M benki.
Mtu akipinga hili jua ndiye mchawi mwenyewe
 
Kikubwaa na zaliwa naishi then baada ya kuishi nakufaaa na maisha menginee yanaendelea why kujipa stress na njia nayo pitaa ingali kuna serikali inabidi itekelezeee ayaaa ....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom