Wenzetu mmewezaje kuvunja 'cycle' ya umasikini wa ukoo/familia?

Wenzetu mmewezaje kuvunja 'cycle' ya umasikini wa ukoo/familia?

Ulaya kuna umasikini mkubwa sana ila viwango hutofautiana na uko kwetu, kwao Serikali inatoa dole money kila mwezi kwa wale masikini kupata basic kama chakula na nguo, uku kwetu tuna umasikini wa kipato na wa akili ya viongozi wetu, hamna watu wenye roho ya kimasikini kama viongozi wa Africa.
Hoja nzito Sana hii, umaskini wa kipato unachangiwa pia na sera za kiuchumi na hali ya kiuchumi ya nchi husika.
 
Kama mzazi hana uwezo akishindwa kumsomesha mtoto sasa si ndio anaanza kurithi umaskini.
Kuna watu hata darasa la saba hawakuhitimu, ila wameweza kutoboa maisha. Shule sio kigezo peke cha kuondokana na umasikini, pia natural brightness naenyewe ina changia, Musukuma asingekua mbuge kama shule ndo kugezo peke.
 
Kunakuwa na matatizo ya kiroho yani, kwa ambao wazazi hawakuwa na mawazo na dunia kuwa kuna watu wa hovyo wanaweza kuharibu future ya familia ndio hivyo tena mnaweza kuporomoka kutoka A class family to F Class...

Laiti mzee angejua mapema kuwa dunia haiko jinsi anavyofikiri maybe familia isingeparanganyika tukarudi kwa ground!

Watoto ndio tuna suffer kwa kufidia uzembe ule.
. Wazazi wanafanyaga vitu kwa manufaa yao na starehe zao ila yanakuja kuharibu maisha ya vizazi hata vitatu mbele
 
Serikali izuie watu kuzaa si upumbavu. Imeshindwa kuendesha nchi vizuri ndio maana hadi leo watu ni masikini. Ianze kuacha ufisadi kwanza na ijikite kutengeneza mazingira wezeshi.
Serikali inachoweza fanya ni kuwekeza kwenye huduma za kijamii na miundombinu.
Huko kwingine tukiisubiria serikali utajikuta unailaumu milele
 
Serikali inachoweza fanya ni kuwekeza kwenye huduma za kijamii na miundombinu.
Huko kwingine tukiisubiria serikali utajikuta unailaumu milele
Kwani Libya Gadafi aliwezaje? Hatuna viongozi wenye akili bali makundi ya fisi waliojaa tamaa na ubinafsi.

Kuna uwezekano taifa lika focus na rasilimali na kuzipeleka panapohitajika ulimwenguni na maisha yakabadilika completely.

Kwani marekani graduate ni boda boda? Ni uvivu wa wenye wadhifa kufanya majukumu yao.

Watafute masoko ya bidhaa za kilimo, we have plenty of arable land. Unakuta soko la bidhaa flani analishikilia waziri kimya kimya na ana export mzigo kwa kampuni yake. Humu humu Africa masoko yapo ila unakuta waziri anataka amonopolize soko anauza yeye pekeyake nyie wengine mlanguane kwa madalali temeke, buguruni, manzese

Nyie wengine hizo process za ku export mzigo vibali vyake tu kupata unaacha na shughuli yenyewe.
 
Umasikini upo wa aina tofauti tatizo tumejulisha masikini zote sehemu kitu kinachofanya tushindwe kusimama kwenye misingi ipi, Kuna umasikini wa mtu binafsi huyo mtu kama ni masikini ajitafakari binafsi matendo yake maana umeambiwa utakula kwa jasho hivyo Kila mtu binafsi afanye kazi Ili ajipatie kipato chake na siyo kusubiri kama mtoto upewe mahitaji yako Sasa hapo ukikwama ujitafakari matendo yako kama siyo kikwazo.
Umasikini wa pili ni umasikini wa familia na tunaposema familia ni wazazi na watoto wao Sasa hapo mwenye wajibu wa kuondoa umasikini kwa kizazi chake ni baba, baba anatakiwa kujua anahitaji watoto wangapi atakaoweza kuwatunza na kuwaandalia urithi maana mali mtu hupewa na babaye hivyo kama baba amezaa bila uwezo wa kutunza familia lawama ni zake na akisaidiwa na mkewe kulinda Mali za familia zisitapanyike hovyo na Hawa familia wanatakiwa kuishi kwa akili na siyo kuishi kama wanyama wanavyoishi mwituni na iwapo wataishi kama wanyama yaani baba Hana mpango wa kujenga nyumba kwaajili ya uzao wake, mavazi familia Haina mpaka wanatembea uchi au nguo zimechanika, chakula hakuna mpaka wakajikombe kwa jirani, watoto hawasomeshi Sasa huyo mzazi mnyama mwitu anatakiwa kuazibiwa na serikali na akionekana ataharibu jamii basi ananyanganywa watoto na kutoruhusiwa kuoa tena kwa kuwekwa gerezani maisha yake yote hata kama ni mama anazaa bila kujua matunzo ya watoto tatizo hapo serikali imezembea wajibu wake kitu kilichozalisha wanyama watu wengi wanaoishi bila utashi wa akili.

Umasikini unaofata ni umasikini wa ukoo huu unapatikana kwa viongozi wa ukoo waliotangulia kutowajibika kuandaa kizazi cha baadaye, yaani wababa wa huo ukoo hawakuwa na utashi wa akili wakutengeneza maisha yao vizuri na vizazi vyao, ndo zile Koo zinasubiri serikali ije iwape mahitaji yao ila wao wanashinda vilabu vya pombe wakipombeka, watoto hawana elimu Wala Mali za wazazi za kujikwamua kiuchumi Bali mzazi anasubiri mtoto aje amrithishe mzazi au mzungu akamsomeshee watoto wake yeye aje afaidike bila kuwekeza nguvu zake Sasa huu ukoo wa hivi unabaki masikini vizazi na vizazi na mtu binafsi hawezi kuwainua wote maana na yeye ataangukiwa na uzito wa watu walioshindwa zana ya kula kwa jasho lako mwenyewe.

Umasikini wa mwisho ni umasikini wa nchi, Sasa hapa ni wale viongozi waliochaguliwa kuongoza Kila mtu katika nchi kuanzia mimba ya mtoto mpaka kuzaliwa na mwisho wazee,
Sasa tunaona Hawa viongozi ni watu muhimu sana wawe watu wenye kupewa maarifa ya ziada jinsi ya kuondoa umasikini wa nchi nzima kwa kuhakikisha Kila mtu aliyekatika nchi anatimiza wajibu wake yaani kuwa na jamii inayojitambua na kujua wajibu wake mfano jamii inajua umuhimu wa shule basi wakati wa kutengeneza mtaa ile jamii itatenga eneo la shule ngazi zote na siyo kujenga tu nyumba eneo lote alafu baadaye wakatafute elimu mtaa wa pili, wataweka maeneo yote muhimu kama watu wenye akili na siyo wanyama wanaishi mtaa huo Sasa hapo ndo serikali Ili isipate lawama kwa kushindwa kuongoza vizuri ndo inaweka viongozi wa mtaa Ili waisaidie kutenga maeneo ya jamii Ili wao waje wajenge miundombinu muhimu imufikie Kila mtu, huduma muhimu zimfikie Kila mtu ili hao watu waendelee kuwepo maana Kila mtu anaumuhimu sana katika nchi bila hao watu basi na nchi haipo maana hao watu wameamrishwa wakafanye kazi kwa lazima Ili wapate vipato na hivyo vipato vinachukuliwa Kodi inayojenga nchi na kuondoa umasikini wa nchi na kufanya nchi iwe tajili wa huduma zote muhimu zinazomfikia Kila mmoja kuanzia mtoto akiwa tumboni anatakiwa kulindwa na serikali maana ni kizazi cha baadaye ila pia ni mtoto katika familia na tena anatoa ajira kwa watu wa afya wa uzazi, atakuja kutoa ajira kwa kada za elimu na baadaye kufanya kazi Ili atengeneze kipato chake na kujenga nchi.

Hivyo umasikini ni matokeo ya kushindwa kutimizwa wajibu wakati sahihi na hii inaanzia mtoto mpaka Mzee, mfano Kuna watoto walipelekwa shule wakaacha kufata elimu na kujiingiza kwenye uhuni na baadaye wakawa baba au mama waliochezea shule lakini hao watu hawaishi kulalamika kwamba wao masikini wahudumiwe na watoto wao, wazazi wanaokaa bila kutafuta nao wanalia umasikini wakitamani watu wengine wajitolee kufanya kazi kwaajili yao, ukoo mzima kulilia mtu mmoja afanye kazi kwaajili yao na wengine wasitoke jasho Katu ila nao wanalia umasikini hauwaachi, Serikali nayo kushindwa kusimama kwenye sehemu yake ya kujenga huduma muhimu, miundombinu Kila mtaa Ili watu wasikwame kwenda kufanya kazi na kulipa Kodi, kusimamia maadili ya jamii nzima na kuondoa zana ya mtu mzima anaweza kujiongoza wakati hakuna kitu kama hicho yaani Bora watoto hapo kwenye watu wazima wengi hawana maadili tena wanafanya matendo kama wanyama wasio na utashi wowote kwa vile hawawajibishwi yaani haishitui Sasa kukuta vijana wanaangalia television bar bila kufanya kazi na watu wazima hawajulikani nini wanafanya Ili kuingiza kipato ni kulala tu au kuzunguka kuomba badala ya kufanya kazi kitu kinacholeta umasikini kwa nchi, imagine Kuna shule imeajili walimu miaka kumi na tatu bila wanafunzi na wao hawashituki tu ndo maana nasema viongozi wasipokuwa na maarifa ya juu ya kuwaongoza watu kwa kusimamiwa muda wote kama watoto Hawa tunaowaita watu wazima wataendelea kuleta umasikini wa kujitakia wao binafsi, jamii na nchi pia, Kila mtu hata kiongozi asimamiwe na mtu wa juu yake Ili kazi zifanyike na kuzaa kazi zingine Ili watu waondoe umasikini kwa jasho lao.
 
Hili nalo pia ni tatizo katika familia nyingi,

Unakuta mtu mmoja kafanikiwa kwenye maisha katika familia yao,na anaona ufahari sana pale ndugu wanapokuja kumlilia shida nae huwasaidia,na anatamani maisha yawe hivyo hivyo,yaani anatamani miaka yote wenzake wawe chini yake tu ili waendelee kumlilia shida,hujiona ni kama mfalme fulani hivi,sasa mtu kama huyu akianguka ghafla kiuchumi,familia/Ukoo wote wanapata tabu,

Unapobarikiwa,jaribu kuwainua na wengine hasa watu wako wa karibu,ili kama mmoja wenu ataanguka kiuchumi basi wawepo na wengine ambao watamuinua na mwenzao tena,hili linafanyika sana kwa baadhi ya jamii za Waarabu na Wahindi,

Kitu muhimu ndani ya Koo ni lazima kuwe na upendo,kuheshimiana,kuaminiana....na hizi good discipline and attitude haziji ghafla au kimiujiza,hujengwa katika malezi tangu utotoni.

Inategemea na familia pia walivyolelewa pamoja kuna familia kila mtoto kalelewa tofauti kunakuwa hakuna bond
 
Serikali inachoweza fanya ni kuwekeza kwenye huduma za kijamii na miundombinu.
Huko kwingine tukiisubiria serikali utajikuta unailaumu milele
Na hakuna serikali inayoweza kukutatulia tatizo asilimia zote. Na ndo maana as long as unaishi katika hii dunia..wewe ulistruggle tangia unatungwa. Kulikua na sperms kadhaa na sperm iliyoshinda ndo wewe ukatungwa. Ukakaa miezi tisa ukatoka ukiwa hai. Umepita kote mpaka leo uko hai. You are naturally a winner..so ni jukumu lako kuswim and fight mpaka mimba zitungwe kwenye uchumi, ndoa, maendeleo, ukoo na mafanikio yazaliwe kote huko.

It involves God's grace+ bidii+ conducive environment. Serikali ndo inatakiwa iprovide conducive environment ila kama ikitokea hakuna basi kama kuna efforts na God's Grace utafanikiwa. Lakin wako wasiomuabudu Mungu so efforts zinawabeba. Sasa sijui kama huwa grace bado inakuwepo..probably. maana sote ni wa Mungu either umuabudu ama la.

Inshort kubreak chains of poverty ni Efforts kwa ukubwa. Bidii, discipline yote hayo. Hata kuwe na generational curse ya aina gani..kama kuna God's Grace itavunjika tu. Am open to learn zaidi na zaidi.
 
Kwani Libya Gadafi aliwezaje? Hatuna viongozi wenye akili bali makundi ya fisi waliojaa tamaa na ubinafsi.

Kuna uwezekano taifa lika focus na rasilimali na kuzipeleka panapohitajika ulimwenguni na maisha yakabadilika completely.

Kwani marekani graduate ni boda boda? Ni uvivu wa wenye wadhifa kufanya majukumu yao.

Watafute masoko ya bidhaa za kilimo, we have plenty of arable land. Unakuta soko la bidhaa flani analishikilia waziri kimya kimya na ana export mzigo kwa kampuni yake. Humu humu Africa masoko yapo ila unakuta waziri anataka amonopolize soko anauza yeye pekeyake nyie wengine mlanguane kwa madalali temeke, buguruni, manzese

Nyie wengine hizo process za ku export mzigo vibali vyake tu kupata unaacha na shughuli yenyewe.
Tatizo ni siasa, watu hawataki lipa kodi sababu hazijulikani zaenda fanya nini
 
Baba yangu ni wa Kwanza kwao na alifika form 6.... Akapata kazi wakati wa MWINYI

Mimi wa Kwanza kwa Baba yangu nikafika chuo....Sijapata kazi mpk sasa.


Ila MIZIMU ya ukoo imeniambia nikitaka kutoboa nisifanye kazi wala kuajiriwa wamenipa UGANGA wao watanipa UTAJIRI kupitia watu.


KOO zetu zina Siri kubwa sana
 
Mkuu kama mtoto anaweza kurithi kipaji cha mzazi inashindikanaje kurithi umaskini? Haishangazi mtoto wa footballer kuwa footballer, mtoto wa Rais kuwa Rais, mtoto wa mfanyabiashara kuwa mfanyabiashara nk. Hata mtoto wa maskini kuwa maskini inawezekana sana kama hatua za makusudi zisipochukuliwa kwa sababu hata mtoto wa Rais kuwa Rais huwa lazima jitihada ziwepo pia. Kipaji tu hakisaidii.
Upo sahihi kabisa, suala la kurithi lipo both side, good and bad things are inherited
 
Baba yangu ni wa Kwanza kwao na alifika form 6.... Akapata kazi wakati wa MWINYI

Mimi wa Kwanza kwa Baba yangu nikafika chuo....Sijapata kazi mpk sasa.


Ila MIZIMU ya ukoo imeniambia nikitaka kutoboa nisifanye kazi wala kuajiriwa wamenipa UGANGA wao watanipa UTAJIRI kupitia watu.


KOO zetu zina Siri kubwa sana

Elimu haijakukomboa uganga ni utapeli na kuibia watu
 
🤣
Genetics ni biological pesa au utajiri ni physical hivi vitu viwili haviingiliani, labda uunganishe na uchawi.........huwezi kuchunguza genetics za umasikini kwenye biological laboratory
Hahahah nimezungumzia swala la Ridhiwani kurithi falsafa za baba yake. Hio ni genetically mtu anatoka nazo kwa mzazi.

Ila kuhusu mtonyo ni swala la miundombinu tu.
 
Ukiniuliza umaskini wangu ni kwanini nitailaumu serikali tu kwa sababu haijanitendea haki.😀

Serikali za watu wanaojielewa hamna umaskini kabisa kiasi kwamba maisha yako level. Unakaa kama average joe ama unakaza ili uwe tajiri.
 
Back
Top Bottom