Wenzetu mmewezaje kuvunja 'cycle' ya umasikini wa ukoo/familia?

Wenzetu mmewezaje kuvunja 'cycle' ya umasikini wa ukoo/familia?

Kuwepo kwa masikini na matajiri ndio kuna ifanya Dunia kua hivi ilivyo,ndio maana Mungu anasisitiza kua unapobarikiwa kipato usisahau kuwasaidia masikini coz alijua masikini watakuwepo,hatuwezi kua wote matajiri au wote masikini,

Kuutokomeza umasikini ni mwenye nacho kumsaidia asiye nacho kama Mungu alivyo sisitiza,ukiwa na uwezo na ukakutana na masikini,toa hicho kidogo ulichonacho umsaidie nae apate mahitaji japo kidogo,kila mtu akiwa na moyo wa kusaidia basi tutapunguza sana hili tatizo la kua na watu ambao hawamudu hata kununua chakula,

Utajiri ni mtihani na umasikini ni mtihani pia,maisha yanahitaji nidhamu ya hali ya juu sana,Binadamu wote ni ndugu na hii Dunia tunapita tu,ukibarikiwa usisahau kuwasaidia wenye uhitaji,maisha ni fumbo.
🙏
 
Ila mwenye dhana kuu ya umasikini Nini? Kwenye Uzi wako fafanua istilahi ili kila mtu akuelewe, vicious poverty circle according to Nurkse
 
Kuwepo kwa masikini na matajiri ndio kuna ifanya Dunia kua hivi ilivyo,ndio maana Mungu anasisitiza kua unapobarikiwa kipato usisahau kuwasaidia masikini coz alijua masikini watakuwepo,hatuwezi kua wote matajiri au wote masikini,
Sawa ila mbona huku kwetu hali ni mbaya sana kwani Ulaya na America waliwezaje kule maskini sio wengi kama kwetu Afrika.

Mimi naona sababu za kimazingira ndio zinaathiri pakubwa mno mitindo ya maisha ya watu.

Mfano kabla ya kuchangamana na mataifa mengine hatukuwa tukijiona masikini ila baada ya kuchangamana na mataifa ya Ulaya automatic tulijiona tupo nyuma na ni masikini vibaya sana.
 
Sawa ila mbona huku kwetu hali ni mbaya sana kwani ulaya na america waliwezaje kule maskini sio wengi km kwetu africa.

Mimi naona sababu za kimazingira ndio zinaathiri pakubwa mno mitindo ya maisha ya watu.

Mfano kabla ya kuchangaman na mataifa mengine hatukuwa tukijiona masikini ila baada ya kuchangamana na mataifa ya ulaya automatic tulijiona tupo nyuma na ni masikini vibaya sana.
Ulaya kuna umasikini mkubwa sana ila viwango hutofautiana na uko kwetu, kwao Serikali inatoa dole money kila mwezi kwa wale masikini kupata basic kama chakula na nguo, uku kwetu tuna umasikini wa kipato na wa akili ya viongozi wetu, hamna watu wenye roho ya kimasikini kama viongozi wa Africa.
 
Kuwepo kwa masikini na matajiri ndio kuna ifanya Dunia kua hivi ilivyo,ndio maana Mungu anasisitiza kua unapobarikiwa kipato usisahau kuwasaidia masikini coz alijua masikini watakuwepo,hatuwezi kua wote matajiri au wote masikini,

Kuutokomeza umasikini ni mwenye nacho kumsaidia asiye nacho kama Mungu alivyo sisitiza,ukiwa na uwezo na ukakutana na masikini,toa hicho kidogo ulichonacho umsaidie nae apate mahitaji japo kidogo,kila mtu akiwa na moyo wa kusaidia basi tutapunguza sana hili tatizo la kua na watu ambao hawamudu hata kununua chakula,

Utajiri ni mtihani na umasikini ni mtihani pia,maisha yanahitaji nidhamu ya hali ya juu sana,Binadamu wote ni ndugu na hii Dunia tunapita tu,ukibarikiwa usisahau kuwasaidia wenye uhitaji,maisha ni fumbo.
Asante sana brother, nimeichukua hii kuliko comment zote.
 
Ulaya kuna umasikini mkubwa sana ila viwango hutofautiana na uko kwetu, kwao serikali inatoa dole money kila mwezi kwa wale masikini kupata basic kama chakula na nguo, uku kwetu tuna umasikini wa kipato na wa akili ya viongozi wetu, hamna watu wenye roho ya kimasikini kama viongozi wa Africa.
Basi itoshe kusema chanzo kikubwa cha ufukara kwenye mafamilia yetu ni viongozi wetu.

Km ilivyo tabia ya baadhi ya ndugu pindi wanapofanikiwa utaka kujiinua na kuonekana wao tu ndio wa maana ndio ilivyo kwa viongozi wetu ni watu wenye roho za kimasikini sana.
 
  • Kuna familia na Koo zipo hakuna aliyemaliza form 4 wote elimu iliwashinda.
  • Kuna familia na Koo mmoja tu kafanikiwa kufika chuo na kumaliza ila kazi hana.
  • Kuna familia na Koo ndio unakuta masikini wa kukufulu, mabint wote wamezalia nyumbani, hakuna aliyeolewa na vijana nao wote wameleta wake zao nyumbani. Hakuna hata mwenye afadhali ya maisha.
Nyumba ukiingia tu inanuka njaa. Wewe ndio umebahatika kupata vijihela, lakini hela yenyewe haikai unaenda unajikuta unarudi pale pale; ile circle ya umasikini haivunjiki.

Wenzangu mnafanyaje mliozaliwa kwenye umasikini?

View attachment 2493306
Picha kutoka maktaba
Umaskini ni zawadi mkuu ukiona ukoonuna umasikini wa kutisha angalia matendo yao na jinsi wanavyofikiri hakuna dhambi hawajawai fanya nk
 
Tatizo hata sio laana, tatizo kubwa ni fikra, Afrika kuendea ni ngumu sana sababu ya kwenda nje ya muda. Unaweza kuoanga bajeti yako nyumbani iko fix kabisa unatembelewa na wageni bila taarifa hapo inabidi ushikamane na bajeti yako waliokuja bila taarifa wasivuruge bajeti yako, kwa hiyo kama ukiweza kukomaa na hilo utaona mabadiliko.

Pia msingi ni mbovu, mtoto amezalia nyumbani mzazi mwenye akili lazma achukue hatua kali bila kujali matokeo, kama utamwacha mtoto anayefuata atajifunza nini toka kwa dadake? Bila shaka ataona ni jambo la kawaida. Kwa hiyo kizazi kitaharibika. Lazma ukate ule uchafu na kuutupa ili uache usafi usonge mbele
 
Basi itoshe kusema chanzo kikubwa cha ufukara kwenye mafamilia yetu ni viongozi wetu.

Km ilivyo tabia ya baadhi ya ndugu pindi wanapofanikiwa utaka kujiinua na kuonekana wao tu ndio wa maana ndio ilivyo kwa viongozi wetu ni watu wenye roho za kimasikini sana.
Hili nalo pia ni tatizo katika familia nyingi,

Unakuta mtu mmoja kafanikiwa kwenye maisha katika familia yao,na anaona ufahari sana pale ndugu wanapokuja kumlilia shida nae huwasaidia,na anatamani maisha yawe hivyo hivyo,yaani anatamani miaka yote wenzake wawe chini yake tu ili waendelee kumlilia shida,hujiona ni kama mfalme fulani hivi,sasa mtu kama huyu akianguka ghafla kiuchumi,familia/Ukoo wote wanapata tabu,

Unapobarikiwa,jaribu kuwainua na wengine hasa watu wako wa karibu,ili kama mmoja wenu ataanguka kiuchumi basi wawepo na wengine ambao watamuinua na mwenzao tena,hili linafanyika sana kwa baadhi ya jamii za Waarabu na Wahindi,

Kitu muhimu ndani ya Koo ni lazima kuwe na upendo,kuheshimiana,kuaminiana....na hizi good discipline and attitude haziji ghafla au kimiujiza,hujengwa katika malezi tangu utotoni.
 
Tatizo hata sio laana, tatizo kubwa ni fikra, Afrika kuendea ni ngumu sana sababu ya kwenda nje ya muda. Unaweza kuoanga bajeti yako nyumbani iko fix kabisa unatembelewa na wageni bila taarifa hapo inabidi ushikamane na bajeti yako waliokuja bila taarifa wasivuruge bajeti yako, kwa hiyo kama ukiweza kukomaa na hilo utaona mabadiliko.

Pia msingi ni mbovu, mtoto amezalia nyumbani mzazi mwenye akili lazma achukue hatua kali bila kujali matokeo, kama utamwacha mtoto anayefuata atajifunza nini toka kwa dadake? Bila shaka ataona ni jambo la kawaida. Kwa hiyo kizazi kitaharibika. Lazma ukate ule uchafu na kuutupa ili uache usafi usonge mbele
Mkuu kumpa mtu chakula akala haliwezi kukusababishia umasikini, acha uchoyo. Baba zetu siku ya ijuuma walikuwa wanaalika kijiji kizima kuja kula nyumbani ila pesa na rizki ziliongezeka tu. Kuliko sisi tunao jifungia ndani kwenye gate
 
Mkuu kumpa mtu chakula akala aliwezi kukusababishia umasikini, acha uchoyo. Baba zetu siku ya ijuuma walikua wanaalika kijiji kizima kuja kula nyumbani ila pesa na rizki ziliongezeka tu. Kuliko sisi tunao jifungia ndani kwenye gate
Baba zako walikuwa na mashamba na mifugo, je wewe umewaiga? Tupo wa3 nyumbani unga ½ unatosha wanakuja wengine wa3 utatosha? Kama ulikuwa na akiba yako hujatoa hapo? Maendeleo utayasikia kwa wengine. Wazungu ndio maana wanaonekana mabepari sababu hawana mambo ya kijinga kuahirisha mambo
 
Mkuu mimi na kupinga umasikini ni man made hauna uhusiano wowote na uumbaji au kiroho, hayo yote ni visingizio vya wale walioshinda kupambanua udhaifu wao na kuishia kumsingizia Mungu.......wa kuristo wa kimißsionary ndo walioanzisha hiyo theory ya kusema umasikini unatoka kwa Mungu, na masikini amebarikiwa kwake ataenda mbinguni, hizo kauli zilitumiwa na hao watu ili exploit mali za waafrika na kutengeneza utii kwa wafasi wao masikini, we can fight and eradicate poverty.
IMG_20230123_233454_265.jpg
 
Anzisha ukoo wako. Yaani jihesabu wewe na mke wako kama ndio unaanza ukoo mpya, usijiassociate na mambo ya kiukoo yasiyo na maana.

Tengeneza value na system yako mpya warithishe na watoto
kwenye ukoo au familia kubwa mnakutana kwenye mambo yale muhimu tu; mfano misiba, sherehe nk, mambo ya kupika pamoja, kutunza watoto wa dada au kaka zako au kuwasomesha sahau, hapa mzunguko wa umasikini hautavunjika. Wengine watarelax mmoja mwenye afadhali utazidi kuumia. tunza familia yako vizuri wengine wakuige na kukuomba ushauri!
 
Hakuna uhusiano kati ya umasikini na Genetics or Race,umasikini unasababishwa na man made,kuanzia life style,bad discipline and attitude,kutokujali muda,kutokua na mipango,kutokujiwekea akiba,kuvamia kazi au biashara ambayo hujaifanyia research,kuiga kwa kuona fulani kafanikiwa kwa kufanya jambo fulani huku ukiwa hujui amepitia njia zipi mpaka kufika hapo alipo,kukata tamaa na mengineyo,

Life is one Big road with lots of sign,So when you riding through the ruts,don't complicate your mind,flee from hate,mischief and jealousy,put ur vision to reality.
 
Back
Top Bottom