Wenzetu waanza kupewa kadi za kuthibitisha wamepata chanjo ya Corona kama Jumuiya ya Kimataifa inavyoelekeza

Nchi inahitaji kumpata Abigaili (1Sam 25: 3ff) kwani Nabali kakosi kibali cha Ukuu na mauti inamsubiri !!
 
Hii ndiyo tofauti kati ya nchi zenye Marais wenye weledi na nchi yenye Rais mataputapu.Imagine wewe ni mfanyabiashara wa kimataifa halafu unakumbuna na hili!
Haya ndo madhara ya kuongozwa na "Juha" , Mshamba, Mburula nk..

Kwahali ilipofikia ni lazima akubali tu chanjo, ila anaona AIBU araanzaje? Anapaswa kukumbuka kuwa "mtu mzima ukikutwa uchi ni lazima uchutame" .....
 
Watakuwa wanakuja Kwetu maana Kwao hatuta kwenda?!
 
Tukiachana na ushabiki... Kwenye hili la chanjo, ninachokiona mimi ni MAJARIBIO YA CHANJO
 
Kibongobongo hiyo kadi mbona inafojika vizuri tu!!
CCM kwa uwezo wa wizi wa kura, na fojali ya chaguzi ni Kweli wanaweza foji Kadi HIZO na hata kupora kama walivyopora oktoba last year !
 
Hatari yake nini ?
hatari yake ni kwamba bado ni chanjo za majaribio, hakuna uhakika juu ya chanjo hizi ndio maana hata baadhi ya mataifa yaliyo tengeneza chanjo hizi kama vile Ujerumani, ufaransa na hata Marekani yenyewe bado wanamalumbano makali sana juu ya uhakika wa chanjo hizi ipi inafaa ipi haifai, bado ni majadala,
, sembuse kwa sisi ulimwengu wa tatu!!! kuwa makini
 
Ni wapi shehe Ponda na shura ya maimamu wamepinga chanjo?
 
Tuendelee kusali na kutubu madhambi yetu bhandugu! Yanatengenezwa mazingira ya Chapa ile iliyozungumziwa, badae tutaambiwa kadi zinapotea kwahiyo inabidi chapa ipigwe mkononi au kwenye vipaja vya uso😁😁 keep praying 🙏 kujifukiza ni mhimu sanaaaa.

HATUTAKI CHANJOOOOO
 
Nimependa hapo kwenye haya maandishi...
"Enjoy Life, Protect Yourself"


NB: Nyie msiopenda kuenjoy life mtasubiri sana.
 
Dikteta sijui kwanini anakataa na wakati ni hiari ya mtu

Utafika wakati serikali itabidi ikubali WHO walete chanjo na wao wenyewe wasimamie utaratibu wa kuzisambaza wakati serikali ikiona aibu kukubali kuhusishwa na chanjo hizo!! Serikali itabidi ijifanye hamnazo wakati wananchi wanapatiwa chanjo!

Serikali ikiendelea na upuuzi wa kukataa kuleta chanjo ,wananchi wengi itabidi wazifuate nchi jirani ambako itabidi waingie gharama kubwa ili kuhudumiwa!!! Wananchi wakianza kwenda nchi za nje kufuata chanjo uchumi wa nchi utatetereka kwani resources will be drained out of the country!!!
 
Mkuu anaweza kuwatengenezea mecca yao hapa hapa bongo ili wahiji na pia kuleta fedha za kigeni maana sisi ni nchi tajiriiii.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…