WFP mmeanza lini uswahili?

Boeing787-8

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2018
Posts
1,155
Reaction score
1,209
Hi wakuu.

Niliomba kazi kwenye hili shirika la kimataifa, nashukuru walini shortlist. Nilipiga interview ya kwanza nkafahulu

Niliitwa Kwa second interview nkapiga nayo majibu yakaja nime be selected Kwa third interview.

Nilipiga third interview, mwisho wakasema watanipa feedback after few couple of days


Sasa mwezi na wiki umepita, no feedback,,,nilijua Hawa WFP watakuwa hawana uswahili kumbe nilikosea.

How come mtu afanye multiple rounds of interview afu msimpe majibu?


Wakuu hii ni sawa?
 
Mwezi mmoja tu unatoka public kuanza kulalamika? Watu wapo busy ku run background check zenu. Wakati mwingine wanaochelewesha ni hao referees wako.
Kuwa mvumilivu. Mpaka kuitwa inaweza ikachukua hadi miezi sita. Na wakiona haya malalamiko huenda wakaipiga chini batch yenu waka shortlist wengine.
 
Background check kwani tumekuwa magaidi?
 
Mmm oky
 
Duu kumbe mpaka referees wanakuwa contacted
 
Dogo, Mimi ndio yule interviewer wa WFP. Ilikuwa majibu yatoke kesho ila umekuja kutusimanga huku jamvini. Huna uvumilivu kabisa dogo, nimekwazika sana na hiki kitendo. Jina lako nalifyeka sasa hivi hapa kwenye laptopu
 
Duu kumbe mpaka referees wanakuwa contacted
Katika kazi nyingi za kimataifa referees ni watu wa muhimu sana. Na wakati mwingine inabidi wawatafute na kuongea nao ana kwa ana kukuhusu wewe.

Kuna mwanafunzi wangu mmoja nilimwandikia recommendation letter nikawa nimesahau. Siku moja pisi ya kizungu inanitafuta inataka tuonane. Kumbe inataka first hand info kumhusu huyo dogo. Ubaya sasa dogo nikawa hata simkumbuki vizuri. Ilibidi nimtafute na kumwambia anitumie bio yake haraka sana. Itoshe tu kusema kuwa dogo alipata ile kazi na sasa anabadilisha BMW na Audi tu...wakati mi hata baisikeli sina dah! 😬

Zingatieni sana referees hasa katika kazi za kimataifa ambako kidogo kuna unafuu katika suala zima la nepotism na connections...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…