What is energy in spirituality

What is energy in spirituality

Nikijua kitu sihitaji tena kuamini, hakuna mtu anamnyima mtu kuamini ni haki ya kila mmoja ila ukisema spiritual ipo nitahitaji uthibitisho, kama ni kulala nimesha lala mara nyingi nakuamka angalau hilo jambo ninauzoefu nalo wala sihitaji kuaminishwa.
Kwahiyo wewe unajua(sio kuamini) kwamba ukilala lazima kesho utaamka hai?
 
Nipo sawa japo hukunielewa, kujua ni matokeo ya kuziamini abstract idea, hivo hakuna kujua bila kuamini.
Ila kuna kuamani pasipo kujua?🤣 sasa baada ya Kuamini spiritual nataka kuthibitisha uwepo wake ili nisihitaji kuamini tu kitu ambacho mimi sikitaki.
 
Kwahiyo wewe unajua(sio kuamini) kwamba ukilala lazima kesho utaamka hai?
Unaongelea spiritual au una ongelea kulala na kuamka?kwa sababu hiyo kulala nakuamka nimesha ithibitisha mara kadhaa kwamba nimelala na nimeamka , uthibitisho wa imani ya hivyo tayari ninayo , naomba uthibitisho wa spiritual au Hicho kinachoitwa uwepo wa Mungu 🤔
 
Unaongelea spiritual au una ongelea kulala na kuamka?kwa sababu hiyo kulala nakuamka nimesha ithibitisha mara kadhaa kwamba nimelala na nimeamka , uthibitisho wa imani ya hivyo tayari ninayo , naomba uthibitisho wa spiritual au Hicho kinachoitwa uwepo wa Mungu 🤔
Mimi naongelea kuamini, kujua na uthibitisho.

Umesema ukijua kitu hauhitaji kuamini ndio maana nikakuuliza wewe ukilala unajua(sio kuamini) kuwa kesho utaamka?
 
Mimi naongelea kuamini, kujua na uthibitisho.

Umesema ukijua kitu hauhitaji kuamini ndio maana nikakuuliza wewe ukilala unajua(sio kuamini) kuwa kesho utaamka?
Nimelala kwa imani na tayari nimethibitisha umuhimu wa kulala kwa kulala na kuamka , kwa hiyo sihitaji tena imani ya umuhimu wa usingizi kwa sababu nimeshathibitisha umuhimu wa kulala .

Ukija kwenye suala la mada iliyopo mezani kulala na spiritual ni vitu viwili tofauti kiimani .

Kulala na kuamka ni tendo lililothibitika tayari hata mimi kila siku nalithibitisha mwenyewe tu.

Je spiritual japo ni imani inathibitika vip?


Imani ya kulala na kuamka tayari hiyo kila mtu anayo experience nayo na imeshathibitika , kwamba alilala akaamka .

Sasa nahitaji uthibitisho wa imani ya spiritual kama ambavyo niliamini nimelala na kuamka na kweli nikathibitisha hilo .
 
sasa baada ya Kuamini spiritual nataka kuthibitisha uwepo wake ili nisihitaji kuamini tu kitu ambacho mimi sikitaki.
Uthibitisho wa maandiko daily tunawapa mnaukataa, hata wa deities experience ktk jamii za dunia kabla ya kufahamiana na kuchangamana pia mnaukataa.

Chakushangaza, daily mnatueleza kila mtu alizaliwa atheist hadi pale wazazi/jamii itakapombadilisha, je ushawahi jiuliza, kama kila mtu huzaliwa atheist toka mwanzo, ni nani mwanzilishi wa hadithi za uwepo wa deities na alizitoa wapi??
 
Mimi naongelea kuamini, kujua na uthibitisho.

Umesema ukijua kitu hauhitaji kuamini ndio maana nikakuuliza wewe ukilala unajua(sio kuamini) kuwa kesho utaamka?
Kwa mfano mwingine nina amini nina panda gari au ndege nitafika safari yangu , na kweli nimepanda gari nimefika hapo imani yangu imethibitika .

Nisipofika imani yangu haijathibitika.

Unaposema kiroho kwa nini ni imani tu bila mchakato wa kuthibitisha hiyo imani ni kwel au sio kwel?
 
Uthibitisho wa maandiko daily tunawapa mnaukataa, hata wa deities experience ktk jamii za dunia kabla ya kufahamiana na kuchangamana pia mnaukataa.

Chakushangaza, daily mnatueleza kila mtu alizaliwa atheist hadi pale wazazi/jamii itakapombadilisha, je ushawahi jiuliza, kama kila mtu huzaliwa atheist toka mwanzo, ni nani mwanzilishi wa hadithi za uwepo wa deities na alizitoa wapi??
Ulishawahi kusoma au kusikia hadithi za gilgamesh?
 
There is nothing called spiritual form of Energy in this Universe.

If it is, Then where did it originated or came from?
 
Nimelala kwa imani na tayari nimethibitisha umuhimu wa kulala kwa kulala na kuamka , kwa hiyo sihitaji tena imani ya umuhimu wa usingizi kwa sababu nimeshathibitisha umuhimu wa kulala .

Ukija kwenye suala la mada iliyopo mezani kulala na spiritual ni vitu viwili tofauti kiimani .

Kulala na kuamka ni tendo lililothibitika tayari hata mimi kila siku nalithibitisha mwenyewe tu.

Je spiritual japo ni imani inathibitika vip?


Imani ya kulala na kuamka tayari hiyo kila mtu anayo experience nayo na imeshathibitika , kwamba alilala akaamka .

Sasa nahitaji uthibitisho wa imani ya spiritual kama ambavyo niliamini nimelala na kuamka na kweli nikathibitisha hilo .
Mkuu kuna watu wengi tu ni marehemu sasa hivi ambao walilala na kuamini wataamka kesho yake ila wakafa, sasa hapo utasemaje imani ya kulala na kuamka imethibitika? Point ni kwamba hakuna mwenye kulala na kujua kesho lazima ataamka, na hapo ndipo imani inapokuja na umuhimu wake.
 
There is nothing called spiritual form of Energy in this Universe.

If it is, Then where did it originated or came from?

Mkuu kuna watu wengi tu ni marehemu sasa hivi ambao walilala na kuamini wataamka kesho yake ila wakafa, sasa hapo utasemaje imani ya kulala na kuamka imethibitika? Point ni kwamba hakuna mwenye kulala na kujua kesho lazima ataamka, na hapo ndipo imani inapokuja na umuhimu wake.
Ila kuna wenye kulala kwa imani na kuthibitisha kuwa wameamka , sasa mimi ninachokitaka ni mtu atoe huo uthibitisho wa mchakato wa kuthibitisha, hiyo spiritual kama ambavyo tumeweza kuthibitisha imani ya kulala halafu tukaamka
 
Ila kuna wenye kulala kwa imani na kuthibitisha kuwa wameamka , sasa mimi ninacglhokitaka ni mtu atoe huo uthibitisho wa mchakato wa kuthibitisha, hiyo spiritual kama ambavyo tumeweza kuthibitisha imani ya kulala halafu tukaamka
Imani kila mtu anayo mkuu, Tatizo ni kwamba Inapozungumziwa Imani inakua based kwenye dini.

Mimi sina dini ila nina Imani, Mfano:

•Hapa ninachati nawewe nikiamini utajibu hii quote wakati sijui kama utakufa au nitakufa dakika 1 mbele kabla hujajibu, Au huenda labda dakika 2 mbele JF itafungiwa lakini bado naitumia, hii ni Imani.

•Ninamalengo ya siku, wiki na Mwaka, Tena kila siku ninajiambia lazima siku fulani nifanye kitu fulani bila kuwaza kwamba huenda nikawa nimekufa, hii ni Imani.

•Napanda basi kuelekea mkoa X nikiamini nitafika, hii ni Imani.

•Ninaelekea mahali X may be sokoni huku nikiamini nitafika na nitapata ninachokitaka hii pia ni Imani.

•Mimi ninafanya Body workout, ninakula balance diet na kufanya mazoezi kwa bidii nikiamini vitaniletea matokeo, hii pia ni Imani.

Kabla hatujaendelea, Kwa uelewa wako Imani ni nini?
 
Kwa mfano mwingine nina amini nina panda gari au ndege nitafika safari yangu , na kweli nimepanda gari nimefika hapo imani yangu imethibitika .

Nisipofika imani yangu haijathibitika.

Unaposema kiroho kwa nini ni imani tu bila mchakato wa kuthibitisha hiyo imani ni kwel au sio kwel?
Wanaopanda gari na kuamini watafika safari zao kama wewe ni wengi ila sio wote wanafika, sasa kwa hao ambao hawakufika imani zao vp kwamba sio za kweli?
 
Imani kila mtu anayo mkuu, Tatizo ni kwamba Inapozungumziwa Imani inakua based kwenye dini.

Mimi sina dini ila nina Imani, Mfano:

•Hapa ninachati nawewe nikiamini utajibu hii quote wakati sijui kama utakufa au nitakufa dakika 1 mbele kabla hujajibu, Au huenda labda dakika 2 mbele JF itafungiwa lakini bado naitumia, hii ni Imani.

•Ninamalengo ya siku, wiki na Mwaka, Tena kila siku ninajiambia lazima siku fulani nifanye kitu fulani bila kuwaza kwamba huenda nikawa nimekufa, hii ni Imani.

•Napanda basi kuelekea mkoa X nikiamini nitafika, hii ni Imani.

•Ninaelekea mahali X may be sokoni huku nikiamini nitafika na nitapata ninachokitaka hii pia ni Imani.

•Mimi ninafanya Body workout, ninakula balance diet na kufanya mazoezi kwa bidii nikiamini vitaniletea matokeo, hii pia ni Imani.

Kabla hatujaendelea, Kwa uelewa wako Imani ni nini?
Imani yako ya Kuamini mimi nitakujibu tayari imethibitika baada ya mimi kukujibu , hauhitaji tena imani ya mimi kukujibu baada ya kuthibitisha kuwa nimeshakujibu labda kwa quote nyingine .
 
Wanaopanda gari na kuamini watafika safari zao kama wewe ni wengi ila sio wote wanafika, sasa kwa hao ambao hawakufika imani zao vp kwamba sio za kweli?
Waliofika imethibitika wamefika ambao hawakufika pia imethibitika hawakufika, kwa hiyo hiyo imani kwa pande zote mbili imethibitika.
 
Ila kuna wenye kulala kwa imani na kuthibitisha kuwa wameamka , sasa mimi ninachokitaka ni mtu atoe huo uthibitisho wa mchakato wa kuthibitisha, hiyo spiritual kama ambavyo tumeweza kuthibitisha imani ya kulala halafu tukaamka
Huko kulala na kuamka sio uthibitisho ni sawa na mtu ambaye anakwambia amepata kitu fulani kutokana na sala na maombi aliyofanya. Wote tunajua wapo waliyolala na kuamini watamka ila hawakuamka.
 
Huko kulala na kuamka sio uthibitisho ni sawa na mtu ambaye anakwambia amepata kitu fulani kutokana na sala na maombi aliyofanya. Wote tunajua wapo waliyolala na kuamini watamka ila hawakuamka.
Pia kutokuamka kwao ni uthibitisho kuwa unaweza kulala pia usiamke.
 
Imani yako ya Kuamini mimi nitakujibu tayari imethibitika baada ya mimi kukujibu , hauhitaji tena imani ya mimi kukujibu baada ya kuthibitisha kuwa nimeshakujibu labda kwa quote nyingine .
Tuko pamoja mkuu!!

Uko wapi agiza chochote nitalipa kwa simu.
 
Back
Top Bottom