What is Wrong with Tanzania?!. Tunashindwa Nini Kufikisha Bidhaa Zetu Kwenye Masoko ya Kimataifa?!.

What is Wrong with Tanzania?!. Tunashindwa Nini Kufikisha Bidhaa Zetu Kwenye Masoko ya Kimataifa?!.

Uko sahihi kabisa tumefeli kwenye eneo hili mfano halisi niliwahi kuomba BET wakati huo nafasi ya kwenda kwenye exhibition ya kazi za mikono Osaka Japan nafasi ambayo serikali ya Japan imewapa bure bileshi Tanzania ili isaidie wafanyabiashara wadogo wa Sanaa za mikono lkn baada ya kupata nafasi hiyo nilitakiwa nilipe ada ya ushiriki(participation fee) niwe na mzigo wa kuonyesha na kuuza niwe na nauli pesa ya kula pesa ya usafiri wa mzigo kutoka Tanzania mpk Japan pesa ya kutolea mzigo Japan hizo pesa zilikuwa nyingi kwa mfanyabiashara mdogo kumudu hivyo nilishindwa.

Lkn nafasi kama hiyo hiyo ukiomba south Africa unalipiwa nauli na serikali yao freight charges pesa ya kula na gharama ya kurudisha mzigo kama ukibaki kwenye show. Hapo unaona kabisa mfanyabiashara wa tz ataendelea kudoda wa south anapeta kwani gharama yake ni kununua mzigo tu.
Mkuu huu ndio wakati wa kumatafuta Paskali unamuelezea tukio zima ulivyopata fursa na kushindwa kwenda, kisha yeye anaandika kwa ufundi ktk gazeti na mitandaoni huku ukishauri na kitu cha kufanya ukitolea mifano yenye ushahidi wa nchi hizo kama SA nina uhakika serikali hii watasoma na kufuata ushauri wako. Haya ndiyo Mh. JPM anataka yashauriwe na yaandikwe ktk media na mitandaoni, hata Mh. Mkapa majuzi kaongea ktk mahojiano na media za nje. CC: Pascal Mayalla
 
Bidhaa nyingi za Tanzania ni feki na siyo imara ukilinganisha na bidhaa za kutoka mataifa mengine.
Mkuu naomba kujua uimara na uhalisia wa korosho na tanzanite za India na Kenya kisha na ubandia au kutokuwa imara kwa bidhaa hizo toka TZ.
 
Wanabodi,

Tanzania kama nchi, tunakabiliwa na tatizo kubwa la Wafanyabiashra wa Tanzania, kushindwa kuingiza bidhaa zetu kwenye masoko ya kimataifa!, tatizo ni nini?!.

Mifano.
Tanzania ndiye mzalishaji pekee wa madini ya Tanzanite, lakini katika masoko ya kimataifa, nchi inayoongoza kwa kuuza Tanzanite ni India, ikifuatiwa na Afrika Kusini, Lebanon, Kenya halafu ndio sisi wenye Tanzanite zetu. Kwa vile Tanzanite inapatikana Tanzania pekee, data za export market ni zile za cut and polished stones, hii inamaanisha ni Tanzanite nyingi inachimbwa na kuuzwa un cut kuliko ile tunaicharanga wenyewe!.

Tanzania iko kwenye top ten wazalishaji wa korosho. Mnunuzi mkuu wa Korossho ya Tanzania ni India akifuatiwa na Kenya, lakini kwenye urari wa soko la processed nuts, Kenya ana export korosho nyingi zaidi sokoni kuliko Tanzania, huku sisi tukiuza korosho isiyobanguliwa!.

Kwenye nchi za Afrika Mashariki, Kenya ndio inaongoza kwa kuuza vinyago ulaya, na hakuna nchonga vinyago Kenya, vyote wananunua kutoka Tanzania, Kenye ndiye muuzaji mkuu wa unga wa sembe kwenye masoko ya ulaya, lakini mahindi yote wananunua kutoka Tanzania!.

Kwenye fursa za AGOA, Watanzania tumeshindwa kuchangamkia hiyo fursa!, Wakenya wanakuja Tanzania, wananunua bidhaa, na kupeleka Kenya, kule wana process na packing na branding, then zinaingia masoko ya kimataifa as products of Kenya!. What is wrong with sisi Watanzania?!.

Katika kusaidia kwenye hili, Taasisi ya Trademark East Africa, inajaribukutusaidia!.
MICHUZI BLOG: Taasisi ya TradeMark East Africa (TMEA) yazijengea Uwezo bidhaa za Tanzania kuingia masoko ya kimataifa.

MATUKIO @ MICHUZI BLOG: Taasisi ya TradeMark East Africa (TMEA) yazijengea Uwezo bidhaa za Tanzania kuingia masoko ya kimataifa.

Paskali
Tutaanza hivi mapema maana tuna hii serikali yetu ya viwanda. Mayala=njaa
 
Hizo Tanzanite India inayoongoza kuuza, na Afrika ya Kusini, wanazipata wapi?!. Hivyo vinyago hao Wakenya wanavipata wapi?!. Hayo Mahindi jee?.

Paskali

Kwenye issue ya Madini tumepoteza mwelekeo na tulishindwa kujipanga, madini hayauzwi kama karanga, bali madini ni issue ya kitaifa, so lazima kungekuwa na kitengo maalumu cha kusimamia hayo mambo ya Madini ya yote na hata Mambo ya Nishati-mafuta, gas, Makaa nk pia

Amini usiamini unaweza kuona mtu katoka Rwanda au Kenya anakuja kununua dhahabu Tanzania na sisi tukaona ni mfanyabiashara Mkubwa sana na hata akikualika Kigali au Nairobi utamuona ti mfanyabiashara hasa na anaishi sehemu ya maana, lakini nyuma ya pazia ni taasisi, sio mali yake bali mali ya taifa
We hujiulizi inakuwaje nchi kama. Rwanda isiyo na Resource, viwanda wala kilimo cha maana lakini wanauwezo wa kununu madege ambayo hata Tanzania na kila kitu hatuwezi?
 
Mkuu mimi ninachofahamu, kwanza sisi wenyewe hatuthamini vya kwetu. Hili tuliache kwanza.
Fikra zetu zikibadilika tutapiga hatua sana....navyoona hatuko mbali. Nyoka anauma kichwani....nikimaanisha anayeongoza kama naye anayasema haelewi kwanini hatusongi mbele basi hakuna namna
 
Bidhaa nyingi za Tanzania ni feki na siyo imara ukilinganisha na bidhaa za kutoka mataifa mengine.
Kwanini unaamini hivyo? Korosho upande n.a. kuvuna mwenyewe halafu kwako iwe fake mpaka iende India ndio itakuwa sawa? Kweli aliyeturoga amekufa na ulozi wake[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2]
 
Matangazo ya biashara atujitangazi mazee. Kama ujitangazi uwezi tusua hata kidogo.
Mfano mzuri kampuni kama KCB Bank [emoji542] na Fast Jet
Makampuni ya nje ya Tanzania yanajitangaza mpaka apa Jamii Forum
Na kampuni zetu za akina NMB bank [emoji542] na Tanapa wanasubiria wapigiwe chapuo na serikali, ili wapate tender na wateja
Poor marketing and poor customer care
Mimi nashindwa kuelewa sehemu kama TRA, TPA na makampuni ya usafirishaji ayajitangazi yanafanya biashara kizamani sana.

Tanapa walitakiwa wachuane na TBL na TCC kwenye marketing lakini wapo kimiya, mtaliii gani atakuja ujitangazi

Wenzetu manyang'au ya Kenya yanajitangaza sana kuhusu Mlima Kilimanjaro na wanapata watalii wengi sana na kutuzidi sisi
 
Integrated Grain Storage and Electronic Commodity Exchange Market inafahamika?
 
Jaribu kusoma hapa chini, kuna mdau alishaniuliza swali kama lako. Pia tanzanite zinapatikana Tanzania tu, hakuna tanzanite ya Kenya wala India.

Kipindi fulani haya madini yalikuwa yanapatikana sana kwenye hizo nchi kwa njia ya magendo. Lakini sasa hivi serikali imejitahidi kudhibiti, tatizo limebakia kwenye sera. Bado hatujaweza kufanikiwa kupata sera imara kwenye haya madini ya tanzanite.
Maziku,

Bahati mbaya sana hao watunga Sera ni walewale tangu miaka 50 iliyopita . . , CCM CCM CCM . .

Hatuwezi kutoka hapa kwenye mtanziko huu mpaka ccm kwanza ife . . , haiwezekani watu walewale (mindset) waliotuletea matatizo ndio watoe solution . . , tunahitaji akili kubwa zaidi . .
 
Tatzo kubwa ni swala la biashara Tumewaachia wahindi (Watanzania wenzetu wenye asili la bara asia ) na wao wametengeneza glass ceiling kwa wenzetu ....ila Mfumo wa ujamaa aukutengeneza MINDSET Ya ujasiliamli na ufanyabiashara kabisa hawa vijana wa 90's watabadirika kama unafatilia utaona kuna mabadiriko makubwa sana now we export at least kuliko zaman mtu anaingia kwenye biashara na kilimo baada Ya kufeli shule na kustaafu tu ...ila now vijana wanachukulia kilimo na biashara kama career Tupo pazur
 
samahani wakuu.nilikuwa nauliza jinsi gn unaweza kufanya ili upate kuonyesha biashara yako katika maonyesho ya sabasaba
 
samahani wakuu.nilikuwa nauliza jinsi gn unaweza kufanya ili upate kuonyesha biashara yako katika maonyesho ya sabasaba
Tembelea
tantrade.or.tz | Linking Production to Markets
Kisha pakua fomu hii.
http://tantrade.or.tz/sites/all/public_files/docs/Application Form _Kiswahili 2017.pdf

Ukifanikiwa kushiriki karibu unitembelee mimi huwa ni
Temporary office mule ndani kwa ajili ya kuyatangaza maonyesho.

Na kunawakati huwa natoa offers kama hizi.
Fursa Kwa Wajasiliamali wa JF. Karibu Ujitangaze Kupitia SABA SABA NA PPR Utokee Kwenye TV 5!. - Google Search


https://www.google.com/url?sa=t&sou...dmILMRwDeCs9YYxzw&sig2=WNTJMf8qsWDk8NHri-o7zA
P.
 
Back
Top Bottom