Whatsssssss!!!!!!!!!????

Mzee mmoja alimwandikia barua mjukuu wake aliyekuwa gerezani.
MJUKUU wangu,msimu huu ctoweza kupanda mahindi kwa kuwa cna nguvu ya kulima na wewe ambaye ungenisaidia upo gerezani.
MJUKUU wake kupata ile barua akamjibu BABU USITHUBUTU KULIMA LILE SHAMBA MAANA ZILE MIL 80 NILIZOIBA NIMEZIFUKIA HUMO SHAMBANI. mapolisi walipoisoma ile barua ikabidi waende kulitufua shamba lote,kumbe hakukuwa na zile pesa wala nin.
baada ya wiki mjukuu akamwandikia babu barua sasa unaweza kupanda mahindi hata kama niko mbali ninaweza kukusaidia babu. [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mama alipomaliza kupika chakula akamwambia mwanae ampigie simu baba yake ili aje ale.......
MTOTO: mama..mama, baba hapatikani bahna
MAMA: subir kama dk 5 hv halafu upge tena yawezakuwa network inasumbua.
Baada ya dakika 5
MTOTO: mama, simu inaita ila kapokea mwanamke
MAMA: Ahsante.... aya mwanangu kula chakula.
Baada ya dk 9 baba akagonga mlango .......ile kufunguliwa kakutana na kibao cha ulimi,....ajakaa poa kapokea sufuria la ubongo...... Hajajua sababu kala mwiko wa koromeo ......ile yupo chini anagalagala kwa maumivu kapewa kifuti cha roho
Ayaaaa.....majirani si wakajaa kuja kuamulia ugomvi?, wakakuta mshua wa watu kachakaa kama katoka vitani
MAMA: (huku akiwa amefura kwa hasira)..... yan we unaniacha nyumban unaenda kutanua na vimada halafu nakupgia cmu unawapa wapokee si dharau hizo, eti mwanangu, yule mwanamke alivyopokea simu alisemaje?
MTOTO: Eti alisema "simu ya mteja unayempigia haipatkani kwa sasa, tafadhali jaribu tena badae"
[emoji12][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Dogo mmoja zuzuzuzu flani hivi anaitwa KARIM alipelekwa kuanza form 1 shule moja Zanzibar huko, si ukafika mda wa kujtambulisha,
wa kwanza 'naitwa Lailat'
wa pili "naitwa Mulhat"
wa tatu "naitwa Naifat"
wa nne "naitwa Najat"
wa tano "naitwa Asnat"
Mwanangu si ikafika zamu ya kichaa wetu KARIM?
Haya mwenzetu mgeni kutoka bara waitwa nani..."naitwa KALIMATI" [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mwanamke Zuzu alikuwa na mchumba wake Zuzu, baadaye uhusiano ulivunjika. Zuzu mwanaume alikuwa akimsumbua sana kumpigia na kumtumia sms yule mwanamke Zuzu kila siku ili warudiane mpaka mwanamke Zuzu akawa anachukia.
Zuzu mwanamke akaamua abadili SimCard, alipoweka ile mpya tu akamtumia sms Zuzu mwanaume ''Nishabadilisha namba hutonipata tena hasidi wewe''..
yule Zuzu mwanaume akamjibu: "Nitahakikisha naitafuta hiyo namba yako mpya mpaka naipata [emoji12][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mwanamke Zuzu alikuwa na mchumba wake Zuzu, baadaye uhusiano ulivunjika. Zuzu mwanaume alikuwa akimsumbua sana kumpigia na kumtumia sms yule mwanamke Zuzu kila siku ili warudiane mpaka mwanamke Zuzu akawa anachukia.
Zuzu mwanamke akaamua abadili SimCard, alipoweka ile mpya tu akamtumia sms Zuzu mwanaume ''Nishabadilisha namba hutonipata tena hasidi wewe''..
yule Zuzu mwanaume akamjibu: "Nitahakikisha naitafuta hiyo namba yako mpya mpaka naipata [emoji12][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Masai na mwanajeshi walikuwa wanapgana yule masai akamrushia mwanajeshi mkuki.
Mwanajeshi kutokana na mazoezi ya kijeshi akaudaka ule mkuki na kuuchoma chini pemben ya miguu yake kisha akatoa bomu na kumrushia masai.
Yule masai akalidaka bomu nae kuonesha mbwembwe akalitupa chini ya miguu!! [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
MKAKA: Hi uwapi swity?
MDADA: Niko home
MKAKA: Unafanya nini?
MDADA: Nakula
MKAKA: Unakula nini?
MDADA: Mama katengeneza macaroni,
ambayo kanyunyizia chiizi na sausage fulani imported ambazo baba amenunua supermaketi Masaki, na saladi, kisha ntateremsha na Epo juisi,
ghafla ikasikika sauti ya mama yake
MAMA: Hivi we Gulo kaka yako atakula nini na we umemaliza ugali na maharage yote?[emoji12][emoji13][emoji13][emoji13]
 
Jamaa alipita sehemu
isiyoruhusiwa katika kambi ya jeshi na akapewa adhabu ya kuhamisha matofali 1000! Jamaa akajitahidi na akabeba matofali 900 na akawa hoi!
Ghafla akakumbuka kuwa mkuu wa kambi ni rafiki yake walisoma wote school, akampigia simu.
JAMAA: vijana wako wamenipa adhabu ya kuhamisha matofali 1000!
MKUU: hao wajinga kweli hawajui tunavyofahamiana!
wasikusumbue mimi ndiyo mkuu wao, zirudishe pale ulipozitoa mwanzo then uje ofisini tuonane. [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Tanzania - Witchcraft (Ushirikina)
 
JAMAA: I miss you
DEMU: Upo home beby nije?
JAMAA: nipo beby, wewe njoo tu utanikuta.
DEMU: poa nakuja beby utanilipia 10,000 ya Taxi
JAMAA: Ah nimekumbuka naenda kwenye kikao nitachelewa kurudi.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Yahaya kapata trip ya kikazi dodoma, kufika akaamua kumtafuta mpenzi wake wa UDOM ili apate pa kujificha. Kesho yake mrembo akamuomba amwazime laki 3, Yahaya akampa ATM kadi na Pin na kumwambia atumie vyovyote anavyotaka, kumbe ATM ina Tshs 5,000 tu. Kabla hajashtukiwa akapanda bus ili arudi Dar, njiani simu ikakata chaji akalala,
Kuamka asubuhi anakuta sms kutoka kwa boss wake ikisema Yahaya nimeweka milioni 10 kwenye akaunti namba yako, usirudi kwanza Dar mpaka uwalipe mafundi [emoji12][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mume na mke kila siku kushindana kwenye familia mpaka maisha yakawa kama yanaboa maana kila kitu kidogo lazima washindane. Mume aliudhika sana maana kila siku mke ndo anashinda.
Siku moja mume akaenda bar, akaanza kupiga stori na mshikaji wake, akamwambia bhana mimi kila kitu tukishindana mke wangu lazima anishinde, hebu nishauri nifanye kitu gani nimshinde??
Mshikaji akatoa idea kwamba ukirudi nyumbani, mwite mkeo nje, anzeni kukojoa kwenye ukuta wa nyumba halafu angalieni nani karusha mkojo juu zaidi ya mwenzake ukutani.
Mme aliporudi nyumbani akamwita mkewe zoezi la kukojoa ukutani likaendelea, mke akaanza, akawa kafikia mita mbili.
Ikafika zamu ya mume, ile anafungua zipu mke akamwambia, anza lakini hakuna kushika kwa mkono [emoji12][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
MTOTO:"Baba nimempenda Lucy mtoto wa jirani yetu nataka awe mpenzi wangu"
BABA:"Heri hata hujamtongoza huyo ni dada yako"
baada ya wiki
MTOTO:"Baba nimekutana na msichana mwingine"
BABA:"Nani huyo"
MTOTO:"Joyce mtoto wa jirani wa pili"
BABA:"Haiwezekani huyo pia ni dada yako ila usimwambie mamako"
mtoto akawa na huzuni mama yake akamuona na kumuuliza
MAMA:"Tatizo ni nini mwanangu?"
MTOTO:"Nimependa wasichana wa jirani zetu kama sita ila baba amekataa eti ni dada zangu"
MAMA:"Aaah usihuzunike mwanangu, mtongoze unayempenda wewe sio kaka yao sababu huyu si baba yako" [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Jamaa flani alilala akaota amekufa, alipofika mbinguni Mungu akamwambia amempa nafasi nyingine ya kuishi.Akaambiwa achague atataka kurudi kama mnyama gani kati ya mbuzi na kuku.
Jamaa akachagua kuku ikambidi aanze kufanya mazoezi ya kutaga mayai kabla hajarudishwa duniani.
Akaanza kutaga yai la kwanza likatoka vizuri akaendelea hivyo hadi akafikisha kumi.
Asubuhi akaamshwa na makofi ya mkewe "balaa gani hii mume wangu, umejisaidia kitandani.!!"
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mshikaji flani baada ya kuzidiwa na kiu ikabidi agonge nyumba ilio karibu kuomba maji,akafunguliwa mlango na mtoto, alipoomba maji akaletewa glass ya maziwa! Alipomaliza kunywa akaongezewa glass nyingine ya maziwa, ikabidi aulize "mbona mnagawa maziwa kwa wingi?" Dogo akamjibu "maziwa yaliingiwa na panya kwa hivyo kila mtu hayataki!" mshikaji akapigwa na butwaa glass ikamponyoka na kuvunjika, Dogo kuona hivyo akapiga kelele "mamaa ile glass ya bibi anayotemea mate imevunjika" [emoji12][emoji13][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mke alikuwa anataka kununuliwa nguo na mumewe
MKE: Honey jana nimeota umeninunulia nguo nzuri"
MUME: "Wow! vizuri sana dear, leo ukiota uwe umeshaivaa tayari!" [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mwalimu kaagiza wanafunzi wa darasa la tano watege vitendawili.
MWANAFUNZI: kitendawili
MWALIM: 'tega"
Mwanafunzi: "NIVUE NGUO NIKUPE UTAMU..!"
MWALIMU: kwa hasira anakufundisha upuuzi huo? toka hapa nisikuone darasani haraka
MWANAFUNZI: Jibu lake ni NDIZI" kama hujui si useme tu [emoji12][emoji13][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Jamaa mwenye roho mbaya uswahilini alienda phamacy,
MSHIKAJI:"Binti
hujambo?"
BINTI:"Sijambo kaka, karibu
nikusaidie nini?"
MSHIKAJI:"Nahitaji dawa ya maumivu, maana jirani yangu Baba Yusuf amenunua BODABODA sasa roho yangu inaniuma kweli..!"
BINTI:"Tobaaaa..! akamuandikia Paracetamol 2x3 [emoji12][emoji13][emoji13][emoji23][emoji23]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…