Read this article and see how Tanzania goes over the top in trying to suffocate Kenya to the extent of jeopardizing its own interests! It could be for one of only two things: jealosy or actual grievances (let's discuss this).
Read here and you will see, Tanzania had ACTUALLY closed its airport to Kenyan air traffick when the JKA caught fire!
Tanzania refused to sell Gas to Kenya but sold it to China! When there was food scarcity in Kenya, Tanzania refused to sell maize to Kenya, saying it also faced food shortages.....but weeks later, sold the same maize to Uganda!
I have heard many stories even on individual levels : Kenyans being denied to fly from Tanzanian airports, others being denied permits to conduct businesses. Let's discuss this issue because I believe those who are doing this, putting these laws, are not doing so for the benefit of the Tanzanians. I fear, before this 4th republic of CCM is out, most of our neighbours will be our enemies!
(Malawi, Rwanda, Kenya, Uganda and.....)
Standard Digital News - Kenya : Tanzania would rather be in Southern Africa, it seems
Hawa ni watu wanaotaka kuleta uchonganishi usio na maana. Nashangaa makala hii imeruhusiwa bila hata ya utafiti mdogo tu usiohitaji hesabu.
Tanzania ilisaidia Kenya wakati wana njaa. Waziri wakati huo(Ruto????sina uhakika) alikwenda kumuona JK akiwa Maramba Tanga. JK akaruhusu kutolewa baadhi ya tani za chakula kutoka national grain reserve kwa Kenya.
Kwahiyo si kweli kuhusu madai hayo.
Pili, gesi haijaanza kuchimbwa katika kiwango cha biashara. Wanasahau kuwa ni China inayotandaza mabomba na gesi hiyo ikiwa tayari itabidi iuzwe nchi za jirani. Waziri Muhongo kasema hata umeme wa ziada itabidi uuzwe. Hakuna sababu ya kuzuia bidhaa inayohitaji wateja.
Tatu, Kenya ni mwekezaji namba 2 baada ya UK nchini Tanzania wala siyo nchi yoyote ya SADC kama anavtyosema mwandishi huyu zuzu. Kama Tanzania ingeizuia Kenya hilo lisingetokea.
Nne, kiwanja kilipoungua sijui Kenya walitaka Tanzania ifanye nini kama hawakuomba msaada. Ilikuwa ni wajibu wao kuomba msaada na sidhani hilo lilifanyika. Lakini pia lazima watu waangalie upande wa kifundi. Je, kulikuwa na facility za kutosha ku handle ndege za Kenya? Kama sivyo je kulikuwa na umuhimu wa kuhatarisha maisha ya watu kwasababu tu ya kumpendeza mkenya?
Tano, Kama Tanzania ingekuwa na chuki na Kenya basi isingetumia rasilimali zake ikiwemo gharama za viongozi kusuluhisha mzozo wa Kenya. Ilibidi waziri mkuu wa Turkey akiyekuwa aje Tanzania ziara yake iahirishwe ili JK na Mkapa waende Nairobi kuokoa roho za Wakenya. Si jirani mwingine wa EAC aliyeahi kufanya hivyo.
Sita, mwandishi anaposema Tanzania ni masikini, ni kweli lakini umasiki huo upo kwa kada gani?
Nadhani masikini wa Tanzania anaweza kuwa na nafuu kuliko masikini wa Kenya.
Westland na Karen siyo kwa mkenya ni kwa wazungu, unless uniambie 'kuosha choo cha mzungu' ni bora kuliko cha Mwafrika. Katika nchi masikini duniani kenya ipi karibia na 140 sasa hapo kuna unafuu gani?
Saba, kama watalii wanakuja na kulala Kenya hilo halina tatizo kwao. Si wana single entry visa na Rwanda?
Tanzania ni mshirika mkubwa sana wa eneo hilo , matusi yataiumiza Kenya na si Tanzania.
Tanzania haitegemei watalii waje Kenya ili waje Tanzania, ila Kenya inategemea watalii waingie kwa mgongo wa rasilimali za Tanzania. Hivyo lazima wawe waangalifu kama kumbu kumbu za kufunga mpaka zinavyoeleza huko nyuma.
Tunafahamu kuwa Kenya wanashabikia sana Tanzania ikiwa na mizozo lakini hilo haiifanyi Kenya iwe bora.
Kenya walipogombana Tanzania haikufaidika na chochote na wala sidhani Tanzania ikiwa na mizozo na nchi nyingine Kenya itafaidika. Lazima Kenya ielewe kuwa wao ni majirani wakubwa kuliko wengine na siasa za majitaka za kutaka watu wagombane ni za hovyo.
Ni lazima wasomi wa Kenya waelewe tatizo la wananchi wa kiwango cha chini na si ma tycoon wachache.
Huu ni uchochezi tu ambao mwisho wake ni Kenya kuwa Loser. Wamesahau soko lao kubwa EAC lipo wapi?