Wife kanizidi kipato lakini kila wiki lazima aniombe elfu 20 ya kusukia


Umeyatafuta umeyapata sasa unalia Lia ww mpe tu ni jukumu lako sasa nae alkua anakutega tu ukatae apate kununa na amefanikiwa
 
Jikune mahali unapofikia, wema usizidi uwezo. Mkeo ashiriki kikamilifu katika kuhudumia familia. Kaeni pamoja mpange budget ya nyumbani.

Sent from my TECNO-N2 using JamiiForums mobile app
 
yani anapata kipato mara 3 ya kipato chako alafu umpe 20 ya kusukia?

Tumia sauti yako, mpige biti kuwa huoni umuhimu wa yeye kufanya kazi , maana pesa yote hujui anafanyia nini na kama anahonga basi sio mda utamuachisha kazi au arudi kwao....

Mkifika uzeeni mwenzio atakuwa ana zaidi ya mil 100 bank wewe utakuwa na mil 5 au 3 ndio hapo utajikuta upo peke ako nyumbani......
 
Ndoa ndio iko hivyo Mkuu. Mwanaume ni provider. Mnakimbilia ssna kuoa halafu game la ndoa linawashinda. Pole sana.
 
Huyu ana ka ubinafsi kuwa makini
Hakuna relationship siku hizi. Ni ubinafsi mtupu. Kila mtu anavutia kwake tu. Ndoa hazina maana tena asee. Sasa hapo hio 2m anapeleka wapi kama jamaa ndio anatoa matumizi? Atakuwa spender mkubwa sana au anajenga jumba kwao.
 
Take care of your woman. Unahic ni kweli ataenda kusuka msuko wa 20k? Anataka umjali tu so that she feels like a woman anaejaliwa na mwanaume wake.

Don't stress it.
Sasa kama jamaa hana? Kwa nini akasirike? Jamaa amesema yeye ndio anatoa mahitaji ya home. Kwa nini mnamtetea sana demu hapa?
 
Mimi nina miaka hamsini na ushee wala sijawahi kuwaza juu ya kuoa!Bado nipo nipo sana.Ngoja kwanza nile hizi rahaa za dunia.Depression ya elfu 20 sitaki mie!
Wanaume wengi tunajiunga na hio club yako Mkuu. Ndoa ni stress tupu ziku hizi. Hasa kwa wanaume.
 
Ameshasema HANA hio hela. Yeye ndio anatoa matumizi ya home? Watu mnaandika posts ndefuuuu, halafu hamjasoma original post
 
Yuko sahihi zaidi ya 100% anataka uwe responsible.
Kutoa matumizi ya nyumbani sio kuwa responsible? Lazima umpe 20k ya kusuka. Yani USHAURI WATU MNATOA HAPA, no wonder wanaume wenzetu wanajinyonga kila siku sababu ya mapenzi. Mtasimama imara lini? Na kuwa kama wanaume? Wenye misimamo na kuwa kama KICHWA CHA FAMILIA HATANKAMA MKE ANAKUZIDI KIPATO?
 
Kukasirika sio kisa hana. Ni namna alivyomjibu. Kama anamuambia msela wake. [emoji28] [emoji28]

Hlf mwanaume kuwaza waza pesa ya mkeo ni umama.
Mwanaume ndio kichwa cha familia. Hata kama mke anakuzidi pesa. Ni lazima mume ujue hela inaenda wapi. Inafanyia nini nk. Ndio maana ya ndoa hio.
 
Nimeshaanza kuona atakuwa huyu dada ni ndugu zangu wakichagga, yaani anavutia kwake kabisa, sasa ukute huyo demu anasomesha watoto wa kaka ake watatu na watoto wa baba ake wa kambo, afu anajenga kwao na kuna kabiashara anafanya mahali, yaani mimi mjomba angu anapata sana shida kwa mke wake japo wote wachagga mke na mume, huyo mama amemzidi pesa lakini anavutiaga kwake, mjomba anabaki ivo though huyu mjomba angu ni mtata angekutana na mtu dhaifu sipati picha.
Hakuna relationship siku hizi. Ni ubinafsi mtupu. Kila mtu anavutia kwake tu. Ndoa hazina maana tena asee. Sasa hapo hio 2m anapeleka wapi kama jamaa ndio anatoa matumizi? Atakuwa spender mkubwa sana au anajenga jumba kwao.
 
Umeandika haraka mno na ww hujaeleweka. Unaposema mahitaji yote ya familia unatoa ww na hiyo 500k yako, hela yake ambayo ni almost 4 times ya kipato chake inaenda wapi??
 
Mkuu kwani 500K unagharamia home. Na Je? Iyo milioni 1.9 ya kwake huwa ina kazi zipi home maana ni mwanamke na ameamua kufanya kazi tena mshahara ni zaidi ya wako.
 
We jua kuhusu pesa unayotoa. Achana na mengine.

ukitaka amani, kuwa provider. Wanawake hawa, wengi hyo power hawawezi kuihandle. Akianza kukuchangia changia. Kuna siku atakuletea mambo ya ajabu sana na ya kukuvunjia heshima.
Ndio maana wengine HATUTAKI hizo stress. Hadi sasa binafsi sijaona mwanamke wa kuoa. Nakula maisha tu. Na ni raha mno kutokuwa na stress za ndoa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…