William Lukuvi ndiye aliyekuwa kipenzi cha Hayati Magufuli

William Lukuvi ndiye aliyekuwa kipenzi cha Hayati Magufuli

Kwa chongolo umetuongopea mchana kweupee

Nikikumbuka mtoto pendwa aliyekuwa anajimilikisha dsm alikuwa anamjibu hovyo huyo chongolo

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Inawezekana Ila mtoto pendwa pia aliwahi kumvimbia na kumjibu hovyo mpango, Ila mwisho nani alibaki?
Huenda hata jiwe alikua kamchoka bashite Ila alijua amimtumbua atawapa ushindi watu ndio ikabidi amsubiri kwenye ubunge
 
This is the fact. Hongera kwa kuliona hilo na wewe. Mama Samia ni Mtanzania halisi na muungwana.
Kuna baadhi ya washauri wake ndio wanamuharibia kwenye hii 'Kesi' ya Mwamba awaache Polisi waaibike yeye ajitoe
 
Za ndani kabisa Waziri William ndiye kiongozi pekee ambaye hakuwahi kupishana na JPM.

Ndiye Waziri pekee aliyekuwa na uwezo wa kumshusha munkali JPM duru 'zinatabanaisha.'

Wakati fulani inasemekana baadhi ya mawaziri wenzake walipokuwa na mgogoro wa wazi na JPM walikuwa wanamfuata William wakiomba akawaombee msamaha.

Vyanzo vya uhakika vinatabanaisha Magufuli alimpenda William kwa sababu ni mkweli na hakuwahi kumdanganya hata alipotaka ukweli wa jambo fulani kutoka kwa wachunguzi ilibainika ni kweli.

Walio karibu na JPM wanadai wakati fulani 2020 alifikiria kumteua William awe Waziri Mkuu.

Hata ile kauli ya JPM ya kusema William na mwenzake ni wazee hawawezi kuwa Rais ilikuwa ni geresha tu bali 2025 KWA NGUVU YA JPM WILLIAM ANGEKUWA MGOMBEA WA U RAIS TANZANIA kupitia CCM.

Nyongeza:

Baada ya Bashiru kuwa Katibu Mkuu Kiongozi chaguo la Magufuli ilikuwa Chongolo amteue kuwa Katibu mkuu wa CCM

Kwa hiyo Chongolo hayupo hapo kwa bahati mbaya mama aliendeleza tu huo uteuzi kwa sababu alikuwa anajua.
Hizi Kashata tu, JPM alimwandaa kabudi hutaki kufa
 
Mada ni Lukuvi, ukaruka ruka humo ndani ukaangukia kwa Chongolo!

Ila unahangaika sana aisee, huyo Magufuli alishakufa sasa hivi anapambana na MUNGU wake huko aliko.
 
Umewahi kufika jimboni kwake?!

Kuhusu jimboni kwake i don'gave f.....!!. Nitampigia awe rais wa nchi sio jimbo.

Kama hakuna maendeleo nadhani atakufaa hata wewe,maana hamkawii kusema anapendelea kwae sasa kama haja fanya lolote jimboni kwake then ni mtu sahihi kwako pia.
 
Kuna baadhi ya washauri wake ndio wanamuharibia kwenye hii 'Kesi' ya Mwamba awaache Polisi waaibike yeye ajitoe

Hahahaaa hata wanaoitwa chawa hawajafikia kujipendekeza kiasi cha kukosa aibu namna hii.
Wakati anasema mwamba hana heshima alikuwa anashauriwa nanani na wewe ulikuwa wapi.

Endeleeni kucheka huku mnalia.
 
Mada ni Lukuvi, ukaruka ruka humo ndani ukaangukia kwa Chongolo!

Ila unahangaika sana aisee, huyo Magufuli alishakufa sasa hivi anapambana na MUNGU wake huko aliko.
Unaelewa maana ya nyongeza ama unataka kufurahisha genge ndugu!

Soma kuelewa.
 
Kuhusu jimboni kwake i don'gave f.....!!. Nitampigia awe rais wa nchi sio jimbo.

Kama hakuna maendeleo nadhani atakufaa hata wewe,maana hamkawii kusema anapendelea kwae sasa kama haja fanya lolote jimboni kwake then ni mtu sahihi kwako pia.
Ngazi yake ya kuletea maendeleo kwa sasa ni jimbo kama ameshindwa kupeleka maendeleo kwenye jimbo lake tu kwa kipindi cha miaka 20 atawezaje kwenye ngazi ya taifa kwa miaka 5 au 10?!
 
Lukuvi sina shaka naye hata kidogo. Anajitahidi sana kufanya kazi zake kwa umahiri unaopaswa.
Akigombea nitamchagua kwa nguvu zangu zote.
Viva William Lukuvi.
 
Lukuvi huyuhuyu aliyefokewa na kuambiwa kampatia kazi mkewe ATCL kwa upendeleo kutumia cheo chake cha uwaziri na kulazimika kumuachisha kazi ndio alikua kipenzi cha Jiwe!!??? Sasa kama hauelewani naye inakuaje?
Hakuwa Lukuvi,alikuwa marehemu waziri wa mambo ya nje Balozi
 
Kama mtu anashindwa kuleta maendeleo kwenye jimbo atawezaje kwenye taifa zima?
Jk alikua mbunge chalinze, palikua hoi hadi anapta uraisi
JPM alikua mbunge chato, palikua hoi hadi anapata uraisi
Mama Samia alikua mbunge makunduchi, pako hoi hadi Sasa
Ikiwa hao walikua maraisi pamoja na majimbo waliyotoka kuwa hoi
Iweje kwa lukuvi iwe issue?
Japo Mimi simkubali lukuvi
 
Jk alikua mbunge chalinze, palikua hoi hadi anapta uraisi
JPM alikua mbunge chato, palikua hoi hadi anapata uraisi
Mama Samia alikua mbunge makunduchi, pako hoi hadi Sasa
Ikiwa hao walikua maraisi pamoja na majimbo waliyotoka kuwa hoi
Iweje kwa lukuvi iwe issue?
Japo Mimi simkubali lukuvi
Sasa huwa wanapimwaje kabla ya kupewa uongozi?!
Inabidi kutafuta watu walioleta mabadiliko makubwa katika maeneo, taasisi au mashirika waliyoongoza ndio wawe viongozi.
 
Ngazi yake ya kuletea maendeleo kwa sasa ni jimbo kama ameshindwa kupeleka maendeleo kwenye jimbo lake tu kwa kipindi cha miaka 20 atawezaje kwenye ngazi ya taifa kwa miaka 5 au 10?!

Ondoa shaka, ataweza sababu atakuwa na viwezeshi vyote mikonini mwake.
 
Hakuwa Lukuvi,alikuwa marehemu waziri wa mambo ya nje Balozi
Umechanganya mkuu. Issue ya mke wa marehemu Balozi ilikua ni kupishana lugha na traffic police. Suala Lukuvi lilikua ajira ta mke wake ATCL

Screenshot_20220104-140543_Chrome.jpg
 
Back
Top Bottom