William Miller: Kama Yesu hakujua Hisabati au kutafsiri mambo bora angalikaa Kimya. Mbona siku ya mwisho wa dunia inakokotoleka kirahisi?

William Miller: Kama Yesu hakujua Hisabati au kutafsiri mambo bora angalikaa Kimya. Mbona siku ya mwisho wa dunia inakokotoleka kirahisi?

Ume-panic sana mpaka inafikia hatua umeamua kujitungia mambo....Hebu kaa chini usome mada ueleww.....mbona mada ina mlenga nwana hisabati nguli wa kukokotoa tarehe Bw William Miller....

Mada haimuongelei Ellen G White.....Kwanini unalazimisha kumuweka Ellen G White....?
Kwa sababu mwishoni mleta mada amewa attack wasabato. Kwamba yesu anachambua majina ya wasabato !! Kitu ambacho hakipo ktk vitabu vyote.

Haya mambo ya ushabiki, unaoleta attacking and defensing kwa imani zetu hizi, hazimsaidii mtu yeyote mkristo kuona ufalme wa Mungu. Hata majuzi nimesikia eti wengine wamefuta Holly Bible ktk taratibu za ibada na kuiingiza wanayoyaita ya kisasa!! Lakini yoote haya, hayaleti uhalali wa dhehebu fulani dhidi ya nyingine machoni pa bwana, bali matendo yako.

Uandishi unaoamsha ushabiki wa wakristo kushambuliana, kwa namna yoyote haufai. Katika imani zetu hizi kuna mambo mengi yalikosewa, lakini ni kulingana nyakati na tamaduni za wakati huo na taathira zake.
 
Hayo ambayo hayako kwenye Biblia mimi siyajui...jambo lolote ambalo haliko kwenye biblia si mhimu kwa wokovu wetu!
ni jambo jema sana umekiri mwenyewe kuwa hayo yasioandika ambayo ni mengi zaidi wewe HUYAJUI. na sidhani kama ni kosa lako ila ni la kihistoria tu na asili zetu. hivyo kwako hakuna kilichoharibika na kwangu pia hakuna kilicho haribika isipokuwa mimi na wakatoliki tuyajuayo yalio nje ya biblia tuna Mungu MREFU na ninyi msio yajua mna Mungu MFUPI.

USHAURI
siku nyingine usirudie tena kuwaita ndugu zako katika kristo kuwa wanamafundisho ya kipagani au ni wapagani ilihali wewe mwenyewe hujui YOTE na wala huna YOTE yaliofanywa na kufundishwa na Yesu na mitume wake. na kama biblia yako inakiri kuwa yalioandikwa ni machache sio yote na wakati huohuo yesu kabla ya kupaa mbinguni aliwaagiza wanafunzi wake wakafundishe YOTE na kusema YOTE aliowaamuru na waliyo jifunza kwake. na hata yatakayo sahaulika aliwaahidia ROHO MTAKATIFU ili kuyakumbuka na kuyabeba yote.

hivyo uhalali wa kuwaita wengine wapagani sijui unautoa wapi ?? na kwa chanzo kipi ??
 
ndio tunajivunia na tunavyo vingi kwelikweli vya mafundisho unayoyaita ya waanadamu vipo vingi tu na vya neno la Mungu vipo vingi tu. na hatuko wachoyo yeyote anasoma hata anaetutukana ruksa anasoma.


pia kuna mengi sana zaidi ya yaliomo kwenye biblia ambayo yesu na mitume wake waliyafanya na kufindisha ila hayajaandikwa. usijisahaulishe kuhusu hilo
Ibada za sanamu kawafundisha nani?
FB_IMG_1540840391863.jpeg
 
Kipimo ni Biblia ,Yesu alifundisha Biblia , mitume walifundisha Biblia .
kabla ya biblia kupatikana walitumia kipimo gani ?? na ambako biblia hazisomwi wanatumia kipimo gani ??

kuna madhehebu zaidi ya 2000 na yote yana biblia moja je ni roho gani huyo kigeugeu anayefundisha kweli zaidi 2000 toka kwenye chanzo kimoja ?? au hajui kusoma ??

kuna mahali unakosea sana jitafakari na uchukue hatu
Wewe nae unafanya kosa kwa kufikiri kwamba elimu ya mbingu inapimwa kwa degree . Hata ukijenga chuo angani kama Roho hayupo ni bure
umetumia kipimo gani au umetumia kigezo gani kujua kuwa watu wajishughulishao kutafuta ELIMU ya mbinguni na duniani kadili ya maagizo ya kitabu cha mithali na agizo la Yesu la kumpenda Mungu kwa AKILI zako zote. hao HAWANA ROHO. ila wewe na watu wenye mawazo na mitazamo kama yako MNA ROHO ?? tueleze umetumia kipimo gani mpendwa ??
Hayo yaliyoandikwa ndiyo Mungu alikusudia tujifunze
na aliyesemama kwamba enendeni ulimwenguni kote mkawafundishe YOTE na kuwaamuru kuyashika YOTE niliowafundisheni na mliojifunza kwangu. alikuwa mwongo sio ? a wewe unaifahamu biblia kuliko yeye ?
 
kabla ya biblia kupatikana walitumia kipimo gani ?? na ambako biblia hazisomwi wanatumia kipimo gani ??

kuna madhehebu zaidi ya 2000 na yote yana biblia moja je ni roho gani huyo kigeugeu anayefundisha kweli zaidi 2000 toka kwenye chanzo kimoja ?? au hajui kusoma ??

kuna mahali unakosea sana jitafakari na uchukue hatu

umetumia kipimo gani au umetumia kigezo gani kujua kuwa watu wajishughulishao kutafuta ELIMU ya mbinguni na duniani kadili ya maagizo ya kitabu cha mithali na agizo la Yesu la kumpenda Mungu kwa AKILI zako zote. hao HAWANA ROHO. ila wewe na watu wenye mawazo na mitazamo kama yako MNA ROHO ?? tueleze umetumia kipimo gani mpendwa ??

na aliyesemama kwamba enendeni ulimwenguni kote mkawafundishe YOTE na kuwaamuru kuyashika YOTE niliowafundisheni na mliojifunza kwangu. alikuwa mwongo sio ? a wewe unaifahamu biblia kuliko yeye ?
Hivi unaandika nini hasa ndugu?
 
Hayo ambayo hayako kwenye Biblia mimi siyajui...jambo lolote ambalo haliko kwenye biblia si mhimu kwa wokovu wetu!

Kama ambavyo hamkufahamu baadhi ya mambo au mliyafahamu isivyo ndivyo hivyo pia mtakuja kuelewa siku moja kwamba Biblia siyo document ambayo imebeba kila jambo ambalo limetokea katika historian ya wokovu Wa mwanadamu. Iko siku mtakuja kuelewa kuwa Biblia ni mapokeo. Ellen White hakuamini katika Utatu Mtakatifu lakini leo baadhi yenu mnaamini jambo hilo tayari.
 
Kama ambavyo hamkufahamu baadhi ya mambo au mliyafahamu isivyo ndivyo hivyo pia mtakuja kuelewa siku moja kwamba Biblia siyo document ambayo imebeba kila jambo ambalo limetokea katika historian ya wokovu Wa mwanadamu. Iko siku mtakuja kuelewa kuwa Biblia ni mapokeo. Ellen White hakuamini katika Utatu Mtakatifu lakini leo baadhi yenu mnaamini jambo hilo tayari.
Biblia siyo document iliyobeba kila kitu? Maajabu! Kwahiyo hayo mengine yako kwenye kitabu gani?
 
3. Papa hatawafumusha wasabato kusali jumamosi kama ulivyodai, badala yake atawalazimisha watu wote kusali siku ya kwanza ya juma (yaani Jumapili) badala ya siku ya saba ya juma (yaani Jumamosi).

Acha uongo mkuu, Jumapili ni siku ya Pili ya Juma
na Jumamosi ni siku ya kwanza(mosi) ya Juma

mtililiko ni huu👇

1. Jumamosi
2. Jumapili
3. jumatatu
4. Jumanne
5. jumatano
6. alhamisi
7. ijumaa

kwahiyo kimahesabu na kimantiki Ijumaa ndio siku ya saba ya juma
 
Yesu alipokuwa ameketi kwenye Mlima wa Mizeituni, wanafunzi wake wakamjia faraghani, wakamuuliza, “Tuambie, mambo haya yatatukia lini, nayo dalili ya kuja kwako na ya mwisho wa dunia ni gani?”

Yesu akawajibu, “Jihadharini, mtu yeyote asiwadanganye. Kwa maana wengi watakuja kwa Jina langu, wakidai, ‘Mimi ndiye Kristo,’ nao watawadanganya wengi.

VITA: Mtasikia habari za vita na matetesi ya vita. Angalieni msitishike, kwa maana haya hayana budi kutukia. Lakini ule mwisho bado. Taifa litainuka dhidi ya taifa, na ufalme dhidi ya ufalme.

NJAA& MATETEMEKO: Kutakuwa na njaa na mitetemeko ya ardhi sehemu mbalimbali. “Ndipo mtasalitiwa, ili mteswe na kuuawa, nanyi mtachukiwa na mataifa yote kwa ajili yangu.

UPENDO KUPOA: Wakati huo, wengi wataacha imani yao, nao watasalitiana kila mmoja na mwenzake na kuchukiana.

ROHO YA UONGO: Watatokea manabii wengi wa uongo, nao watawadanganya watu wengi. Kwa sababu ya kuongezeka kwa uovu upendo wa watu wengi utapoa, lakini yule atakayevumilia hadi mwisho ataokolewa.

Injili ya Ufalme itahubiriwa ulimwenguni kote kuwa ushuhuda kwa mataifa yote. Ndipo mwisho utakapokuja. “Hivyo mtakapoona lile ‘chukizo la uharibifu’ lililonenwa na nabii Danieli limesimama mahali patakatifu (asomaye na afahamu), basi wale walioko Uyahudi wakimbilie milimani. Yeyote aliye juu ya dari ya nyumba asishuke ili kuchukua chochote kutoka ndani ya nyumba. Aliye shambani asirudi nyumbani kuchukua vazi lake. Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo! Ombeni ili kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi au siku ya Sabato. Kwa maana wakati huo kutakuwa na dhiki kuu ambayo haijapata kuwako tangu mwanzo wa dunia mpaka sasa: wala haitakuwako tena kamwe. Kama siku hizo zisingefupishwa, hakuna hata mtu mmoja ambaye angeokoka. Lakini kwa ajili ya wateule, siku hizo zitafupizwa. Wakati huo kama mtu yeyote akiwaambia, ‘Tazama, Kristo huyu hapa!’ Au, ‘Kristo yuko kule,’ msisadiki. Kwa maana watatokea makristo wa uongo na manabii wa uongo, nao watafanya ishara kubwa na maajabu mengi ili kuwapotosha, ikiwezekana, hata wale wateule hasa. Angalieni, nimekwisha kuwaambia mapema. “Kwa hiyo mtu yeyote akiwaambia, ‘Yule kule nyikani,’ msiende huko. Au akisema, ‘Yuko kwenye chumba,’ msisadiki. Kwa maana kama vile umeme utokeavyo mashariki na kuonekana hata magharibi, ndivyo itakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu. Kwa maana popote ulipo mzoga, huko ndiko wakusanyikapo tai. “Mara baada ya dhiki ya siku zile, “ ‘jua litatiwa giza, nao mwezi hautatoa nuru yake; nazo nyota zitaanguka kutoka angani, na nguvu za anga zitatikisika.’


UJIO WA PILI WA KRISTO: “Ndipo itakapotokea ishara ya Mwana wa Adamu angani, na makabila yote ya dunia yataomboleza. Nao watamwona Mwana wa Adamu akija juu ya mawingu ya angani, katika uwezo na utukufu mkuu. Naye atawatuma malaika zake kwa sauti kuu ya tarumbeta, nao watawakusanya wateule wake kutoka pande zote nne za dunia, kutoka mwisho mmoja wa mbingu hadi mwisho mwingine.
Mathayo 24:3‭-‬7‭, ‬9‭-‬31 NEN
Kwa hoja hii mjadala naamini ulifungwa
 
Miller hakuanzisha usabato. Walioanzisha SDA ni wakina Joseph Bates, James White na Ellen White na wengine.

Miller alikuwa mbabtist....na hata Ellen white na wenzake alikuwa wababtist, baada ya hiyo Great Disappointment, walianza kusoma biblia upya na kujifunza unabii upya, na ndipo EGW akaonyeshwa maana halisi ya unabii wa Daniel 8:14 na akaonyeshwa patakatifu pa mbinguni na akaonyeshwa lile sanduku la agano lililo na Amri Kumi za Mungu, na amri ya nne ya ya sabato ilikuwa inang'aa kuliko amri zingine.

Na ndiyo alipoendelea kujifunza biblia akaendelea kufunuliwa zaidi kuhusiana na sabato. Na ndipo yeye na wenzake wakaondoka katika kanisa la Baptist na kuanza kusali siku ya saba ya Juma, na ndipo SDA kama dhehebu likaanzishwa.
Kwahiyo huo unabii wa kwanza ulikuwa feki na mkauamini mkaishia kuwa Disappointed?

Sasa unauthibitisho gani ufunuo huo mwingine sio the Next disappointed ?
 
Kukosea kutafsiri unabii siyo dhambi...hata wayahudi hawakuulewa unabii wa ujio wa Yesu, walikuwa wanamsubiri masihi mwingine. Hata wanafunzi wa Yesu walikuwa wanajua kuwa Yesu anakuja kusimika ufalme wake duniani, na ndiyo maana alivyowaambia anaenda zake mbinguni hawakumuelewa.

Pointi ni kwamba, huo unabii ulikuwa unalenga tukio fulani, lakini si kama yeye alivyoelewa, swali ni kwamba nyie mnaombeza Miller mnatoa tafasri gani ya huo unabii?
Kutoa unabii ni jambo moja, kukosea kutafsiri unabii ni jambo jingine
 
Alichokuwa anakiona Yohana katika ndoto kuliashiria jambo jingine halisi. Kwa mfano anasema aliona Mwanamke amevikwa Jua,Nyota na Mwezi. Kwa hiyo huwezi kusema ni kweli kuna mtu anaweza kuvaa Jua au Nyota. Kumbe hayo maono kila moja lilikuwa na maana yake ambayo Kanisa la Mwanzo walikuwa wakielewa maana yake. Kimsingi lugha na staili aliyotumia ni lugha ya mafumbo iitwayo APOCALYPTIC. Ilikuwa ni lazima Yohana awasiliane na wanakanisa katika lugha hiyo ili kumkwepa Kaizari NERON ambaye ndiye leo wasbato mnasema ni PAPA ajaye.
Mkuu uko vizuri sana kwenye mambo ya tafsiri za kibiblia
Mimi nimezaliwa kwenye familia ya kiLutheri lakini nawaelewa na kuwaheshimu sana hasa Mapadri kwenye suala la tafsri na theolojia
 
Imani na mahesabu wapi na wapi? Huyo Miller hajiulizi kwanini Newton alichapisha mambo ya mahesabu na fizikia ambayo hadi leo tunayatumia lakini mambo mengine ya imani alielewa kwamba hiyo tasnia ina namna yake, akaiheshimu na kuacha iende kiimani.
Sasa tuambie hizo hesabu za kiunabii zikoje? Au unaona hazina manana!
 
1. Tupatie andiko kwamba Mbingu ina vyumba au horizons.
2. Yesu ni Mungu na hivi ana uwezo wa kutuombea akiwa popote pale.je,kulikuwa na ulazima gani kwake kuingia huko Chumbani("patakatifu pa patakatifu") toka mwaka 1844 hadi leo ili kufanya tu hiyo huduma ya maombezi?
3. Ellen White yeye alifundisha kwamba Yesu yuko hapa patakatifu pa patakatifu akiendesha hukumu ya kipelelezi(Investigative Judgement).Je, huduma ya maombezi ni hukumu ya upelelezi?
Dah! Upelelezi gani tena wakuu? Ina maana Yesu hawezi kuona madhambi yetu hadi afanye upelelezi? Je ndo hali inayochangia hukumu kuchelewa kisa upelelezi haujakamilika? Kama Yesu alitufia msalabani kuna haja gani ya yeye kujifungia chumbani tena?
 
Back
Top Bottom