Tetesi: Wilson Nkambaku anafuata baada ya Nyalandu kuondoka CCM!

Tetesi: Wilson Nkambaku anafuata baada ya Nyalandu kuondoka CCM!

Hiyo sifa namba 5 niliamini anayo na angetafakari kabla ya kufanya maamuzi. Lakini uliposema anayo hiyo sifa kama Nyalandu nimeumbuka kwa sababu nimegundua kumbe ni usanii tu. Waulize CHADEMA waliokoa shilingi ngapi za Watanzania walipoibua madhambi ya Nyalandu kama waziri katika serikali yetu.
 
Aisee. Kama huyo kijana atarudi jimboni mi ntampa kura, he's so intelligent. Kingu Hana chake Na naiona Singida ikiwa Kama Arusha
Ila kuna ka mgawanyiko hapo.Mbona wale hawajaenda kumuona mwenzao hospitalini?
 
Anaitwa Wilson Nkambaku, Kwa sasa ni Katibu wa CCM mkoa wa Mbeya aliyepangiwa kazi mwaka huu. Alikua mkuu wa wilaya awamu ya nne katika wilaya za Meatu na Arumeru kabla ya kurithiwa na Alexander Mnyeti.

Kwanini anaondoka?

1.Ikumbukwe huyu kijana wa Kinyaturu ndiye aliyerithi mikoba ya Nyalandu kwenye kiti Urais wa UKWATA pale Iiboru Sekondari miaka ya nyuma baada ya kumaliza muda wake.

2. Exposure zake zote nje ya nchi ni sawa na za Mh Nyalandu, alifanikiwa haya yote kupitia kwa kaka yake huyu ambaye ameondoka CCM na kwenda CHADEMA.

3.Alishinda nafasi ya Ubunge kwenye kura za maoni CCM 2010 jimbo la Singida Magharibi, lakini akadhulumiwa kwa fitna na hongo za CCM,alihamia CHADEMA ili kufanikisha mipango yake ambapo aliaminiwa na wananchi wakaahidi kumchagua kwa kura zote lakini baadae aliyekua Rais wakati huo alitumia nguvu nyingi kwa kumtumia Mh Nyalandu kumshawishi asihamie CHADEMA ili jimbo la Singida Magharibi lisiende na maji,ailirudi CCM kwa kushawishiwa na Nyalandu na baadae kupewa ukuu wa Wilaya.

4.Ndiye rafiki mkubwa sana pengine kuliko hata marafiki wengine wa Nyalandu hapa nchini.

5.Hawezi kuiona future yake ya kisiasa kwenye hii CCM iliyojaa visasi iliwa kaka yake ameondoka CCM.

5. Ni kijana mwaminifu na mlokole asiyekua na doa hata kidogo, features zake ni sawa na za Nyalandu.

6. 2020 kijana wa Kinyiramba Elibariki Kingu ajiandae mapema tu kuachia jimbo la watu.Itakua ni Combination ya Tundulu LISSU+Nyalandu kumnadi Nkambaku.


Je,mnafikiri Nyalandu yuko peke yake?
Kuna mengina ndani ya kapu, Lakini kuna tetesi kua Mh Nyalandu ana Marafiki zake Wenyeviti na Makatibu wa CCM wa sasa wa wilaya na mikoa wasiopungua 100 ambao ndio walikua wapambe zake kwenye kusaka sahihi za kukamilisha mipango ya kugombea Urais 2015 ambao watamfuata muda si mrefu.

CCM nawaasa kaeni mtulie tuu, msianze kuchafua watu wanapoonfoka chamani. Watafteni na hawa 100 kabla hawajaondoka.
Vyovyote vile itakavyokuwa hata kama watahama milioni sita wenye akili tunajua hawahami kwa kuwa ni wazalendo wanahama kutafuta maslahi binasfsi na kamwe si kwa maslahi ya umma.
 
Aisee. Kama huyo kijana atarudi jimboni mi ntampa kura, he's so intelligent. Kingu Hana chake Na naiona Singida ikiwa Kama Arusha
Duu, maskini Dodoma ....mtajanjaruka lini muwe kama wa-Singida?
 
Mahanju wewe ni muongo wala huna hoja labda chadema wanakulipa unayemzungumzia ni kada safi wa ccm.nahawezi kukihama chama cha mapinduzi
Sasa unachobishia ni kitu gani wewe? Huyu kijana CCM wamemtesa sana kufanyia figisu figisu kura za maoni ya ubunge mara mbili, angekua anathaminiwa asingetolewa ukuu wa Wilaya. Huko ukatibu tu wa chama ni juhudi za kina Nyalandu. Hutaki achaa
 
Kwanza nikwambie Kuwa hata Nkambaku akienda CDM hawezi shinda kwa mgongo wa LISU. Lisu naye safari hii hawezi shinda. DC MTATURU amewekwa pale aimed baada ya kuwasambaratisha Mwanza. Wilaya ya Hiyo ndiyo kazaliwa Mtaturu anayejipanga 2020.

Kinachoweza kumharatibu Nkambaku ni Kama ataamua kuja CDM, ijapo kwa Watu wa Mbeya wanasema uchaguzi unaondelea huko wamevurunda sana na RC wa LINDI ambapo uteuzi haukulenga Watu wenye sifa, Bali Watu ambao Zambi a naona what amsaidia yeye au Watu ataksopenda wagombee 2020. Hii naambiwa Nkambaku aliingizwa king
Wewe inawezekana hata Nkambaku humjui unaropoka tuu, tuulize wazee wa wilaya hiyoo tulieshida nae. Kana kashindwa Njau aliyekua aki-cover projects zote ambazo LISSU hakufanya lakini hakuambulia chochote. Mtatura hawezi kitu na asije akajidanganya, Wanaikungi wote wanajua kua amewekwa pale kwa ajili ya LISSU, wmejiandaa kumuonyesha nini maana ya nguvu ya umma.

Khaa yaani mtaturu apambane na LISSU? Kwa level ipi? Wewe LISSU kwa Ikungi ni habari ya mjini.Mtaturu hakuna kitu hapo tena asijidanganye na kelele zake zisizo na madhara.

Mwanza usiifananishe na Ikungi bhana, Kura za makabila flani ziibeba CCM kwa sababu ya Mgombea urais. Wale Mabula wote walibebwa na Magufuli wala hakuna lingine usimtetee Mtaturu.

Khambaku Singida magharibi ameshinda mara mbili lakini CCM wanamfanyia fitna, ngoja ahamie chadema uone kama yule Mnyiramba atapata kitu.
 
Vijana kwenye siasa si wa kuwaamini.Wanapoona maslahi binafsi yana yameathirika,hawakawii kubadili mtizamo.Mpatie begi lililojaa minoti!!
 
Anaitwa Wilson Nkambaku, Kwa sasa ni Katibu wa CCM mkoa wa Mbeya aliyepangiwa kazi mwaka huu. Alikua mkuu wa wilaya awamu ya nne katika wilaya za Meatu na Arumeru kabla ya kurithiwa na Alexander Mnyeti.

Kwanini anaondoka?

1.Ikumbukwe huyu kijana wa Kinyaturu ndiye aliyerithi mikoba ya Nyalandu kwenye kiti Urais wa UKWATA pale Iiboru Sekondari miaka ya nyuma baada ya kumaliza muda wake.

2. Exposure zake zote nje ya nchi ni sawa na za Mh Nyalandu, alifanikiwa haya yote kupitia kwa kaka yake huyu ambaye ameondoka CCM na kwenda CHADEMA.

3.Alishinda nafasi ya Ubunge kwenye kura za maoni CCM 2010 jimbo la Singida Magharibi, lakini akadhulumiwa kwa fitna na hongo za CCM,alihamia CHADEMA ili kufanikisha mipango yake ambapo aliaminiwa na wananchi wakaahidi kumchagua kwa kura zote lakini baadae aliyekua Rais wakati huo alitumia nguvu nyingi kwa kumtumia Mh Nyalandu kumshawishi asihamie CHADEMA ili jimbo la Singida Magharibi lisiende na maji,ailirudi CCM kwa kushawishiwa na Nyalandu na baadae kupewa ukuu wa Wilaya.

4.Ndiye rafiki mkubwa sana pengine kuliko hata marafiki wengine wa Nyalandu hapa nchini.

5.Hawezi kuiona future yake ya kisiasa kwenye hii CCM iliyojaa visasi iliwa kaka yake ameondoka CCM.

5. Ni kijana mwaminifu na mlokole asiyekua na doa hata kidogo, features zake ni sawa na za Nyalandu.

6. 2020 kijana wa Kinyiramba Elibariki Kingu ajiandae mapema tu kuachia jimbo la watu.Itakua ni Combination ya Tundulu LISSU+Nyalandu kumnadi Nkambaku.


Je,mnafikiri Nyalandu yuko peke yake?
Kuna mengina ndani ya kapu, Lakini kuna tetesi kua Mh Nyalandu ana Marafiki zake Wenyeviti na Makatibu wa CCM wa sasa wa wilaya na mikoa wasiopungua 100 ambao ndio walikua wapambe zake kwenye kusaka sahihi za kukamilisha mipango ya kugombea Urais 2015 ambao watamfuata muda si mrefu.

CCM nawaasa kaeni mtulie tuu, msianze kuchafua watu wanapoonfoka chamani. Watafteni na hawa 100 kabla hawajaondoka.
Hapo No.5, unataka kumaanisha nini unaposema ni kijana mwaminifu, mpole, mlokole na wakati huohuo unasema tena features zake ni sawa na Nyaradu huyu anayetuhumiwa mpaka na tuhuma za UFUSKA au?
 
Back
Top Bottom